Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2016

Shamrashamra zimemalizika katika mji wa Milan zimemalizika na kutua sasa Madrid

Shamrashamra zimemalizika katika mji wa Milan na badala yake sherehe hizo za kushangilia ubingwa zimehamia kwenye jiji la Madrid ambako Real wanasubiriwa kupokelewa na mashabiki wao baada ya kufanikiwa kutwaa taji la vilabu bingwa barani Ulaya. Baada ya mchezo kumalizika, makocha wote wawili walikuwa na mitazamo tofauti kutokana na timu zao zilivyocheza na matokeo yaliyopatikana baada ya mechi kumalizika. Zidane yeye amefanikiwa kubeba taji hilo akiwa kocha wa saba kati ya wale ambao waliwahi kutwaa kama wachezaji na baadaye kutwaa taji hilo wakiwa makocha. Zidane ametumia muda mfupi sana kuiwezesha Madrid kushinda Champions League ukilinganisha na watangulizi wake. Ndani ya mezi sita amefanikiwa kutwaa taji hilo tangu alipokabidhiwa timu toka mikononi mwa Rafael Benitez. Amesema siri kubwa ya mabadiliko na mapinduzi aliyoyafanya kwenye kikosi cha Real ni kuwasisitiza wachezaji wake kupambania mafaniko bila kuchoka na kikubwa ni falsafa yake ya kwa

MTIBWA SUGAR ITAENDELEA KUMPA NAFASI SHAABAN NDITTI

Shaaban nditti anamaliza msimu wake wa 17 mfululizo katika ligi kuu Tanzania bara na mchezaji huyo wa zamani wa Taifa Stars bado ana nguvu, maarifa, mbinu, na uwezo wa kupambana bila kuchoka na wachezaji vijana. Wakati wengi ‘wameingia na kutoka’ katika ligi kuu bara, Nditti amedumu tangu mwaka 1999 alikoanza soka lake akiwa na timu ya Singida United ya Singida. Alisajiliwa na Mtibwa Sugar kwa mara ya kwanza mara baada ya Mtibwa kutwaa ubingwa wao wa pili mfululizo wa VPL mwishoni mwa 2000. “Na bado kama Mungu anampa uzima basi atafikisha miaka 25 maana bado mwenye nguvu na anawajibika ipasavyo, na pia ana jitunza haswa”, anasema Yusuph Mgwao mshambuliaji wa zamani wa Simba SC na Mtibwa ambaye amewahi kucheza na Nditti katika timu zote hizo miaka ya 2004 na 2005. Nditti aliondoka Mtibwa na kusajiliwa na Simba mwishoni mwa mwaka 2003 lakini alishindwa kutulia klabuni hapo na baada ya kumalizika kwa msimu wa 2004 akaamua kurejea Mtibwa ambako

YANGA SASA WATAKUWA WABABE WA AFRIKA

Na Baraka Mbolembole Mabingwa mara mbili mfululizo wa ligi kuu Tanzania Bara, timu ya Yanga SC imekuwa timu ya kwanza Afrika Mashariki (Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi) kufuzu kwa hatua ya makundi katika michuano ya Shirikisho Afrika. Yanga ilikuwa timu ya kwanza pia ukanda huu kufuzu kwa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika mwaka 1998. Ni wa kwanza katika kila kitu na licha ya kupoteza game ya marejeano jana Jumatano huko mjini Dundo, Angola dhidi ya wenyeji wao Esperanca, mabingwa hao mara 26 wa kihistoria Tanzania Bara wamefanikiwa kukata kiu ya mashabiki wao na wadau wa kandanda Tanzania ambao wamekuwa wakilalamika namna klabu ya VPL zinavyoshindwa mapema katika michuano ya CAF kila mwaka. Timu ya mwisho ya Tanzania na Afrika Mashariki kufuzu kwa hatua ya makundi ya michuano ya CAF ni Simba SC ambayo inakumbukwa namna walivyowavua ubingwa wa ligi ya mabingwa Zamalek ya Misri na kufuzu kwa hatua

Farid anarejea leo nchini kutoka Hispania sasa kusubiria mazungumzo

Farid alitafutiwa timu hiyo na wakala wake ambaye hapo awali Farid ilikuwa apelekwe moja ya klabu za Ligi Kuu ya Hispania, maarufu kama La Liga, kati ya Las Palmas na Athletic ya Bilbao kwa majaribio, lakini wakala wake akashauri mchezaji huyo aanzie timu ya Daraja la Kwanza Hispania ili kupata nafasi ya kucheza na kuinuka haraka. Baada ya majaribio na Klabu ya Tenerife, Farid alifanya vizuri na Klabu hiyo ikakubali kiwango chake hivyo Farid anarejea nchini kusubiria mazungumzo ya Klabu yake ya Azam fc na Tenerife ili kuweza kuitumikia klabu hiyo. Farid alikwenda Hispania Aptili 21 mwaka huu akitoka kuichezea klabu yake, Azam FC katika mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Esperance.

Magazetini leo

SAMATTA DAKIKA 90, GENK IKIVUNA USHINDI MNONO NYUMBANI

Mbwana Samatta amecheza dakika zote 90 za mchezo kati yake ya Genk dhidi ya Anderlecht na kuisaidia Genk kuibuka na ushindi wa magoli 5-2 katika kampeni za kuhakikisha timu yao inapata nafasi ya kushiriki michuano ya Europa League. Anderlecht walianza kufunga goli la kuongoza dakika ya 25 kupitia kwa kiungo wao Filip Djuricic lakini goli hilo lilisawazishwa na Leon Bailey dakika ya 45 na kuufanya mchezo huo kwenda mapumziko timu zote zikiwa sare kwa kufungana goli 1-1. Kipindi cha pili Suarez aliiweka tena mbele Anderlecht kwa kuifungia bao la pili dakika ya 60 lakini dakika tano baadaye Buffel aliisawazishia Genk. Dakika ya 76, Pozuelo aliiweka mbele Genk kwa kutupia bao la tatu kisha Ndidi akaongeza bao la nne kabla ya Nikos Karelis hajamaliza shughuli kwa kufunga goli dakika ya 90 ya mchezo. Samatta kucheza dakika zote 90 ni faraja kubwa kwasababu mchezo uliopita alitolewa kipindi cha kwanza wakati Genk ilipocheza na KV Oostende. Samatta ame

Utata wazuka kuhusu msichana wa Chibok

Kuna utata kuhusu ni nani alimuokoa na jina la msichana ni lipi. Kumezuka utata kuhusu msichana wa Chibok ambaye aliokolewa nchini Nigeria. Kwanza jeshi linasema kuwa ndilo lilimuokoa msichana huyo aliyetjwa jina kuwa Falmata Mbalala. Hata hivyo wanaharakati na viongozi wa kijamii wanasema kuwa msichana aliyeokolewa, jina lake ni Amina Ali Nkek na kuwa alipatikana katika msitu wa Sambisa na kundi la vijana na kudumisha usalama. Msitu huo ndio maficho makuu ya wanamgambo wa Boko Haram. Mwenyeki wa chama cha wazazi wa Cibok mjini Abuja Hosea Abana Tsambido aliiambia BBC kuwa vijana hao walikuwa na habati kubwa kumpata msichana huyo. BBC

WATAKA UWANJA WA NDEGE MWANZA UJENGWE KISASA ILI KUINUA SEKTA YA UTALII

Na Tiganya Vincent-MAELEZO_Dodoma Baadhi ya Wabunge wanaotoka Kanda ya Ziwa wameomba Wizara ya Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano kujenga Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa kiwango cha Kimataifa ili kuimarisha sekta ya Utalii na usafiri wa anga katika kanda ya Ziwa. Walisema kuwa hatua itasaidia watalii wanaokuja nchini kushuka moja kwa moja mkoani Mwanza na kisha kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na maeneo mengine ya vivutio vya hapa nchini bila kupitia nchi jirani. Kauli hiyo imetolewa jana na Wabunge Dkt.Raphael Chegeni  na Mhe. Ezekeil Maige wakati wakichangia hotuba kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi  na Mawasiliano kwa mwaka ujao wa fedha. Mhe. Dkt.Chegeni alisema kuwa Uwanja wa Ndege wa Mwanza ni muhimu ukajengwa kwa viwango vya Kimataifa ili uweze kuruhusu ndege mbalimbali kubwa na ndogo kuweza kutua bila tatizo.

Wema :Huyu Alikiba mumuache kwa kweli

Msanii Wema Sepetu Inatoka Facebook Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote "Ila huyu bichwa wangu mimi ananikoshaga sana. Na mumuachage tu kwakweli. Bichwa una sifa lakini maana si kwa Vocal hizi. Halafu mimi siwezi kukubania namba bana. Naupenda sana huu wimbo jamani. Wajua kutukunaga mashabiki wako. Good work Bichwa wangu Officialalikiba did it again ladiez & Gentlemen" aliandika Wema Sepetu Mbali na hilo Wema Sepetu amempa pongezi msanii Alikiba kwa kuweza kusaini mkataba chini ya kampuni ya muziki ya 'Sony Music' na kusema kuwa alistahili hilo na zaidi ya hilo kwani anakipaji kikubwa. " God Grants accordingly... Congrats Bichwa wangu for that Big Contract... You deserve it & more... Time Heals all wounds... The Sky remains to be the only Limit for u b

Bingwa

Tabia Mbovu Zinazowarudisha Wengi Nyuma Kimafanikio.

By: Hisia za Mwananchi / Posted: Wednesday 11th May 2016 Mara nyingi tumekuwa tukisema tabia zako ulizonazo ndizo zinazopelekea maisha yako yawe bora au mabovu. Ni jambo ambalo tumekuwa tukikumbushana kwamba siku zote maisha ya binadamu yanaongozwa na tabia alizonazo binadamu huyo. Kwa mantiki hiyo, ikiwa na maana kwamba kwa kujijengea tabia za aina fulani kwenye maisha yako, ndivyo maisha yako yataendelea kuwa hivyo   kama tabia zako jinsi zilivyo. Tatizo walilonalo wengi ambalo linakuwa linawasumbua sana ni kule kurudishwa nyuma na tabia zao. Utakuta mtu anauwezo mzuri kabisa wa kutengeneza pesa za kutosha lakini kila wakati anakuwa hana au anaishi maisha ya kimaskini kwa sababu ya kujijengea tabia mbaya. Ili kufanikiwa unatakiwa kutambua mapema tabia zinazo kurudisha nyuma kimafanikio. Je, unajua ni tabia gani zinazokurudisha sana nyuma kwenye maisha yako? 1. Kuamini maisha ni magumu. Siku zote ukweli wa maisha uko hivi; ili uweze kufanikiwa ni lazima uwe c

Askofu afuata nyayo za Mmagufuli kutumbua majipu

MAJALIWA: SERIKALI KUSAKA WALIOKULA FEDHA ZA WATUMISHI HEWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watanzania Waishio  nchini Uingereza  kwenye ubalozi wa Tanzania uliopo London Mei 14, 2014.   Kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Kikanda na Kimataifa, Augustine Mahiga. Kushoto ni Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Msafiri  Marwa . WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeamua kupambana na wala rushwa ili kiasi kidogo cha rasilmali kilicholengwa kiweze kuwafikia wananchi. Ametoa kauli hiyo juzi (Jumamosi, Mei 14, 2016) wakati akizungumza na Watanzania waishio Uingereza kwenye mkutano uliofanyika kwenye Ubalozi wa Tanzania jijini London, Uingereza. “Jambo tuliloamua kuanza nalo ni kupambana na rushwa. Tumeamua kufanya hivyo ili kurudisha umoja na maelewano miongoni mwa Watanzania, tunataka tuibadili Tanzania ili iwe ni ya Watanzania wote… tu

Bayern Munich wafanya party kusherekea Ubingwa wa Bundesliga

Wachezaj wa mabingwa mara nne mfululizo wa Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga), Bayern Munich wamefanya party kusherekea ubingwa wa ligi hiyo ambapo walijumuika kwa pamoja wakiwa na kocha wao, Pep Guardiola na baadhi ya viongozi wa klabu hiyo. Mkurugenzi wa michzo wa Bayern Munich, Matthias Sammmer akizungumza jambo na Juan Bernat. Robert Lewandowski. Jerome Boateng akizungumza jambo na kocha wake, Pep Guardiola. Thomas Muller akicheza katika jukwaa. Robert Lewandowaski akionyesha uwezo wake wa kucheza. Bendi ya OneRepublic ikiwaburudisha wachezaji wa Bayern Munich waliojumuika kufurahia ubingwa wa Ligi Kuu ya Ujerumani.

Serikali yasitisha ubomoaji nyumba

Leo ni leo wakimataifa

Mapya ya Mose Iyobo mahusiano yake na mpenzi wake Aunt Ezekiel

Mose Iyobo ambaye amezaa na star wa Bongo movie Aunt Ezekiel amesema hasa hasa amenufaika sana na umaarufu wa Aunt Ezekiel kwa kujulikana zaidi. “Kuwa na mahusiano na mama Cookie kumenisogeza sana,” alisema Mose. “Kwa sababu ni star wa filamu toka kitambo sana. Mimi nilikuwa najulikana lakini siyo kivile, lakini nilivyokutana na Mama Cookie kuna vitu vingi vimeongezeka katika maisha yangu,” alisema Mose. Pia Mose amesema mwanae Cookie ataonyeshwa hadharani rasmi kwa mara ya kwanza tarehe 21 mwezi huu baada ya kutimiza mwaka mmoja. Source: Bongo5

Sporah Luhende Ndiye Mshindi wa Tarent Miss Dar City Center, 2016

Miss Dar city center Talent ilivyofana jana   majaji wakifuatilia kinyang’anyiro Mashabiki   Sporah Luhende akiwa kwenye pozi HATIMAYE shindano la kumtafuta Miss Dar City Centre Talent limefanyika usiku wa alhamisi  katika Ukumbi wa Maisha Basement uliopo Kijitonyama jijini Dar. Katika kinyang’anyiro hicho, kilichoshirikisha warembo kibao hatimaye mrimbwende Sporah Luhende aliibuka mshindi wa kipaji baada ya kuimba Wimbo wa Mahaba Niue wa msanii Maua Sama. Kilele cha shindano hilo la warembo linatarajiwa kuwa Mei 21, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Golden Tulip City Centre. Shindano hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Global Publishers kupitia Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba  inayoendeshwa kupitia Magazeti ya Championi, Ijumaa, Risasi, Amani, Uwazi  ambapo droo ya ndogo ya bahati nasibu hiyo itachezeshwa Mei, 18  na droo kubwa yenye ushindi wa nyumba itachezeshwa mwezi ujao.

Bongo Movie – Rose Ndauka afunguka

Msanii wa filamu nchini Rose Ndauka ameweka wazi kuwa kwenye tasnia hiyo wapo baadhi ya watu wachache ambao wameingia kwenye tasnia hiyo wakiwa na lengo la kujiuza na kupata wanaume, ambao wamekuwa wakiichafua tasnia hiyo. Kupitia kipindi cha Mkasi, Rose Ndauka aliweka sawa kuwa kuna wasanii ambao wanaingia kwenye tasnia hiyo kuwa kuwa wana vipaji na wanataka kufanya filamu kama kazi na kusema wapo baadhi ambao kweli wameingia kwenye filamu ili kupata wanaume au mabwana kupitia tasnia hiyo. “Kiukweli si kila msanii anayeingia kwenye filamu anataka kupata wanaume japo wapo baadhi ya watu wanasukumwa na hiyo hali lakini ukweli ni kwamba wapo wasanii ambao wanaingia kwenye filamu sababu wana vipaji na wanataka kufanya filamu kama kazi na kufanikiwa kimaisha” alisema Rose Ndauka. Mbali na hilo msanii huyo alisisitiza kuwa kitendo cha wanawake kujiuza ni si kwenye tasnia ya filamu tu hata katika maisha ya kawaida watu hao wapo hivyo amedai hali

KESSY AMWAGA WINO YANGA

Wakati timu ya Simba ikiendelea kufanya vibaya beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za mkataba wa kujiunga na Yanga Kuna msemo wa Kiswahili unasema ‘ukisusa wenzio wala’, msemo huu umetimia baada ya beki wa kulia wa kikosi cha Simba SC Hassan Kessy kutia dolegumba kwenye fomu za usajili za Yanga na kujiunga na mabingwa hao wa mitaa ya Twiga na Jangwani. Kessy ametia saini juzi mkata wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Yanga kwa miaka miwili kuanzia mwezi ujao (June, 2016). Awali Kessy alikuwa akiitumikia klabu ya Simba kabla ya kufungiwa mechi tano na wekundu hao wa Msimbazi kwa madai ya kuigharimu timu kutokana na kitendo cha kuoneshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Toto Africans mchezo uliomalizika kwa Simba kupoteza kwa bao 1-0. Licha ya Simba kumfungia Kessy, tayari beki huyo mwenye uwezo mkubwa wa kukaba ns kupandisha mashambulizi mkata wake wa na Simba unamalizika mwisho wa msimu

kijana mlemavu wa akili amombaa radhi na nguli wa hip hop Marekani

Rapa 50 Cent ameomba radhi familia ya kijana mlemavu wa akili kwa kupost video ya kijana huyu akiwa kazini na kusema ametumia kilevi flani huku akifanya kazi kwenye uwanja wa ndege nchini Marekani. 50 Cent alipondwa vikali na mashabiki wake kwa kitendo hicho alichomfanyia kijana huyu huku familia yake ikitaka awaombe radhi uso kwa uso na kulipa faini ya dola milioni moja. 50 Cent ameomba radhi kwa kuandika barua kumuomba msamaha kijana huyo aitwaye Andrew Farrell. Na sasa familia yake imemtaka 50 cent alipe dola 100,000 kwa taasisi ya Autism Speaks, Mchango huo ni mdogo zaidi ukilinganisha na dola milioni 1 ambazo baba wa kambo wa Andrew alitaka walipwe.

Trump :Mike Tyson sio mmbakaji

Mgombea urais nchini Marekani Donald Trump amesema atabaki na msimamo wake wa kumtetea Mike Tyson kuwa hajawahi kumbaka mtu na kwamba sio mmbakaji. Wampinzani wa Donald Trump wametumia kesi ya ubakaji ya mwaka 1992 ya bongia Mike Tyson ambapo Donald Trump alimtetea mpiganaji huyo. Donald amejibu kwa kusema “Sababu Mike Tyson amenikubali na kuliweka wazi jambo hilo mitandaoni, basi ishakuwa issue, Sijaonana na Mike kwa miaka mingi sasa ila yeye kafanya hivyo kuonyesha anakubali nachosema”

Msanii Snura atobia alipojifunzia nyonga

  Msanii Snura ambaye  video ya wimbo wake wa mpya ‘Chura’ umefungiwa  na serikali kutokana na kutokuwa na maadili na kukiuka utamaduni wa kitanzania amefunguka na kusema kuwa yeye kukata viuno amejifunzia kwenye ngoma za asili. Snura amefafanua na kuomba radhi kwa watanzania kutokana na video yake hiyo kutokuwa na maadili na kuwadhalilisha wanawake. “Mimi ni mwanamke na niliwachukua wanawake wenzangu kucheza lakini haina maana kuwa niliwachukua ili niwadhalilishe hapana, ila nakiri kuwa nilichokosea ni kuwaingiza kwenye maji ndiyo maana ilionekana kama ni udhalilishaji kwao. Lakini kucheza hakumdhalilishi mtu na ndiyo maana kuwa bendi wachezaji show wake wanakatika hata kwenye ngoma zetu za asili tunakatika, mimi nimejifunza kukatika kwenye ngoma za asili kwani ndiyo kipaji changu cha kwanza na huko ndiyo nimejifunzia kiuno” alisema Snura