Skip to main content

WENGER AITOLEA NJE MAN UTD, AGOMA KUMUUZA VAN PERSIE KWA DAU DOGO


LONDON, England
KLABU ya Arsenal imegoma kumuuza mshambuliaji wake nyota, Robin van Persie kwa kitita cha pauni milioni 20 kwa klabu ya Manchester United.
Kocha Mkuu wa Arsenal, Arsene Wenger alisema juzi kuwa, watakuwa tayari kumuuza mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi iwapo klabu yoyote inayomuhitaji itatoa kitita cha zaidi ya pauni milioni 25 na 30.
“Van Persie ni mmoja wa washambuliaji bora duniani, kama si bora, na lengo langu ni kumbakisha katika klabu. Nitafanya kile ambacho ni bora kwa maslahi ya Arsenal,”alisema kocha huyo raia wa Ufaransa.
Msimamo huo wa Wenger huenda ukatoa mwanya kwa klabu ya Manchester City, ambayo nayo inamuwinda nyota huyo, kuongeza dau la kumsajili.
Awali, Manchester United ilikuwa tayari kumsajili Mholanzi huyo kwa kitita cha pauni milioni 15 kabla ya kuongeza dau na kufika pauni milioni 20.
Mbali na Manchester United na Manchester City, mshambuliaji huyo pia anawaniwa kwa udi na uvumba na klabu ya Juventus ya Italia.
Manchester City inataka kumuuza mmoja kati ya wachezaji wake, Edin Dzeko au Carlos Tevez ili iweze kupata pesa za kutosha kumsajili Van Persie.
Kocha Mkuu wa Manchester City, Roberto Mancini anaamini kuwa, ni klabu yake pekee yenye uwezo wa kutoa pesa inazihitaji Arsenal kwa ajili ya kumuuza nyota huyo.
Manchester United imekuwa ikimpa Van Persie thamani ndogo kutokana na kuwa na umri wa miaka 29 na pia yupo kwenye mwaka wa mwisho katika mkataba wake na Arsenal.
Tayari Van Persie ameshaeleza azma yake ya kutaka kuihama klabu hiyo, akiwa anataka kufuata nyayo za Cesc Fabregas aliyejiunga na Barcelona ya Hispania msimu uliopita.
Hivi karibuni, Van Persie aligoma kuongeza mkataba mpya wa kuichezea Arsenal, hali iliyodhihirisha wazi kuhusu msimamo wake wa kutaka kuhama.
Kocha Wenger amemwacha mchezaji huyo katika ziara ya barani Asia kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi na kusisitiza kuwa, hatamuuza kwa dau dogo.
Wenger alisema juzi kuwa, yupo tayari kumbakisha Van Persie katika klabu yake hadi mkataba wake utakapomalizika iwapo hakutakuwa na klabu itakayoweza kulipa dau analolitaka.
Kocha huyo alisema anaamini Van Persie ataendelea kuitumikia Arsenal kwa moyo wote kwa sababu anapenda kucheza soka na hiyo ndiyo heshima pekee anayoweza kuipata akiwa mchezaji.
Bodi ya wakurugenzi ya Arsenal huenda ikafunga mjadala kuhusu uhamisho wa nyota huyo, lakini kwa kutegemea maamuzi ya Wenger.
Wenger hakufurahishwa na maamuzi ya bodi hiyo katika usajili wa wachezaji wapya msimu uliopita na ndio sababu ameamua kumuuza kwa pesa nyingi ili apate pesa za kununua nyota wengine wapya.
Kocha Mkuu wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amethibitisha kuwasilisha ofa ya kumsajili nyota huyo kwa klabu ya Arsenal.
Hata hivyo, kocha huyo hakuwa tayari kueleza iwapo wataongeza dau kwa ajili ya kumnasa nyota huyo baada ya pesa walizotenga awali kukataliwa.
Van Persie ameifungia Arsenal mabao 41 katika mechi 53 msimu uliopita na alichaguliwa kuwa mchezaji nyota wa mwaka wa Chama cha Wanaska wa Kulipwa wa England.
Arsenal inatarajiwa kucheza mechi za kirafiki katika nchi za Malaysia, China na Hong Kong katika kipindi cha wiki mbili zijazo.
Hata hivyo, Van Persie atabaki England wakati timu yake itakapokuwa katika ziara hiyo, akifanya mazoezi ya viungo kwenye kituo cha mazoezi cha klabu hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...