Skip to main content

MFUNGAJI BORA AMIS TAMBWE ‘MR. HAT-TRICK’ VPL 2015/16


Amis Tambwe akishangilia moja ya goli lake alilofunga kwenye mchezo wa leo kati ya Yanga dhidi ya Stand United

Na Baraka Mbolembole

Mshambuliazi wa kimataifa raia wa Burundi, Amis Tambwe amefanikiwa kuvunja rekodi yake mwenyewe ya magoli katika historia ya wachezaji wa kulipwa katika ligi kuu Tanzania bara (VPL).

Mrundi huyo kwa mara ya kwanza alitua Tanzania na kujiunga na Simba SC akitokea Vitalo’O ya kwao Burundi msimu wa 2013/14 na kufanikiwa kushinda tuzo binafsi ya mfungaji bora baada ya kufunga jumla ya magoli 19.

Awali kabla ya ujio wa Tambwe mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Boniface Ambani alikuwa akishikilia rekodi ya mfungaji wa magoli mengi zaidi kwa msimu kwa wachezaji wa kigeni, si hivyo tu, Ambani aliweka rekodi ya mshambulizi aliyefunga magoli mengi zaidi (17) akicheza msimu wake wa kwanza VPL.

Lakini huyu Tambwe ‘Mr. hat-trick’ ni balaa. Ni mfano bora zaidi wa kulipwa na bila shaka vijana wengi washambuliaji wa baadaye watakuwa wakijifunza namna mchezaji huyo alivyo stadi kiufungaji. Utulivu wake, ufuatiliaji wake wa ‘move’ za mchezo, uwezo wake wa kujipanga, kutumia nafasi, kujitengenezea nafasi yeye mwenyewe na kutengeneza nafasi za kufunga kwa wachezaji wenzake.

Tambwe alifunga jumla ya magoli 15 msimu uliopita akichezea Simba hadi nusu ya msimu kisha kujiunga na Yanga baada ya kutemwa na timu yake hiyo ya kwanza Tanzania kwa madai ya kuporomoka kwa kiwango chake chini ya mkufunzi Mzambia, Patrick Phiri.

Yanga ilifanya usajili wa Tambwe muda mfupi baada ya kumtimua aliyekuwa kocha wao Mbrazil, Marcio Maximo mwezi Disemba, 2014. Chini ya Mholland. Hans Van der Pluijm, Tambwe amefanikiwa kufunga jumla ya magoli 35 katika VPL pekee katika kipindi cha miezi 14 waliyofanya kazi pamoja klabuni Yanga.

Jumanne hii, Mrundi huyo amefanikiwa kufunga goli lake la 20 msimu huu huku zikiwa zimesalia game nne kabla ya kumalizika kwa msimu. Tambwe ni mtulivu licha ya siku za karibuni baadhi ya watu kudai kwamba kiwango chake kimeshuka jambo ambolo si la kweli.

“Nina cheza vizuri na kuisaidia timu yangu kupata ushindi. Watu wanataka kuniona nikifunga kila mara na inapotokea sifungi wanasema nimeshuka kiwango. Wanatakiwa kutazama na mchango wangu kwa wachezaji wengine, si lazima nifunge mimi lakini nachukia kumaliza mechi bila kufunga”.

Anasema mshambulizi huyo wakati nilipofanya nae mahojiano mafupi kwa njia ya mtandao baada ya kufunga goli lake la 20 msimu huu na kuisaidia Yanga kushinda 3-1 ugenini dhidi ya Stand United katika game ambayo ilishuhudiwa mshambulizi-pacha wake, Donald Ngoma akizamisha magoli mawili, goli moja kwa usaidizi wa Tambwe.

Goli lake hilo limemfanya kumpiku mshambulizi Mganda, Hamis Kizza ambaye hadi kufikia mchezo wa 22 wa timu yake ya Simba alikuwa amefunga magoli 19 ambayo amesimamia hapo hadi sasa. Wakati timu yake ikihitaji pointi tatu tu baada ya game ya Azam FC siku ya Jumatano, Tambwe amefunga magoli 20 kati ya 61 ya timu yake ambayo katika michezo 26 ya msimu uliopita ilifanikiwa kufunga jumla ya magoli 52 kwa msimu wote. Yanga imefunga jumla ya magoli 61 katika michezo 26 ya msimu huu (magoli 9 zaidi ya msimu uliopita).

Wakati msimu uliopita katika ligi iliyokuwa na michezo 26, Yanga waliruhusu nyavu zao mara 18 msimu huu wamepelekwa nyavuni mara 15 (magoli matatu pungufu ya yale ya msimu uliopita.

Bila shaka ubingwa utaenda tena Yanga msimu huu, na Tambwe atatetea tuzo binafsi ya ufungaji bora ambayo alishuhudia ikienda kwa mchezaji mwenzake wa Yanga, Saimon Msuva msimu uliopita baada ya kufunga jumla ya magoli 17 (magoli mawili zaidi yake).

Tambwe amefunga jumla ya magoli 54 katika msimu wake wa tatu VPL. Hakuna mkali wa nyavu kama Mrundi huyu. Mfalme wa magoli ya kichwa.INtoka kwa  Shaffih Dauda

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.