Baada ya kibali cha kuwazika nchini Tanzania wahamiaji toka Ethiopia waliofariki ndani ya lorry walilokuwa wanasafiria kutolewa na Serikali yao ya
Ethiopia, Serikali ya Tanzania iliamua mazishi ya Raia hao wa Ethiopia
kufanyika Juni 29, 2012 Alasiri Mkoani Dodoma na Morogoro kwa baadhi ya
miili iliyokuwa imehifadhiwa hospitali ya Mkoa Morogoro na kazi
inayoendelea hapa ni ya uchimbaji wa makaburi.
Vijana
84 wahamiaji kutoka Ethiopia walionusurika kifo wakipita mmoja baada ya
mwingine wakitoa heshima zao za mwisho na kuwaaga ndugu zao kwa kutupa
udongo kwenye makaburi yaliyohifadhi miili ya wenzao waliopoteza maisha
katika tukio la kusafirishwa kwenye Lorry.
Kijana
Chafamo Yosef (kulia) Muamiaji raia wa Ethiopia akitoa neno la shukrani
muda mfupi baada ya kumalizika kwa mazishi kwa jinsi ambavyo wamepatiwa
msaada na serikali ya Tanzania tangu siku walipokutwa wametelekezwa,
miongoni mwa vitu alivyoahidi akifika nchini kwao Ethiopia ni
kuwaelezea watu wa Ethiopia kuwa walidanganywa na kusababishiwa
matatizo makubwa hadi baadhi yao kupoteza maisha lakini wao Mungu
amewanusuru, wameona nchi nzuri ya Tanzania, wamekutana na serikali
nzuri iliyowahudumia kila kitu, na wananchi wenye mioyo ya huruma na
ukarimu.
Raia
wahamiaji kutoka Ethiopia walionusurika kifo wakiwa wameinamisha vichwa
vyao chini kuwaombea sala wenzao waliopoteza maisha wakati wa shughuli
ya mazishi.
Safari
ya mwisho ya kuwasindikiza na kuwahifadhi katika nyumba zao za milele
wahamiaji 43 (21 Dodoma, 23 Morogoro) kutoka Ethiopia waliopoteza
Maisha ilihitimishwa kwa kazi ya kufukia makaburi iliyofanywa na vijana
na wananchi mbalimbali waliojitokeza kwenye mazishi hayo.
Wahamiaji
hawa (walionusurika) wamekuwa watu waliozamia katika sala na maombi
baada ya kunusurika kifo ukizingatia baadhi ya wenzao walikufa katika
tukio hilo, kila baada ya chakula jioni wanapewa muda wa kufanya maombi.
Wahamiaji kutoka Ethiopia walipatiwa kila aina ya msaada wa muhimu uliohitajika kwa wakati kama malazi, mavazi, chakula dawa, matibabu ya kisaikolojia nk
Mtoa
huduma ya kwanza wa Msalaba Mwekundu akimfunika mmoja wa wahamiaji
kutoka Ethiopia ambaye alikuwa na tatizo la maumivu kifuani.
Vijana
walioandaliwa kwa ajili ya shughuli ya Mazishi wakishusha miili ya
Marehemu kwenye nyumba zao za milele (makaburi) ikiwa ni hatua za
mwisho za kuhitimisha safari ya mwisho ya kuwapumzisha watu hao
waliopoteza maisha.
Vijana
Wahamiaji kutoka Ethiopia walionusurika kifo wakilia kwa uchungu muda
mfupi baada ya miili ya Wenzao waliopoteza maisha kuwasili eneo la
maziko mjini Dodoma, jumla ya Waethiopia 43 walipoteza maisha ambapo 21
wamezikwa Dodoma na 23 Morogoro.
Vijana Wahamiaji kutoka Ethiopia walionusurika kifo wakiwa wamejipanga mistari miwili wakionekana wenye
huzuni muda mfupi baada ya kuwasili eneo lililoandaliwa katika Manispaa
ya Dodoma kwa ajili ya kuwazika wenzao waliopoteza maisha katika tukio
hilo la kusikitisha, jumla ya Waethiopia 43 walipoteza maisha ambapo 21
wamezikwa Dodoma na 23 Morogoro. Picha zote na Jery Mwakyoma
Comments