Skip to main content

KAMBI ZA WAKIMBIZI WA BURUNDI NCHINI TANZANIA KUFUNGWA ~RAIS KIKWETE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Serikali itahakikisha kambi za wakimbizi wa Burundi katika Tanzania zinafungwa na wakimbizi wanarudi kwao kwa sababu hawana tena sababu ya kuendelea kuwa wakimbizi katika Tanzania.

Amesema kuwa hali ya usalama, amani na utulivu katika Burundi ni mazingira mwafaka kwa kila Mrundi kuishi kwao badala ya kuendelea kuwa mkimbizi katika Tanzania.

Rais Kikwete ameyasema hayo, Alhamisi, Julai 19, 2012, wakati alipokutana na kuzungumza na Sheikh Mohammed Rukara, Mjumbe Maalum wa Rais wa Burundi, Mheshimiwa Pierre Nkurunziza, Ikulu, mjini Dar es salaam. Sheikh Rukara pia ni Mkuu wa Uchunguzi wa Malalamiko ya Wananchi (Ombudsman) katika Burundi.

“Tutashughulika na wakimbizi kwa sababu hawana tena sababu ya kubakia Tanzania kama wakimbizi. Tutahakikisha kuwa kambi za wakimbizi wa Burundi katika Tanzania zinafungwa,” Rais Kikwete amemwambia Sheikh Rukara.

Rais pia ameisifu Burundi kwa mafanikio makubwa ambayo yamepatikana tokea amani irejee katika nchi hiyo jirani na hasa tokea Rais Nkurunziza alipoingia madarakani miaka saba iliyopita.

“Mmefanya kazi kubwa na nzuri sana katika ujenzi wa barabara, ujenzi wa shule, ujenzi wa vyuo vya elimu ya juu na zaidi ya yote ujenzi wa amani na umoja. Ni vyema kuwa macho na kuendelea kulinda amani,” amesema Rais.

Sheikh Rukara amemshukuru tena Rais Kikwete kwa mchango wake mkubwa katika kutafuta amani ya Burundi. “Mheshimiwa Rais ulituokoa sana,” amesema Sheikh Rukara.

Miongoni mwa mambo mengine, katika salamu zake maalum, Rais Nkurunziza amemshukuru Rais Kikwete kwa kuhudhuria Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Burundi zilizofanyika mjini Bujumbura Julai 2, mwaka huu, 2012.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
19 Julai, 2012

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.