Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2012

WALIMU WAGOMA KILA KONA, WANAFUNZI NAO WACHACHAMAA, SERIKALI YAONYA, YATISHIA KUWAFUTIA MISHAHARA

Waandishi Wetu   NCHI imetikiswa. Mgomo wa walimu ulioanza jana katika sehemu mbalimbali nchini, umeathiri kwa kiasi kikubwa sekta ya elimu huku kukiwa na taarifa za matukio yasiyokuwa ya kawaida yaliyoambatana na mgomo huo usio na ukomo. Katika sehemu mbalimbali nchini, walimu waliripotiwa kugoma kwa kutoingia madarasani na wengine walifika kazini na kusaini vitabu vya mahudhurio kisha kuondoka hali iliyosababisha wanafunzi kurandaranda ovyo katika sehemu za miji iliyo karibu na shule hizo. Mjini Dodoma ,wabunge jana walimbana Naibu Spika, Job Ndugai wakitaka shughuli za Bunge zisitishwe ili kujadili mgomo wa walimu ambao umeanza rasmi jana nchi nzima, na kuziacha shule nyingi zikiwa na walimu wakuu na wakuu wa shule pekee. Hata hivyo, Ndugai alisema Bunge lisingeweza kujadili suala hilo kwani tayari Serikali ilikuwa imelifikisha mahakamani baada ya kushindwa kuafikiana na walimu katika ngazi ya usuluhishi.Wakati hayo yakiendelea, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru

YANGA BINGWA WA KOMBE LA KAGAME

Wachezaji wa Yanga wakiwa na kombe la ubingwa wa michuano hiyo jana kwenye dimba la Taifa Dar es Salaam. Wachezaji wa Yanga na Azam wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa CECAFA.Inatoka kwa mudau.

JOSE CHAMELEONE AVAMIA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UGANDA, ASHINIKIZA AREJESHEWE PASIPOTI YAKE

Chameleone akiteta jambo na mmoja kati ya wafuasi wake nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda. Chameleone akipiga gita huku wafuasi wake wakiwa wamebeba mabango nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda. Polisi wa Uganda wakimtuliza Chameleone na wafuasi wake wakati walipofanya maandamano ya amani nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda. Ofisa mmoja wa polisi akizungumza na wafuasi wa Chameleone nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda. Mwanamuziki Jose Chameleone na wafuasi wake sikuchache zilizopita  wapovamia kwenye ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda na kushinikiza arejeshewe pasi yake ya kusafiria. Jose, mmoja wa wanamuziki tajiri katika nchi za ukanda wa Afrika, aliendesha gari lake aina ya Range Rover Sport na kuliegesha karibu na ubalozi huo. Mwanamuziki huyo pamoja na wafuasi wake walikuwa na mabango yaliyokuwa na maandishi yanayomtaka mfanyabiashara Eric Shigongo arejeshe hati yake ya kusafiria. J

SHIGONGO AJIBU MAPIGO YA CHAMELEONE

Mkurugenzi wa Global Publishers, Eric Shigongo(kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya sakata lake na Chameleone. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho. MD wa Global Publishers Ltd, Eric Shigongo, mapema juzi ameongea na media kuhusu madai ya Jose Chameleone kudai paspoti yake, ambaye  alikwenda Ubalozi wa Tanzania nchini kwake Uganda kushinikiza kurejeshewa paspoti yake. Eric alifunguka kwa kusema kuwa, kampuni yake na msanii huyo waliingia makubaliano ya kufanya shoo kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini, liliofanyika Uwanja wa Taifa Julai 7 mwaka huu, ambapo katika mazungumzo ya awali, msanii huyo aliomba kulipwa dola 5000 na kulipiwa tiketi 2 za ndege ili kuhudhuria tamasha hilo, masharti ambayo yalikubaliwa. Mazungumzo hayo ya awali yalifanyika kati ya Global Publishers na agenti wa Chameleone ajuliikanae kwa jina la George. Kabla ya kutuma fedha hizo, kampuni yake ilihitaji kujiridhisha kama ajen

Ufunguzi Wa Mkutano Mkuu Maalum Wa Kumpata Mgombea Uwakilishi Jimbo La Bububu Zanzibar.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi Yussuf Mohd Yussuf akitoa hotuba ya Kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai ili kufungua Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Kumpata Mgombea Uwakilishi Jimbo la Bububu kufuatia Kifo cha aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo,Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Zanzibar. Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM waliohudhuria katika Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Kumpata Mgombea Uwakilishi Jimbo la Bububu kufuatia Kifo cha aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo,Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Zanzibar. Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM wakishangilia Hotuba ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai katika Ufunguzi wa Mkutano Mkuu Maalum wa Uchaguzi wa Kumpata Mgombea Uwakilishi Jimbo la Bububu kufuatia Kifo cha aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo hilo,Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Maruhubi Zanzibar. PICHA NA YUSSUF SIMAI-

MWEZI MTUKUFU: Machangu wala Kichapo na Viboko Vya Nguvu huko Kinondoni Ni Kutoka Kwa Kikundi Cha Jumuia Ya Uamsho Tanzania Bara!

Stori: Issa Mnally na Richard Bukos Machangu wamekiona cha mtemakuni! Wakati Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ukiwa katika chungu cha nane, akina dada wanaofanya biashara haramu ya kuuza miili maarufu kama Machangudoa au Chipsi Funga au Wauza Sukari Tamu, wamekula viboko laivu baada ya kutuhumiwa kuwatega Waislamu. Tukio hilo lilijiri katikati ya wiki hii ambapo vijana wa Kiislamu waliodai ni wa kikundi cha Jumuiya ya Uamsho Tanzania Bara walizunguka mitaa mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam na kuwashushia fimbo machangu ambao kwa sasa wametapakaa kila kona jijin WATUMIA BAJAJ Kwa mujibu wa shuhuda wetu, waumini hao, wakiwa wamevaa kanzu huku wakitembea na bakora mkononi walichukua  jukumu la kukodi Bajaj na kuzunguka maeneo mbalimbali jijini inapofanyika biashara hiyo haramu ya ukahaba. BARABARA YA SHEKILANGO Vijana hao waliolenga kukomesha biashara hiyo hasa kipindi hiki cha mfungo walianzia kwenye Barabara ya Shekilango inayok

UPDF sends 3,200 more troops to Somalia

The army has passed out a new battalion comprising of 3,237 specially trained troops for deployment against the al Qaeda-linked al-Shabaab terrorists in the war-torn Somalia. UPDF soldiers from Battle Group 10 carry out military exercises during a pass out ceremony at Singo This will be Uganda’s 10th battle group to be deployed in Somalia since the inception of the African Union (AU) peacekeeping mission (AMISOM) in 2007. The battle group 10 will replace battle group eight that will return home upon their arrival in Mogadishu. The troops, who completed a four-month course at Singo military centre in Nakaseke district on Friday, comprise of British and French trained snipers equipped with distinct martial skills. Other foreign trainers came from the Africa Contingency Operations Training and Assistance (ACOTA), which comprises of mainly retired UN servicemen and women. Passing out the team on Friday, Maj. Gen. Levy Karuhanga,

Frank Ocean: The Rosa Parks Of The Gay Hip-Hop Movement

by Chuck "Jigsaw" Creekmur   \ From here on, Caushun will forever be known as the Claudette Colvin of Hip-Hop. Caushun was unabashedly out when he was thrust upon the Hip-Hop community as one of the first rappers to be presented as openly gay and embraced by the powers that be. He was also covered heavily in the media as one that would have waved the rainbow flag inside the otherwise open doors on the House of Hip-Hop. As the story was told in the mid-2000s, he was signed to Baby Phat Records and touted through of the music elite’s insider parties. Russell and Kimora Lee Simmons took the fabulously flamboyant Caushun under their mighty marital wing and introduced him to the world. Jason Herndon, Caushun by his real name, has to be somewhere in the deep recesses of obscurity, stewing. Pissed. Crushed even. Frank Ocean stole his moment. Frank Ocean, when history is told and re-told, will be regarded as the Rosa Parks

WASANII WAKIKE NIGERI WENYE MAUMBO MAKUBWA NI DILI

KAMA ilivyo sehemu nyingi duniani, hata Nigeria sura za wasanii wa kike wenye maumbo makubwa ndizo hutawala kwenye kurasa za mbele za magazeti ya udaku na majarida ya burudani. Wasanii hao wanageuka gumzo la majiji kama Lagos na Abuja haswa inapotokea hafla kubwa hususani zile za usiku. Hii ni kutokana na maumbo yao makubwa ya mwili na jinsi wanavyopenda kuvaa nguo ambazo huacha wazi sehemu kubwa za miili yao haswa matiti. Mastaa hao wengi wao wamekuwa wakikiri hadharani kwamba si kitu cha ajabu kufanya hivyo kwani kila mmoja ana utaratibu wake wa kuvaa hasa kwenye matukio maalum ya usiku. Hivyo kwao kama kuna mapaparazi wanawafuatilia ni juu yao. Watajiju. Wengi wa wasanii hao huvaa saizi 12 au zaidi. Wakikupitia karibu lazima usisimke na ugeuke nyuma kuwaangalia hata mara tano. Ifeoma Okeke Ana mvuto halafu ni mpana, anajua kutinga staili za aina yake ambazo akipita lazima ugeuze shingo. Licha ya unene wake, lakini anaamini kwamba hana mpinzani kwenye

Tume ya kukusanya maoni ya Katiba yaendelea kukusanya maoni

Bi. Aziza Juma (27), mkazi wa Wilaya ya Kishapu, mkaoni Shinyanga akitoa akitoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipofanya mkutano kijijini hapo jana (Alhamisi, Julai 26, 2012) Wananchi wa Kijiji cha Maganzo, Kata ya Songwa, Wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wakifuatilia mkutano wa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya jana (Alhamisi, Julai 26, 2012) Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba katika picha ya kumbukumbu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Michungwani iliyopo kijiji cha michungwani, Kata ya Segera wilayani Handeni mkoani Tanga mara baada ya mkutano wa kukusanya maoni kuhusu Katiba Mpya.

ast Africa moves to curb cyber crimes

By JAMES GASHUMBA, EANA East Africa is fast-tracking the implementation of joint initiatives to combat the rising challenge of cyber crimes that threaten peace and stability in the region. Dr Bitange Ndemo. Photo/Nation Government officials say the region is vulnerable to a range of online criminal activities, including financial fraud, drugs human trafficking, and terrorism. “There is need to develop a common platform to address cyber security. As a region, we must begin to cooperate to deal with cyber threats atNational and regional levels,” Kenya’s Permanent Secretary in the Information Ministry Dr Bitange Ndemo said at an East African Internet Governance Forum in Nairobi, Kenya. Kenya has scaled up efforts to combat cyber crimes through a multi-stakeholder approach involving the government, industry and civil society organizations. “Kenya has a national cyber security steering committee hosted by the Communications Commission of Kenya (CC

Mh .KOMBA AREJEA KUTOKA INDIA

Kepteni John Komba akiwa na mkewe Salome, nyumbani kwake Mbezi, Dar es Salaam. MKURUGENZI wa Kundi la Tanzania One Theatre (TOT), ambaye pia ni Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba amerejea nchini kutoka India, ambako alikwenda kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kumtibu ugonjwa wa nyonga uliokuwa ukimsumbua upande wa mguu wake wa kulia. Akizungumza na waandishi wa habari leo, nyumbani kwake Mbezi kwa Komba, mjini Dar es Salaam, Komba alisema alirejea nchini juzi baada ya kupatiwa matibabu hayo kwenye hospitali ya Appolo iliyopo Hydrabad nchini India tangu mwanzoni mwa wezi huu. Komba alisema, aliondoka nchini Julai 2, 2012 baada ya kupelekwa na serikali kwa maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete, Spika wa Bunge Anna Makinda na Katibu wa Bunge John Kashilila na kwamba alikwenda baada ya kukosa matibabu hapa nchini kwa sababu ya mgomo wa madaktari.

NGASA AICHANGANYA AZAM

Ngasa akiondoka kwenye jukwaa la mashabiki wa Yanga baada ya kuzawadiwa jezi Mshambuliaji Mrisho Ngasa juzi alifanya vitendo vya ajabu wakati timu yake ya Azam ilipokuwa ikimenyana na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo katika mechi ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Kagame. Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Ngasa aliingia uwanjani kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Kipre Tchetche. Kituko chake cha kwanza ni kwenda kushangilia bao la pili aliloifungua Azam katika mechi hiyo kwenye jukwaa wanalokaa mashabiki wa Yanga. Muda wote wa pambano hilo, mashabiki hao walikuwa wakiizomea Azam, lakini baada ya mchezaji huyo kufunga bao na kuwafuata, walianza kumshangilia kwa mayowe mengi.

RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA AWASILI MKOANI RUVUMA

Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Joseph Mkirikiti akimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa katika uwanja wa ndege wa Songea. Meya wa manispaa ya Songea mstahiki Charles Mhagama akisamiana na rais mstaafu wa awamu wa tatu Mhe Benjamin Mkapas baada ya kutua mjini Songea Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Joseph Mkirikiti kushoto akimuongoza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa kwenda kuangalia vikundi vya ngoma katika uwanja wa ndege mjini Songea. Rais wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa akiangalia vikundi vya ngoma (havipo pichani) katika uwanja wa ndege wa Songea akiwa na kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe Joseph Mkirikiti. Katikati ni mwenyekiti wa CCM mkoa Cornel Msuha kulia ni mama Anna Mkapa na wa pili kulia mke wa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu Mama Afisa Mwambungu. PICHA NA MUHIDIN AMRI

WAZIRI WA UCHUKUZI DR HARRISON MWAKYEMBE AZINDUA HUDUMA MPYA ZA SHIRIKA LA NDEGE LA QATAR OTOKA KIA

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika hilo Bw. Marwan Koleilat kwa niaba ya shirika hilo la ndege la Qatar zawadi ya picha yenye kivuli cha Mlima Kilimanjaro . Mkurugenzi mtendaji wa masoko wa shirika la Qatar Bw. Marwan Koleilat kwa niaba ya shirika hilo akimpa Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison zawadi ya yenye nembo ya ndege ya shirika hilo la Qatar. Mgeni rasmi katika uzinduzi huo,waziri wa mawasiliano na uchukuzi Dr. Harrison akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakiwemo na wahariri wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani),mapema jana kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA.

RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA AWASILI MKOANI RUVUMA

Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Joseph Mkirikiti akimkaribisha Rais mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa katika uwanja wa ndege wa Songea. Meya wa manispaa ya Songea mstahiki Charles Mhagama akisamiana na rais mstaafu wa awamu wa tatu Mhe Benjamin Mkapas baada ya kutua mjini Songea Kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Joseph Mkirikiti kushoto akimuongoza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa kwenda kuangalia vikundi vya ngoma katika uwanja wa ndege mjini Songea. Rais wa awamu ya tatu Mhe Benjamin Mkapa akiangalia vikundi vya ngoma (havipo pichani) katika uwanja wa ndege wa Songea akiwa na kaimu mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mhe Joseph Mkirikiti. Katikati ni mwenyekiti wa CCM mkoa Cornel Msuha kulia ni mama Anna Mkapa na wa pili kulia mke wa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu Mama Afisa Mwambungu. PICHA NA MUHIDIN AMRI

Busta Rhymes to Release Free Album ‘Year of the Dragon’ in August

Busta Rhymes Busta Rhymes is giving the people what they want. During his appearance on “106 & Park,” the Cash Money rapper made a big announcement regarding his next studio album, Year of the Dragon . Instead of a conventional release, he plans to distribute it for free through Google’s online music store , Google Play. “The Year of the Dragon album is not my Cash Money debut, this is my Google album and this album is going to be given to everybody for free,” said the rap veteran . “Google Play is where the album is going to be available.” Due in mid-August, the follow-up to 2009’s Back on My B.S. will include collaborations with Lil Wayne, Rick Ross, Trey Songz, Robin Thicke, Maino, and Gucci Mane .

Kaburu anahatia kupanga kumuua Mandela

Mtu aliyepanga njama za kutaka kumuuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amepatikana na hatia. Mahakama ya Pretoria ilimpata kiongozi wa kundi la -Boeremag linaloamini kuwa mtu mweupe ni bora alipatikana na hatia ya kupanga kummua Mandela mwaka 2002. Bwana Mike du Toit ndiye aliyepanga milipuko tisa katika eneo la Soweto mjini Johannesburg mwaka 2002. Kiongozi huyo wa kundi la ki-baguzi ni mtu wa kwanza kupatikana na hatia tangu utawala wa wengi uanze mwaka 1994 Afrika kusini. Wachanganuzi wanasema kuwa bado kuna hali ya kutopendana katiki ya watu wa rangi tofauti nchini Afrika kusini. Hata hivyo kundi kama la Boeremag,inayomaanisha Nguvu za Makaburu miongoni mwa Makaburu ,halina ufuasi mkubwa. Mahakama hiyo ya Pretoria imempata Du Toit, ambaye alikuwa msomi baada ya kusikiliza kesi hiyo kwa miaka tisa.

MAKAMBA AMJIBU ZITTO KUHUSU ON MOBILE

NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia jana alimuumbua mbunge wa Kigoma Kaskazini Zuberi Zitto kuwa serikali ilishaisimamisha kampuni ya Onmobile kuendelea kufanya kazi toka mwezi Juni mwka huu. Alisema serikali iliamua kuisimamisha kampuni hiyo kuendelea kufanya kazi baada ya kampuni hiyo kuandika barua ya kuomba leseni. Makamba alisema baada ya serikali kuipokea barua hiyo tarehe 29 february mwaka huu iliijibu barua hiyobaada ya kubaini mapungufu mbalimbali katika maombi hayo. Naibu huyo alisema baadhi ya mapungufu hayo ni pamoja na kampuni hiyo kutosajiliwa BRELA na kutoa mchanganuo wa kibishara. Hata hivyo, alisema baada ya serikali kugundua kuwa pamoja na kuomba leseni pia kampuni hiyo ilikuwa ikiendelea kufanya kazi kupitia kampuni za Vodacom na Airtel Alisema hivyo hoja iliyotolewa na Zitto kuwa kampuni hiyo inafanya kazi bila leseni ilishagunduliwa na serikali na kuchukuliwa kwa hatua. Akizungumzia kuhusiana na wizi wa kazi za wasanii, Makamba alisema serikali

MILOVAN ALALAMIKIA MAANDALIZI SIMBA

KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic amesema kutolewa mapema kwa timu yake katika michuano ya Kombe la Kagame kumechangiwa na maandalizi hafifu. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 3-1 na Azam juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kocha huyo alisema Simba haikufanya maandalizi ya kutosha kabla ya kushiriki michuano hiyo. Milovan alikiri kuwa kikosi chake bado dhaifu kutokana na kuundwa na wachezaji wengi wapya na pia wachezaji wake bado hawajaweza kucheza kwa uelewano mkubwa. Alisema alishalibaini tatizo hilo kabla hata ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Kagame na alishawaeleza mapema viongozi wa klabu hiyo. “Bado sina kikosi kizuri, ambacho unaweza kujivunia wakati unashiriki katika michuano migumu kama hii," alisema. Milovan alisema licha ya timu yake kutwaa ubingwa wa Kombe la Urafiki kwa kuifunga Azam kwa njia ya penalti, bado hajaweza kuunda kikosi imara na chenye ushindani. “Lazima timu ipate maandalizi ya kutosha kabla y

Somalia lazima imalize kipindi cha mpito

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema Somalia ni lazima imalize kipindi cha mpito katika tarehe iliyopangwa, huku likionyesha wasiwasi mkubwa kutokana na muda huo kuzidi kuelekea ukingoni. Baraza hilo limeitaka serikali ya mpito pamoja na viongozi wa siasa nchini Somalia kuongeza juhudi na kutimiza matakwa yote yanayotakiwa kufikia tarehe 20 mwezi ujao (Agasti) ambao ndio muda wa mwisho uliopangwa. Somalia imekuwa na serikali ya mpito tangu mwaka 2004 lakini haijapata serikali kamili tangu mwaka 1991. Baraza la usalama lilitangaza tarehe hiyo mwezi Februari na kutoa wito kwa pande zote kutimiza makubaliano hayo yenye lengo la kuimarisha hali ya usalama, kuunda serikali kuu, pamoja na kuandika katiba. Baraza hilo limeukaribisha mkutano wa bunge uliofanyika jana. Bunge la Katiba la Somalia lilikutana mjini Mogadishu hapo jana baada ya kuwa limeahirishwa mara kadhaa huko nyuma. Kikao cha kwanza cha Bunge Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Abdullahi Osman, amesema kuwa wajumb

Zitto Kabwe aug’ang’ania urais 2015

NA THOBIAS MWANAKATWE Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, ameung’ang’ania urais kwa kusema kama urais upo utakuja tu na kwamba hana mashaka na uwezo, uadilifu, uzalendo wake pamoja na kuwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama. Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, ametoa kauli hiyo siku chache, baada gazeti moja (siyo NIPASHE) kuandika kuwa wabunge wawili wa Chadema wamemsafishia njia ya kugombea kiti hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. Hata hivyo, juzi ikiwa ni siku moja baada ya kuchapishwa kwa habari hiyo, wabunge hao ambao ni Joshua Nassari (Arumeru Mashariki na Halima Mdee (Kawe) walitoa taarifa katika vyombo vya habari za kutoa kauli za kukanusha na kujiweka mbali na mpango wa kumpigia debe Zitto. Zitto alitoa kauli hiyo bungeni jana wakati akichangia makadiro ya mapato na matumizi ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa fedha 2012/13. “Ndugu zangu wasanii, najua kuwa suala la tamasha la Kigoma limeleta maneno

Mtoto wa Rambo Afariki Dunia

LOS ANGELES, Marekani MCHEZA filamu nyota wa Marekani, Sylvester Stallone ‘Rambo’ juzi aliwaongoza ndugu na jamii katika mazishi ya mtoto wake, Sage. Sage (36) alifariki dunia wiki iliyopita kwa kile kinachodaiwa kuwa ni utumiaji uliokithiri wa dawa za kulevya. Ibada ya mazishi ya Sage ilifanyika katika kanisa la St Martin lililopo Brentwood na mazishi yake yalifanyika katika makaburi ya Westwoodmjini Los Angeles. Muda wote wa ibada na mazishi ya mtoto huyo, Rambo alionekana akitokwa na machozi. Rambo (66) alikuwa amevaa suti nyeusi, tai nyeusi na shati jeupe. Pia alikuwa amevalia miwani myeusi. Katika mazishi hayo, Rambo alikuwa ameongozana na mke wake wa sasa, Jennifer Flavin. Mke wa zamani wa Rambo na mama wa Sage, Sasha Czack naye alikuwepo kwenye mazishi hayo pamoja na mtoto mwingine wa mcheza filamu huyo, Frank. Mashabiki mbali mbali wa Rambo pia walishiriki katika mazishi hayo wakiwa wamebeba maua na picha zake pamoja na za Sage. Sage alikuwa akiwa amekufa nyumbani kwake

Simba yatupwa nje Kombe la Kagame, yapigwa 3-1 na Azam

SIMBA leo imetolewa katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuchapwa mabao 3-1 na Azam katika mechi ya robo fainali iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mshambuliaji John Bocco ndiye aliyeibuka shujaa wa Azam baada ya kuifungia mabao yote matatu, moja kipindi cha kwanza na mengine kipindi cha pili. Bao pekee la Simba lilifungwa na Shomari Kapombe. Ushindi huo umeiwezesha Azam kutinga nusu fainali, ambapo sasa itakutana na AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Vita imefuzu kucheza hatua hiyo baada ya kuitoa Atletico ya Burundi mabao 2-1 katika mechi iliyochezwa kuanzia saa nane mchana. Mechi nyingine ya nusu fainali itazikutanisha Yanga na APR ya Rwanda. Yanga imetinga hatua hiyo baada ya kuitoa Mafunzo ya Zanzibar kwa penati 5-3 wakati APR iliitoa URA ya Uganda kwa mabao 2-1. Kwa mujibu wa ratiba, mechi zote mbili za nusu fainali zitachezwa Alhamisi wiki hii. Mechi ya kwanza itazikutanisha Azam na APR wakati katika mechi ya pili, Yanga itavaana na