Skip to main content

JOSE CHAMELEONE AVAMIA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UGANDA, ASHINIKIZA AREJESHEWE PASIPOTI YAKE


Chameleone akiteta jambo na mmoja kati ya wafuasi wake nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.
Chameleone akipiga gita huku wafuasi wake wakiwa wamebeba mabango nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.

Polisi wa Uganda wakimtuliza Chameleone na wafuasi wake wakati walipofanya maandamano ya amani nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.

Ofisa mmoja wa polisi akizungumza na wafuasi wa Chameleone nje ya ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda.


Mwanamuziki Jose Chameleone na wafuasi wake sikuchache zilizopita  wapovamia kwenye ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini Uganda na kushinikiza arejeshewe pasi yake ya kusafiria.


Jose, mmoja wa wanamuziki tajiri katika nchi za ukanda wa Afrika, aliendesha gari lake aina ya Range Rover Sport na kuliegesha karibu na ubalozi huo.


Mwanamuziki huyo pamoja na wafuasi wake walikuwa na mabango yaliyokuwa na maandishi yanayomtaka mfanyabiashara Eric Shigongo arejeshe hati yake ya kusafiria.


Jose aliweka kambi kwa muda nje ya ubalozi huo na kupiga gita lake huku akiimba nyimbo mbali mbali. Wafuasi wake walikuwa wamebeba mabango ya kupinga kitendo cha Shigongo kumnyang'anya hati yake ya kusafiria.


Baadhi ya mabango yalisomeka: 'Shigongo upo juu ya sheria?' , 'Tafadhali Tanzania nisaidieni', 'Nahitaji nirejeshewe hati yangu ya kusafiria'.


Shigongo ndiye aliyemwalika Jose kufanya onyesho wakati wa tamasha la matumaini lililofanyika hivi karibuni kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Jose alifanya onyesho wakati wa tamasha hilo, lakini inasemekana kuwa Shigongo alikataa kumlipa pesa zake kwa madai kuwa, tayari alishamlipa meneja wa mwanamuziki huyo, aliyejulikana kwa jina la George.


Imeelezwa kuwa, Shigongo alimlipa George dola 3,500 za Marekani kwa ajili ya Jose kufanya onyesho hilo, lakini mwanamuziki huyo alikana kumtambua meneja huyo.


Jose alifanikiwa kuondoka nchini baada ya kupewa hati ya muda ya kusafiria katika ofisi za ubalozi wa Uganda hapa nchini.


Uamuzi wa Jose kuvamia ubalozi wa Tanzania nchini Uganda, ulifanyika saa chache baada ya kutoka kufanya onyesho kwenye Uwanja wa Amahoro mjini Kigali, Rwanda.


Maofisa kadhaa wa polisi wa Uganda walifika kwenye ofisi za ubalozi huo wakiwa na gari yenye namba UP-2627 kwa ajili ya kulinda usalama.


Hata hivyo, Jose aliwaeleza polisi hao kuwa, yeye na wenzake waliamua kufanya maandamano ya amani kwa lengo la kushinikiza arejeshewe hati yake ya kusafiria.


Baadaye, nyota huyo wa muziki alikutana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Uganda, ambaye alimuahidi kwamba atalifanyia kazi suala lake kwa kuwasiliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Tanzania, Inspekta Saidi Mwema.Iatoka kwa mdau.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.