Skip to main content

Piatia hapa kilicho semwa na Simba Alhamisi

IMBA awamu hii haitaki masikhara kabisa. Unaambiwa  Alhamisi mashindano ya Kombe la SportPesa yalizinduliwa rasmi ambapo bingwa wake atatua jijini Liverpool kukipiga na Everton ya Theo Walcott.
Sasa mabosi wa Simba fasta tu wakachukua simu na kuwaambia nyota wao kuwa kuna fedha ndefu zinawahusu endapo watakamilisha kazi hiyo.

Mbali ya kwenda kucheza Everton ambayo staa wa zamani wa Arsenal, Walcott na nahodha wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney wanaichezea, bingwa wa michuano hiyo atazawadiwa Dola 30,000 (Sh 68 milioni).

Mabosi wa Simba ambao wametumia zaidi ya Sh3 bilioni msimu huu, wamewaambia nyota wao wakiwamo Emmanuel Okwi na John Bocco waliofunga mabao 34 Ligi Kuu Bara, kuwa wakitwaa taji hilo watagawana zawadi hiyo kwani wao wanataka heshima ya kwenda England kukipiga na watani hao wa jadi wa Liverpool.

Mashindano hayo yatakayofanyika kuanzia Juni 3 hadi 10 nchini Kenya, yatahusisha timu za Simba, Yanga, Singida United na JKU ya Zanzibar kutoka Tanzania.

Nyingine zinazotarajiwa kushiriki ni za wenyeji Kenya ambazo ni Gor Mahia, AFC Leopards, Kariobangi Sharks na Kakamega Homeboys. Wawakilishi wa Simba na Yanga, Said Tully na Charles Mkwassa, walithibitisha kuwa lazima wapeleke nyota wao wote tofauti na msimu uliopita ambapo, walichezesha timu za vijana.

“Kama timu tumejiandaa na tupo tayari kuhakikisha tunalinda heshima ya Simba na Tanzania kwa ujumla. Tutakwenda na kikosi kamili ili kuendeleza ubabe kama tulivyofanya msimu huu kwenye ligi,” alisema Tully aliyeongozana na Ofisa Habari wao, Haji Manara.

Naye Manara alisema: “Fedha za ubingwa zitakwenda kwa wachezaji endapo wataifanya kazi hiyo kwa ukamilifu. Tunataka heshima, pesa watagawana.”

Kwa upande wake Mkwasa alisema: “Tulikuwa tukisumbuliwa na majeraha kwa baadhi ya wachezaji muhimu ndio maana tuliteleza, hii ni nafasi nyingine kwenda kutwaa ubingwa huo ili tucheze na Everton.”

Mbali ya bingwa kujizolea dola 30, 000, timu zitakazoshika nafasi ya pili na tatu zitapata kifuta jasho cha dola 7,500 na dola 5,000 (Sh16 milioni na Sh 11 milioni). Kabla ya mashindano hayo kila timu itapewa dola 10,000 (Sh22 milioni) kwa ajili ya maandalizi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.