Skip to main content

SIMBA, AZAM ZAGOMA KUCHEZA AMAAN, FAINALI YAHAMISHIWA DAR






MECHI ya fainali ya michuano ya soka ya Kombe la Urafiki kati ya Simba na Azam imehamishwa kutoka Uwanja wa Amaan, Zanzibar kwenda Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi hiyo, ambayo awali ilikuwa ichezwe kesho kwenye Uwanja wa Amaan, sasa itachezwa Alhamisi kwenye Uwanja wa Taifa.

Katibu wa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo, Suleiman Jabir aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam leo kuwa, uamuzi huo umefikiwa kutokana na timu hizo mbili kugoma kucheza uwanja wa Amaan.

Jabir amewaomba radhi mashabiki wa soka wa Zanzibar kutokana na fainali hiyo kuhamishiwa Dar kwa madai kuwa, jambo hilo lipo nje ya uwezo wao.

Awali, Simba na Azam ziligoma kucheza fainali hiyo kwenye Uwanja wa Amaan kwa madai kuwa ni mbovu na umesababisha kuumia kwa baadhi ya wachezaji wao.

Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' aliwaambia waandishi wa habari kuwa, eneo la kuchezea soka kwenye uwanja huo ni bovu.

Kaburu alisema wapo tayari kucheza fainali hiyo kwenye uwanja wowote, lakini si Uwanja wa Amaani.

Alisema waliwasilisha malalamiko hayo kwa waandaaji kwa muda mrefu, lakini hawakuweza kuyafanyia kazi.

Kaburu alisema kutokana na timu yake kushiriki kwenye michuano ya Kombe la Kagame, wana hofu wachezaji wao wanaweza kuumia zaidi kwenye mechi hiyo.

Aliwataja wachezaji wa Simba walioumia tangu kuanza kwa michuano hiyo kuwa ni Lino Masimbo, Salim Kinje na Mussa Mudde.

Meneja wa Azam, Patrick Setter alisema klabu yake inawapenda na kuwaheshimu mashabiki wa Zanzibar, lakini kutokana na hali ya uwanja wa Amaan, hawawezi kucheza mechi ya fainali visiwani humo.

“Tupo tayari hata kwenda kucheza Pemba ama kwingine kokote, lakini sio hapa Amaan. Hofu yetu ni wachezaji wetu wengi zaidi kuumia,"alisema.

Kwa mujibu wa Patrick, wachezaji wa Azam walioumia tangu kuanza kwa michuano hiyo ni Michael Kipre, Jabir Azizi na Kipre Tchetche.

Alisema hawagomi kucheza mechi hiyo Uwanja wa Amaan kwa sababu ya maslahi, bali wanajali zaidi afya za wachezaji wao.

Rais wa ZFA, Amani Makungu alisema wapo tayari kupokea lawama kutoka kwa wapenzi wa soka wa Zanzibar, lakini hawana la kufanya.

Alisema walikuwa wakifikiria kuihamishia mechi hiyo Uwanja wa Gombani, Pemba lakini wameshindwa kutokana na gharama kubwa kwa vile viongozi wa Simba na Azam wametaka kusafirishwa kwa ndege.

Inatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...