Skip to main content

SIMBA, AZAM ZAGOMA KUCHEZA AMAAN, FAINALI YAHAMISHIWA DAR






MECHI ya fainali ya michuano ya soka ya Kombe la Urafiki kati ya Simba na Azam imehamishwa kutoka Uwanja wa Amaan, Zanzibar kwenda Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo, ambayo awali ilikuwa ichezwe kesho kwenye Uwanja wa Amaan, sasa itachezwa Alhamisi kwenye Uwanja wa Taifa.

Katibu wa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo, Suleiman Jabir aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam leo kuwa, uamuzi huo umefikiwa kutokana na timu hizo mbili kugoma kucheza uwanja wa Amaan.

Jabir amewaomba radhi mashabiki wa soka wa Zanzibar kutokana na fainali hiyo kuhamishiwa Dar kwa madai kuwa, jambo hilo lipo nje ya uwezo wao.

Awali, Simba na Azam ziligoma kucheza fainali hiyo kwenye Uwanja wa Amaan kwa madai kuwa ni mbovu na umesababisha kuumia kwa baadhi ya wachezaji wao.

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' aliwaambia waandishi wa habari kuwa, eneo la kuchezea soka kwenye uwanja huo ni bovu.

Kaburu alisema wapo tayari kucheza fainali hiyo kwenye uwanja wowote, lakini si Uwanja wa Amaani.

Alisema waliwasilisha malalamiko hayo kwa waandaaji kwa muda mrefu, lakini hawakuweza kuyafanyia kazi.

Kaburu alisema kutokana na timu yake kushiriki kwenye michuano ya Kombe la Kagame, wana hofu wachezaji wao wanaweza kuumia zaidi kwenye mechi hiyo.

Aliwataja wachezaji wa Simba walioumia tangu kuanza kwa michuano hiyo kuwa ni Lino Masimbo, Salim Kinje na Mussa Mudde.

Meneja wa Azam, Patrick Setter alisema klabu yake inawapenda na kuwaheshimu mashabiki wa Zanzibar, lakini kutokana na hali ya uwanja wa Amaan, hawawezi kucheza mechi ya fainali visiwani humo.

“Tupo tayari hata kwenda kucheza Pemba ama kwingine kokote, lakini sio hapa Amaan. Hofu yetu ni wachezaji wetu wengi zaidi kuumia,"alisema.

Kwa mujibu wa Patrick, wachezaji wa Azam walioumia tangu kuanza kwa michuano hiyo ni Michael Kipre, Jabir Azizi na Kipre Tchetche.

Alisema hawagomi kucheza mechi hiyo Uwanja wa Amaan kwa sababu ya maslahi, bali wanajali zaidi afya za wachezaji wao.

Rais wa ZFA, Amani Makungu alisema wapo tayari kupokea lawama kutoka kwa wapenzi wa soka wa Zanzibar, lakini hawana la kufanya.

Alisema walikuwa wakifikiria kuihamishia mechi hiyo Uwanja wa Gombani, Pemba lakini wameshindwa kutokana na gharama kubwa kwa vile viongozi wa Simba na Azam wametaka kusafirishwa kwa ndege.

Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...