Skip to main content

TIC : Cha jipambanua katika jitihada zake za kutangaza fursa za uwekezaji

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey
Mwambe amefanya ziara ya kikazi nchini Ujerumani na Uholanzi kati ya 
Mei 14 na 17 mwaka huu katika jitihada zake za kutangaza fursa 
za uwekezaji  ili kushawishi na kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza nchini.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji  Tanzania Bw. Geoffrey Mwambe (kulia) alipomtembelea  Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mhe. Dkt. Possi Abdallah ofisini kwake Berlin, Ujeruman
  
Akiwa nchini Ujerumani Bw. Mwambe alisema lipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini
Ujerumani Mhe. Dkt. Possi Abdallah ambapo walifanya kikao cha kazi kabla 
ya kushiriki kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Ujerumani na nchi
za Afrika Mashariki lililofanyika Mei 15, 2018 katika mji wa Berlin.

Pichani  baada ya kukamilisha zoezi la kusaini MOC . waliokaa kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe na kushoto ni Mwenyekiti wa DCIB Bw. Hans Biesheuvel. Pamoja nao kulia ni Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji wa TIC Bw. John Mnali,Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe. Irene Kasyanju,Mkurugenzi Mkuu wa DCIB Dkt Dewanand Mahadew na Bi Zeinab Dauda Meneja wa DCIB Afrika Mashariki.


Alisema Kongamano hilo liliandaliwa ili kutoa nafasi kwa nchi za ukanda wa Afrika 
Mashariki kunadi fursa za uwekezaji kwa wafanyabiashara wa Ujerumani
na dunia kwa ujumla. 


Vilevile siku mbili baada ya kongamano, Kituo kilifanya ziara nchini Uholanzi ambapo kilifanikiwa kusaini makubaliano ya mashirikiano (MOC) na Taasisi ya 
Biashara za Kimataifa ya Uholanzi (DCIB) pamoja na kufanya mkutano na baadhi 
ya wafanyabiashara wa Taifa hilo wenye nia ya kuja kuwekeza nchini. 

Sekta zitakazohusika ni pamoja na mafuta, gesi, kilimo, afya, usafirishaji, 
viwanda, fedha, mazingira, nishati na mawasiliano. 

Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Bw. Geoffrey Mwambe alipomtembelea Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju ofisini ,The Hague,  Uholanzi.
"Kupitia kongamano hilo niliwezakuelezea majukumu ya Kituo,msaada unaotolewa
kwa wawekezaji katika kuanzisha miradi, hali ya uchumi na mikakati mbalimbali
inavyotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi mahiri wa 
Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli  kwa lengo la kuboresha mazingira
ya biashara na uwekezaji ili kuvutia uwekezaji wa mitaji ya kutoka nje (FDI),
"alisema Bw. Mwambe.

Akiainisha baadhi ya maeneo ambayo yanafanyiwa kazi na Serikali alisema kuwa ni 
pamoja  na kuweka mazingira wezeshi ya usajili wa biashara na leseni kwa wawekezaji
wa ndani na nje pamoja na kuondoa urasimu ndani ya mifumo ya Serikali kuanzia ngazi
ya Mtaa/Kijiji hadi Taifa ili kufanikisha utekelezaji wa miradi ya uwekezaji kwa 
muda mfupi. 

Bw. Mwambe alisema pia aliwahakikishia wawekezaji wa nchini Ujerumani na Dunia kwa ujumla
kuwa Tanzania ni nchi yenye fursa nyingi na mahali salama kwa uwekezaji ndani ya 
Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika;  hivyo wawekezaji wenye mitaji na teknolojia
wanakaribishwa kuja kuwekeza kwenye sekta mbalimbali  ambazo kwa sasa ni kipaumbele
cha Taifa yaani viwanda, kilimo, madini, mifugo, uvuvi, miundombinu,
uzalishaji na usambazaji umeme na miundombinu kwa ujumla. 



Nae mwakilishi wa Benki ya Stanbic kwa Kanda ya Afrika Mashariki Bw. Jibran
Qureishi alieleza kuwa kwa sasa Tanzania inafanya vizuri katika masuala ya 
Kiuchumi ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Matokeo 
hayo chanya ni kutokana na uongozi mahiri wa Mheshimiwa Rais Dkt.John Pombe
Magufuli aliyeanzisha vita ya kupambana na rushwa; na kupunguza
urasimu kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji.

Bw. Qureishi ambaye ni mchumi mbobezi aliweka bayana kwamba Tanzania ina 
nafasi kubwa ya kuendelea kufanya vizuri zaidi katika nyanja ya uchumi kwa 
miaka ya hivi karibuni baada ya kukamilika kwa miradi mikubwa ya maendeleo 
inayotekelezwa  na Serikali kwa kutumia rasilimali  za ndani na sio mikopo
kama ilivyokuwa imezoeleka. 

Akitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni mradi wa kuzalisha umeme wa Stiegler's 
Gorge, ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma na upanuzi
wa bandari. Kwa ujumla ziara ya Kituo nchini Ujerumani na Uholanzi
imekuwa ya manufaa yenye manufaa .


"kwa upande wa Ujerumani tumekutana na makampuni ambayo yameonesha nia ya 
kuwekeza kwenye sekta za viwanda, afya, ujenzi, miundombinu, mawasiliano, 
usafirishaji na nishati,pili kuanza kwa utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano
kati ya Kituo na Taasisi ya Biashara za Kimataifa ya Uholanzi kunatoa fursa ya 
kutekelezwa masuala mbalimbali kwenye miradi ya ubia, upatikanaji wa fedha za
miradi, uhamishaji wa teknolojia na ujuzi, kuandaa semina au warsha na misafara
ya wawekezaji,"alisema Bw. Qureishi.


Alisema pia kituo kinatarajia kupokea kundi la kwanza la wafanyabiashara 
kutoka Uholanzi mapema mwaka 2018 hadi 2019 na jambo la tatu  kwa upande wa 
Uholanzi wamekutana na makampuni yaliyoonesha nia ya kuwekeza kwenye sekta 
za utalii, ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza spea za magari, uanzishaji wa
chuo cha mafunzo ya ufundi (Vocational Training), uanzishaji wa mradi wa
usimamizi wa usalama wa mizigo kuanzia bandarini mpaka eneo husika na usimikaji
wa mitambo ya kutengeneza bidhaa mbalimbali za ngano.


Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju amesema
kusainiwa kwa makubaliano kati ya TIC na DCIB ni hatua kubwa ambayo itarahisisha
utekelezaji wa sera, diplomasia ya uchumi. Mhe. Balozi amehitimisha kwa kuhimiza
wadau wa sekta binafsi ya Tanzania kutumia vema makubaliano hayo kama fursa ya 
kuongeza biashara na uwekezaji kwa kushirikiana na wadau kutoka Uholanzi.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.