Skip to main content

Simba kuwatema mastaa kibao msimu ujao


Kocha Mfaransa Pierre Lechantre, amepanga kufumua kikosi chake na kukisuka upya kwa mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.


Katika mkakati huo, Lechantre anatarajia kuwatema wachezaji zaidi ya saba ili kutoa nafasi kwa wapya kusajiliwa.
Simba inatarajiwa kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu.
Hata hivyo, Lechantre atakuwa na uhakika wa kutimiza ndoto yake endapo klabu ya Simba itamuongeza mkataba mpya.
Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema mkataba wa Lechantre unatarajiwa kujadiliwa na Kamati ya Utendaji baada ya kumalizika mechi za Ligi Kuu Jumatatu wiki ijayo.
Akizungumza jana, Lechantre alisema anataka kuisuka Simba iwe na nguvu ya kushindana na miamba mingine ya soka Afrika katika mashindano ya kimataifa, hivyo atalazimika kuwatema baadhi ya wachezaji maarufu.
Panga la wachezaji saba linatarajia kuwapitia Juuko Murshid, Laudit Mavugo, Juma Liuzio, Jamal Mwambeleko, Mwinyi Kazimoto, Mohammed Ibrahim na Nicholas Gyan.
Kazimoto, Mavugo na Ibrahim mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huu na uwezekano wa kuongezwa ni mdogo wakati Gyan licha ya kucheza mara kwa mara anatarajiwa kutolewa kwa mkopo.
Lechantre alisema baadhi ya wachezaji hakuridhika na viwango vyao tangu alipoanza kazi Simba na ametoa baraka kutolewa kwa mkopo au kuachwa.
“Wachezaji wote ni wazuri lakini uwezo wao unazidiana, kuna baadhi ambao nitawaambia kama wamepata timu za kucheza ruksa kuondoka, wameshindwa kupata nafasi na viwango vyao vitapotea,” alisema Lechantre.
Lechantre alisema anataka washambuliaji wawili, beki wa kati na kulia, kiungo mkabaji na winga mmoja ambao watakuwa na tija katika program yake.
“Mkakati wangu kuwa na wachezaji 11 bora ambao wataanza katika kikosi cha kwanza, pia nataka watakaokuwa benchi wawe na uwezo kama walioanza kikosi cha kwanza,” alisema Lechantre.
Gharama
Msimu huu Simba ilitumia Sh1.3 bilioni katika usajili wa wachezaji 14, ambao ni Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima, Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, John Bocco, Yusuph Mlipili, Salum Mbonde, Said Mohammed, Emmanuel Mseja, Ally Shomari, Jamal Mwambeleko, Poul Bukaba na Nicholas Gyan.
Thamani ya usajili iliongezeka katika dirisha dogo, baada ya kumpata beki Mghana Asante Kwasi kutoka Lipuli na kwa ujumla wao ndio walioipa ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.