Skip to main content

Balozi Seif awataka Waumini wa Dini ya Kiislamu pamoja na Wazazi kujenga Misingi ya Maadili imara


Na Othman Khamis Ame

Waumini wa Dini ya Kiislamu pamoja na Wazazi wanahitajika kuendelea kujenga Misingi ya Maadili imara ambayo inaonekana kulega lega hasa kwa Vijana kunakosababishwa na Mambo tofauti likiwemo la kukua kwa Mawasiliano ya Sayansi na Teknolojia Duniani.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati akiiungua Ijitimai ya 17 ya Kimataifa inayofanyika katika majengo ya Jumuiya ya Fiy Sabilillah Tablih Markaz Fuoni Migombani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Balozi Seif alisema Watanzania wengi hasa Vijana wamekuwa wakijijengea Utamaduni wa kuiga maadili mabovu badala ya kufanya mema ambayo yanakwenda kinyume na Mila, Silka na hata Taratibu za Dini.

Balozi Seif alitoa rai kuwa pamoja na mada nyengine zilizoandaliwa katika Ijitimai hiyo ni vyema kwa wahadhiri watakaopata fursa waitumie hadhara hiyo kujadili kwa kina mbinu zitakazosaidia kurejesha maadili mema miongoni mwa Vijana Nchini.

Makamu waPili wa Rais wa Zanzibar alitahadharisha kwamba mmong’onyoko wa maadili ni tishio kwa Ustawi wa Taifa lolote lile hapa Duniani.

“Siku hizi si jambo la ajabu kukutana na kundi la Vijana wa Kiislamu wanatumia dawa za kulevya zinazopelekea kujiingiza katika vitendo viovu”. Alitanabahisha Balozi Seif .

Akikumbusha suala la umuhimu wa Waislamu kufanya kazi, Balozi Seif alisema hakuta kuwa na njia ya mkato wa kuendesha afamilia bila ya kufanya kazi kwa bidii.

Alisema Uislamu kupitia Kitabu kitukufu Qurani sdambamba na Hadithi zake imesisitiza umuhimu wa kufanya kazi za halali ili kuwa na sababu ya kujipatia chumo la halali.

Balozi Seif alikariri moja ya Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Kiongozi wa Dini ya Kiislamu Mtume Muhammad { SAW } ikisema chumo bora ni lile mja alichumalo kwa mikono yake.

“ Tabia iliyojengeka katika Jamii yetu ya ubadhirifu wa Mali za Umma tukumbushane kuwa tabia hiyo haifai na tuachane nayo mara moja”. Alitahadharisha Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwahakikishia waumini wa dini zote Nchini kwamba Serikali itaendelea kuheshimu uhuru wa kuabudu kwa kushirikiana na Taasisi zote za Kidini Nchini kwa lengo la kustawisha Jamii yote.

Alisema Katiba ya Nchi ijnaeleza wazi kwamba kila mtu ana haki ya kuabudu dini aitakayo mradi havunji sheria za Nchi.

Kuhusu suala la Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaomba Viongozi wa Dini zote kuhamasisha wafuasi wao kushiriki kikamilifu katika zoezi la kuhesabiwa linalotarajiwa kufanyia usiku wa kuamkia tarehe 26 Agisti Mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...