Skip to main content

Walimu watakiwa kuepuka habari potofu za uundwaji wa mfuko mmoja wa jamii.



Walimu watakiwa kuepuka habari potofu za uundwaji wa mfuko mmoja wa  jamii.
Walimu  wametakiwa  kuondokana na dhana potofu kuwa uundwaji kuwa  mfuko wa  jamii mmoja utawapunja mafao yao baada ya kustaafu inayowasababisha kuomba kustaafu  kwa  hiari.
Hatua hiyo imekuja baada ya wimbi kubwa la walimu kuomba  kustaafu kwa hiari kutokana na habari za uongo za mitandaoni zinazoeleza endapo utaundwa mfuko huo mafao yao yatapunjwa.


Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu  wa Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania, Winfrida Rutahindwa  katika  Mkutano uliowakutanisha Maofisa  elimu, walimu na Wakuu wa Shule za Manispaa ya Ilala.



Amesema idadi kubwa ya walimu wamekuwa wakiomba kustaafu sababu ya habari za uongo zinazosambazwa na kwamba mfuko huo utakapoundwa utawasaidia kuwaborshea maslahi ya mafao yao.
“Wimbi kubwa la walimu wanastaafu kwa hiari kuogopa kupunjwa mafao kisa mchakato wa kuundwa mfuko mmoja wa jamii nawaombeni muwe na subira serikali inafanya jambo  jema la kuwanufaisha,”amesema.

Amewataka walimu kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria na taratibu za utumishi wa umma na kwamba kufanya hivyo kutasaidia kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Amewasisitiza maofisa elimu na wakurugenzi kuwahudumia vizuri pale wanapowasilisha changamoto zao na kwamba kuwanyanyasa kutasababisha matokeo mabaya ya wanafunzi.

Amewakumbusha wakuu wa vyuo nchini kutopokea walimu ambao hawajawasilisha barua za ruhusa ya masomo  na kuwataka walimu kufundisha kwa bidii..

Comments