Skip to main content

Tabia Mbovu Zinazowarudisha Wengi Nyuma Kimafanikio.


Mara nyingi tumekuwa tukisema tabia zako ulizonazo ndizo zinazopelekea maisha yako yawe bora au mabovu. Ni jambo ambalo tumekuwa tukikumbushana kwamba siku zote maisha ya binadamu yanaongozwa na tabia alizonazo binadamu huyo. Kwa mantiki hiyo, ikiwa na maana kwamba kwa kujijengea tabia za aina fulani kwenye maisha yako, ndivyo maisha yako yataendelea kuwa hivyo  kama tabia zako jinsi zilivyo.Tatizo walilonalo wengi ambalo linakuwa linawasumbua sana ni kule kurudishwa nyuma na tabia zao. Utakuta mtu anauwezo mzuri kabisa wa kutengeneza pesa za kutosha lakini kila wakati anakuwa hana au anaishi maisha ya kimaskini kwa sababu ya kujijengea tabia mbaya. Ili kufanikiwa unatakiwa kutambua mapema tabia zinazo kurudisha nyuma kimafanikio. Je, unajua ni tabia gani zinazokurudisha sana nyuma kwenye maisha yako?1. Kuamini maisha ni magumu.Siku zote ukweli wa maisha uko hivi; ili uweze kufanikiwa ni lazima uwe chanya kwanza. Lakini kwa bahati mbaya wengi wetu hawako hivi. Ni watu wa kuamini sana maisha hasi ikiwa pamoja na kuamini maisha ni magumu. Mara nyingi wengi wetu tumelishwa imani ya kwamba maisha ni magumu sana na kusahau tu kwamba maisha yanachangamoto ambazo zinatakiwa kutatuliwa kila siku.Ukitaka kuelewa vizuri juu ya hiki ninachosema, jaribu kumuuliza kila unayekutana naye ' Maisha vipi?' Au mwambie 'maisha yanaendaje?'. Wengi kati yao watakwambia maisha ni magumu sana. Kwa kuwa na Imani hii maisha ni magumu inawarudisha wengi nyuma kimafanikio kwa sababu akili zao zote zinaamini ugumu katika maisha basi na ndivyo inavyokuwa.Soma; Kama Unaona Maisha Ni Magumu Utawezaje Kushinda?
Acha kuamini sana maisha yako ni magumu.
2. Kuahirisha mambo mara kwa mara.Pia wengi wanakwama kufikia mafanikia kwa sababu ya tabia ya kuahirisha mambo. Utakuta mtu anauwezo kabisa wa kufanya jambo fulani muda huu lakini unashangaa anaahirisha. Kwa tabia hiyo ya kuahirisha jambo hili leo na lingine kesho, hupelekea mambo mengi kutokufanyiwa kazi. Matokeo yake mwisho wa siku hujikuta kukwama na kushindwa kufanikiwa. Kwa hiyo kuahirisha mambo ni moja ya tabia inayowarudisha wengi kimafanikio bila hata pengine wao kujua.3. Kulaumu wengine.Wapo wengine pia ambao maisha yao hurudi nyuma kutokana na kulaumu wengine. Unaweza ukashangaa hili linatokeaje? Sikiliza, unapolaumu wengine unakuwa unaona wao ndio wanajukumu la kubadilisha maisha yako na kusahau kwamba jukumu hio unalo wewe. Wewe ndio unayewajibika kwa sehemu kubwa juu ya maisha yako na sio mtu mwngine. Kama utaendelea kulaumu wengine ndio chanzo cha maisha yako kuwa mabaya, tambua kabisa utakuwa umejibebesha tabia ambayo inakurudisha nyuma.Soma; Kama Unataka Mabadiliko Makubwa, Anza kubadili Kitu Hiki Kwanza.4. Kujilinganisha na wengine.Ili uweze kufanikiwa na kufika mbali, acha kujilinganisha sana na watu wengine. Fanya kwa sehemu yako lakini kwa ubora wa hali juu. Ikiwa utaamua kujilinganisha sio mbaya lakini isiwe kupitiliza. Kama utaendelea kujilinganisha sana itakupelekea uendelee kuiga maisha ya wengine sana, ambayo kiuhalisia sio yako. Hivyo, ikiwa unataka kufanikiwa acha kuendeleza tabia hii ya kujilinganisha sana na wengine, itakukwamisha na utashndw kufanikiwa.Kwa sehemu hizo ni baadhi ya tabia mbovu ambazo zinawarudisha wengi nyuma kimafanikio iwe kwa kujua au kutokujua.Tunakutakia kila la kheri na ansante kwa kutembelea AMKA MTANZANIA kwa ajili ya kujifunza.Kwa makala nyingine za mafanikio pia endelea kujifunza kupitia DIRA YA MAFANIKIO kila wakati.Ni wako rafiki,Imani Ngwangwalu,Simu; 0713 048035,Email;dirayamafanikio@gmail.comBlog; dirayamafanikio.blogspot.com  

Article Source: Hisia za Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.