Skip to main content

Cheo cha Ofisa Habari chafutwa ZFA

CHAMA cha Soka cha Zanzibar (ZFA) kimemuondoa msemaji na ofisa wake wa habari, Munir Zakaria kwa madai kuwa, cheo hicho kimefutwa.
Uamuzi wa kufutwa kwa cheo hicho ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya chama hicho kilichofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye hoteli ya Ocean View mjini hapa.
Katika kikao hicho kilichoongozwa na rais mpya wa ZFA, Amani Makungu, wajumbe walifikia uamuzi wa kukifuta cheo hicho kwa vile hakimo kwenye katiba.
Katibu Mtendaji wa ZFA, Kassim Haji Salum alisema juzi mjini hapa kuwa, uteuzi wa ofisa habari ulifanyika kimakosa katika uongozi uliopita kwa vile cheo hicho hakimo kwenye katiba.
Salum alisema kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, msemaji mkuu wa masuala mbalimbali yanayoihusu ZFA ni rais wake kwa kushirikiana na katibu mkuu.
"Kwa mujibu wa katiba yetu, rais anazo nafasi nne za kufanya uteuzi wa watu wa kumsaidia kazi, lakini hakuna nafasi ya ofisa habari. Kazi ya kukisemea chama ni ya rais kwa kushirikiana na katibu mkuu", alifafanua.
Hata hivyo, Salum alisema Zakaria ataendelea kuwa mjumbe wa kawaida wa kamati ya utendaji ya ZFA kwa vile uteuzi wake ulifuata katiba.
“Kwa sasa tumeamua kufanya kazi zetu kikatiba zaidi na kufutwa kwa cheo cha ofisa habari ni utekelezaji wa mkakati wetu huo,”alisema.
Uchunguzi uliofanywa na Burudani umebaini kuwa, kuondolewa kwa Zakaria katika nafasi hiyo kulitokana na kauli yake kwa vyombo vya habari kwamba, iwapo Simba na Azam zitafuzu kucheza fainali ya michuano ya Kombe la Urafiki, mechi hiyo itachezwa Dar es Salaam badala ya Zanzibar.
Imedaiwa kuwa, Zakaria alitoa kauli hiyo bila kupata idhini kutoka kwa viongozi wa chama hicho pamoja na waandaaji wa mashindano hayo.
Kauli hiyo iliwakera wadau wa michezo visiwani Zanzibar, ambao wamekuwa wakihoji iweje fainali hiyo ihamishiwe Dar es Salaam katika hatua ya mwisho wakati mechi zote za mwanzo zilichezwa kwenye Uwanja wa Amaan.
Katika hatua nyingine, ZFA imemteua Suleiman Mahmoud Jabir kuwa mkurugenzi mpya wa ufundi wa chama hicho wakati Abdalla Juma Mohamed ameteuliwa kuwa mwanasheria wa chama.
Salum alisema juzi kuwa, kazi za mkurugenzi huyo wa ufundi ni kupanga programu za maendeleo ya soka kwa timu za madaraja yote na pia mitaala ya mafunzo ya soka kwa waamuzi, makocha na viongozi wa klabu.Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.