Skip to main content

JOSE CHAMELEONE AVAMIA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UGANDA, ASHINIKIZA AREJESHEWE PASIPOTI YAKE


Chameleone akiteta jambo na mmoja kati ya wafuasi wake nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.
Chameleone akipiga gita huku wafuasi wake wakiwa wamebeba mabango nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.

Polisi wa Uganda wakimtuliza Chameleone na wafuasi wake wakati walipofanya maandamano ya amani nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.

Ofisa mmoja wa polisi akizungumza na wafuasi wa Chameleone nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.


Mwanamuziki Jose Chameleone na wafuasi wake sikuchache zilizopita  wapovamia kwenye ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda na kushinikiza arejeshewe pasi yake ya kusafiria.


Jose, mmoja wa wanamuziki tajiri katika nchi za ukanda wa Afrika, aliendesha gari lake aina ya Range Rover Sport na kuliegesha karibu na ubalozi huo.


Mwanamuziki huyo pamoja na wafuasi wake walikuwa na mabango yaliyokuwa na maandishi yanayomtaka mfanyabiashara Eric Shigongo arejeshe hati yake ya kusafiria.


Jose aliweka kambi kwa muda nje ya ubalozi huo na kupiga gita lake huku akiimba nyimbo mbali mbali. Wafuasi wake walikuwa wamebeba mabango ya kupinga kitendo cha Shigongo kumnyang'anya hati yake ya kusafiria.


Baadhi ya mabango yalisomeka: 'Shigongo upo juu ya sheria?' , 'Tafadhali Tanzania nisaidieni', 'Nahitaji nirejeshewe hati yangu ya kusafiria'.


Shigongo ndiye aliyemwalika Jose kufanya onyesho wakati wa tamasha la matumaini lililofanyika hivi karibuni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Jose alifanya onyesho wakati wa tamasha hilo, lakini inasemekana kuwa Shigongo alikataa kumlipa pesa zake kwa madai kuwa, tayari alishamlipa meneja wa mwanamuziki huyo, aliyejulikana kwa jina la George.


Imeelezwa kuwa, Shigongo alimlipa George dola 3,500 za Marekani kwa ajili ya Jose kufanya onyesho hilo, lakini mwanamuziki huyo alikana kumtambua meneja huyo.


Jose alifanikiwa kuondoka nchini baada ya kupewa hati ya muda ya kusafiria katika ofisi za ubalozi wa Uganda hapa nchini.


Uamuzi wa Jose kuvamia ubalozi wa Tanzania nchini Uganda, ulifanyika saa chache baada ya kutoka kufanya onyesho kwenye Uwanja wa Amahoro mjini Kigali, Rwanda.


Maofisa kadhaa wa polisi wa Uganda walifika kwenye ofisi za ubalozi huo wakiwa na gari yenye namba UP-2627 kwa ajili ya kulinda usalama.


Hata hivyo, Jose aliwaeleza polisi hao kuwa, yeye na wenzake waliamua kufanya maandamano ya amani kwa lengo la kushinikiza arejeshewe hati yake ya kusafiria.


Baadaye, nyota huyo wa muziki alikutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Uganda, ambaye alimuahidi kwamba atalifanyia kazi suala lake kwa kuwasiliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Tanzania, Inspekta Saidi Mwema.Iatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...