Skip to main content

Yanga Kaeni Mkao wa Kula

 

 

SWALI: Awali ya yote, hongera kwa kuchaguliwa kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga kwa kura nyingi.
JIBU: Asante, nashukuru sana.
SWALI: Kabla ya uchaguzi huu, ulikuwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili ya Yanga na sasa ni mjumbe wa kamati ya utendaji. Nini mikakati yako kwa Yanga?
JIBU: Kwa kweli namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwa na afya njema hadi sasa. Pia napenda kuwashukuru wanachama wenzangu wa Yanga kwa kuniamini na kunipa kura nyingi kuliko wagombea wote.
Unajua bila ya wanachama kukuamini, hawawezi kukupa heshima kubwa kiasi hiki. Nawaomba waendelee kuniamini na mimi nawaahidi kwamba, nitaitumikia klabu yetu kwa moyo wangu wote na nguvu zote.
Jambo la msingi ni kwamba, viongozi wapya wa Yanga tunakabiliwa na changamoto kubwa ya kuchapa kazi ili kuhakikisha tunaleta mabadiliko makubwa kiuongozi na katika timu ili tuweze kufikia malengo tutakayojipangia. Tunapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia kauli mbiu yetu ya Yanga mbele, nyuma mwiko.
SWALI: Umepanga kufanya nini katika kutekeleza ahadi ulizozitoa kwa wanachama wakati wa kampeni?
JIBU: Nimepanga kufanya mambo makubwa matatu. La kwanza ni kushirikiana na viongozi wenzangu kuhimiza umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama ili kuondoa makundi yaliyojitokeza wakati wa uchaguzi, ambayo yakiachwa, yanaweza kuwa chanzo cha mgogoro.
Unajua umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama ni jambo muhimu kuzingatiwa kama kweli tunataka kupata maendeleo. Tukigawanyika, hatutaweza kufanikiwa kwa lolote lile. Kwa maana hiyo, nitahakikisha kila mwanachama, kuanzia ngazi ya matawi, anashiriki kikamilifu katika kutoa maamuzi mbalimbali muhimu yanayoihusu Yanga.
Jambo la pili ni kwamba, nitahakikisha Yanga inakuwa na timu imara za vijana wa umri mbalimbali kwa ajili ya kujenga timu bora ya baadaye. Na utaratibu huu utaanzia mikoani kupitia kwa matawi yetu.
Kama utakumbuka vizuri, zamani Yanga ilikuwa ikiyatumia matawi yake ya mikoani kusaka vipaji vya wachezaji. Tumepanga kuurejesha upya utaratibu huu kwa kusaka vipaji vya vijana watakaounda timu hizi za vijana kutoka mikoani na Dar es Salaam. Wachezaji tutakaowachukua ni wale wenye mapenzi ya kweli na Yanga.
Jambo la tatu ni kwamba, nataka kuiona Yanga ikipata mafanikio makubwa katika michuano ya ligi na kimataifa kwa kutoa kipaumbele kwa wachezaji na benchi la ufundi.
Nimepanga kutoa kipaumbele kwa wachezaji na benchi la ufundi kwa sababu kama hawapati haki zao vizuri na kwa wakati, hawawezi kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Hivyo nitahakikisha kuwa, uongozi mpya wa Yanga unawapatia wachezaji haki zao kwa wakati na kwa kiwango kinachokubalika.
Jambo lingine muhimu nitakalolipa kipaumbele ni kuhakikisha kuwa, katiba ya Yanga inafanyiwa marekebisho ili iweze kwenda na wakati na kuondosha kabisa migogoro iliyokuwepo miaka ya nyuma. Ninapenda kuona viongozi wakitimiza wajibu wao bila kuingiliana ama kuwekewa vikwazo na wanachama.
SWALI: Katika msimu uliopita, ulifanikiwa kumsajili mshambuliaji Haruna Niyonzima kutoka APR ya Rwanda kwa pesa nyingi. Na msimu huu pia umechangia usajili wa wachezaji kadhaa wapya. Je, bado una mikakati yoyote ya kusajili mchezaji mwingine mpya?
JIBU: Kwa kawaida huwa napenda sana kufanya kazi zangu kwa siri bila mtu mwingine kufahamu lolote kama ilivyokuwa kwa Niyonzima. Hivyo ni kweli kwamba ninaye mchezaji mwingine ninayeendelea kufanya mipango ya kumsajili na mipango itakapokuwa tayari, tutawajulisha.
SWALI: Kuna taarifa kwamba ulikuwa katika mipango ya kumsajili mshambuliaji Meddie Kagere wa Polisi ya Rwanda na alikuwepo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo na viongozi. Je, mipango hiyo imefikia wapi?
JIBU: Ni kweli tulikuwa na mipango hiyo na niliifanya kwa kushirikiana na wadau wengine wa Yanga, lakini ilikwama kidogo kutokana na kujitokeza kwa hali ya kutokuelewana kati yetu na mchezaji huyo.
Lakini bado hatujakata tama kwa sababu lolote linaweza kutokea kwa vile muda wa usajili bado haujamalizika. Kama utakumbuka, mwisho wa usajili wa wachezaji wapya ni Agosti 10 mwaka huu ifikapo saa 5.59 usiku.
SWALI: Kwa sasa, Yanga inashiriki katika michuano ya Kombe la Kagame mkiwa mabingwa watetezi. Nini mikakati yenu kwa ajili ya michuano hiyo?
JIBU: Japokuwa tulianza vibaya kwa kufungwa na Atletico ya Burundi, mikakati yetu ni kuhakikisha tunautetea vyema ubingwa wetu. Waswahili wana msemo usemao kuteleza si kuanguka. Nawaomba wanachama na mashabiki wa Yanga wawe wavumilivu kwa sababu uwezo wa kufanya vizuri tunao.
Vilevile napenda kuwahakikishia wana Yanga wote kuwa, wasiwe na wasiwasi kuhusu michuano ya ligi kuu kwa sababu timu ipo imara na itakuwa chini ya viongozi makini, hivyo uwezo wa kurejesha taji letu msimu ujao tunao. Kilichotokea msimu uliopita ni matatizo tu madogo madogo, ambayo hayawezi kutokea tena.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...