Skip to main content

Posts

Showing posts from April, 2014

Warioba atunukiwa nishani iliyotukuka.

Na Hudugu Ng'amilo Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba juzi usiku alikuwa miongoni mwa viongozi na watu mashuhuri waliotunukiwa nishani na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam. Katika maelezo ya kutoa nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano daraja la kwanza, ilielezwa kuwa Jaji Warioba, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliuenzi na bado anauenzi Muungano huo. "Katika kipindi chako, pamoja na nyadhifa nyingine, ulikuwa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani...katika kipindi hicho na hadi sasa umeendelea kuwa mwaminifu, umeutunza, umeulinda na umeuenzi Muungano," ilisema sehemu ya taarifa ya kutoa nishani. Hivi karibuni, Jaji Warioba amekuwa akishambuliwa na baadhi ya Wajumbe wa Bunge la Maalumu la Katiba, pia baadhi ya wana CCM kutokana na Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyoiong

Kuwa Mzalendo Sambaza Upendo

MISS ILALA 2013 DORIS MOLLEL AKABIDHI VITABU 50 SHULE YA MSINGI PUGU DAR

Miss Ilala 2013, Doris Mollel ijumaa ya wiki iliyopita alitembelea shule ya msingi Pugu jijini Dar es Salaam na kukabidhi vitabu 50 za hadithi kwa wanafunzi wa shule hiyo katika harakati zake binafsi za kuwajengea wanafunzi na watoto utamaduni na tabia ya kujisomea kwenye umri mdogo. Miss Ilala huyo wa mwaka 2013 alitumia nafasi hiyo kuwahamasisha wanafunzi kujisomea kama ufunguo wa maisha yao ya baadaye. Miss Ilala 2013, Doris Mollel, akisaini kitabu cha wageni baada ya kutembea shule hiyo ya msingi Pugu jijini Dar es Salaam. Doris Mollel akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo ya msingi ya Pugu muda mfupi baada ya kukabidhi vitabu hivyo. Miss Ilala 2013, Doris Mollel akimkabidhi vitabu Mwalimu Josephine Matiku kwenye hafla rasmi ya makabidhiano shule hapo ijumaa iliyopita jijini Dar. Miss Ilala 2013, Doris Mollel akipozi na walimu wa shule hiyo wakati wa halfa ya kukabidhi vitabu. Miss Ilala 2013, Doris Mollel katika picha ya pamoja na baadhi ya wan

JK ATUMA RAMBIRAMBI KIFO CHA GURUMO

RAIS Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kutokana na kifo cha mwanamuziki maarufu na wa siku nyingi, Muhidini Gurumo kilichotokea juzi mjini Dar es Salaam. Gurumo alifariki dunia juzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya ugonjwa wa moyo uliomsumbua kwa muda mrefu. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Rais Kikwete alisema mchango wa marehemu Gurumo kwa Taifa ni mkubwa na wa kupigiwa mfano kupitia kipaji alichojaaliwa na Mwenyezi Mungu ambacho alikitumia kikamilifu kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla. “Nimesikitishwa na kuhuzunishwa na taarifa za kifo cha Gurumo ambaye alikuwa mmoja wa wasanii wa muziki wa dansi nchini waliolitumikia Taifa hili kwa bidii tangu miaka ya sitini kupitia sanaa ya muziki, Katika bendi mbalimbali za muziki wa dansi kuanzia Bendi ya NUTA Jazz, Mlimani Park Orchestra, Orchestra

Mripuko wauwa 71 Abuja

Hali ya taharuki kufuatia mripuko katika kituo cha basi katika kiunga cha Abuja,Nigeria. (14.04.2014) Tuhuma zinaelekezwa dhidi ya kundi la Boko Haram juu ya kwamba hakuna taarifa ya kudai kuhusika na shambulio hilo kutoka kwa wapiganaji hao wa itikadi kali za Kiislamu ambapo hasa wamekuwa wakiendesha zaidi harakati zao kaskazini mashariki mwa Nigeria.Mbali ya watu 71 waliouwawa polisi imesema watu 124 wamejeruhiwa katika shambulio hilo ambalo ni la kwanza kufanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo katika kipindi cha miaka miwili. Kamadori wa kikosi cha anga Charles Otengbade ambaye ni mkurugenzi wa oporesheni za msako na uokozi amesema wataalamu wa usalama wanashuku kwamba bomu hilo limeripuka likiwa ndani ya basi. Mabaki ya maiti za watu zilizorowa damu ilikuwa imetapakaa kila mahala wakati vikosi vya usalama vikihangaika kudhibiti umma wa watu uliokuwa umezonga kutaka kujuwa kilichojiri na askari wa zima moto wakilimwagi

Tundu Lissu atikisa Bunge

Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu.PICHA|MAKTABA Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu amesema Tanganyika ilikufa kwa amri iliyotolewa na Mwalimu Julius Nyerere na siyo kwa makubaliano katika hati ya Muungano. Lissu alitoa kauli hiyo jana alipopata fursa ya kukamilisha dakika 16 za hotuba yake ya ufafanuzi wa maoni ya walio wachache iliyokuwa imekatishwa baada ya matangazo ya moja kwa moja ya Televisheni ya Taifa (TBC1) kukatika Jumamosi iliyopita. Huku akinukuu maneno yaliyopo katika vitabu vilivyoandikwa na Profesa Issa Shivji na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa, Lissu alisema Jamhuri ya Muungano ilizaliwa bila uhalali wa kisheria kwa kuwa hayakuwapo makubaliano ya kila upande wa Muungano. Alisema Aprili 26, 1964 (Siku ya Muungano), Mwalimu Nyerere alitoa amri ya masharti ya mpito ya mwaka 1964 ambayo pamoja na mambo mengine iliifuta Tanganyika. Akichambua kitabu cha &

Bilal, Magufuli,Kova wanusurika kifo ajali ya helikopta Dar

Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Ghalib Bilal amenusurika kifo katika ajali ya helikopta iliyoanguka katika Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam ilipokuwa ikiruka kwenda kukagua madhara ya mafuriko. Pamoja na Dk. Bilal, wengine walionusurika kifo katika ajali hiyo ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick na Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambao walipata majeraha madogo. Taarifa za ajali hiyo zikiambatana na picha kadhaa za helikopta hiyo ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na baadaye kuthibitishwa na Mkuu wa Majeshi (CDF), Jenerali Davis Mwamunyange. Helikopta iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal baada ya kuanguka jana katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana. Mwamunyange afafanua Akizungumza na mwandishi wetu, Jenerali Mwamunyange alisema ajali hiyo ilihusish

Ukraine ,Rais awaonya wapinzani

Rais wa Ukraine awaonya waasi Mashariki mwa nchi Kaimu Rais wa Uraine, Oleksandr Turchynov,amewapa wapiganaji wanaounga mkono Urusi hadi mwisho wa leo Jumatatu kuondoka kutoka katika majengo ya serikali katika miji ya mashariki mwa Nchi hiyo la sivyo wakabiliwe na jeshi la Ukraine wazalendo. Bwana Turchynov amesema kuwa iwapo waasi hao hawatatii makataa hayo ya leo asubuhi, majeshi ya Ukraine yatatekeleza kile alichokitaja kuwa mashambulizi rasmi dhidi ya ugaidi. (MM) Katika hotuba ya runinga, rais huyo wa muda amesema kuwa hatokubali kuona kilichofanyika Crimea mwezi uliopita kikirudiwa tena nchini mwake. Huku hayo yakijiri ,Urusi imelaani tahadhari hiyo ya Bwana Turchynov , ikiishutumu serikali ya Ukraine kwa kutangaza vita dhidhi ya watu wake . Urusi imepinga vikali tetesi za Marekani na Ukraine kuwa ndiyo inayochochea ghasia hizo na uasi katika miji iliyoko mashariki mwa Ukraine . Urusi imesisitiza

Wakenya washinda mbio za Marathon za London

Wilson Kipsang, wa Kenya akimaliza kama mshinda wa mbio za Marathon za London 2014 Kijiji cha Iten nchini Kenya kilijitangazia kuwa "makazi bingwa wa mbio za masafa marefu" kufuatia mazingira yaliyojionesha Jumapili kijijini hapo kwenye mji mkuu wa kaunti ya Elgeyo Maraket kufuatia ushindi wa pili wa Wilson Kiprotich Kipsang kwenye mbio ndefu zijulikanazo London Marathon zilizofanyika jijini London , Uingereza. Kipsang alivunja rekodi kwenye mbio za "London Marathon" kwa kukimbia kwa muda wa saa mbili, dakika nne na sekunde 27. Aliibuka mshindi dakika chache baada ya jirani yake kutoka kijiji hicho hicho cha Iten na mshindi wa mara mbili duniani, Ednah Ngeringwony Kiplagat alishinda mbio za wanawake kwa kutumia saa mbili dakika 20 na sekunde 21 huku akimshinda mwanamke mwingine mkazi wa kijiji cha Iten, Florence Kiplagat. Kipsang na Kiplagat wanaishi umbali wa mita 700 kutoka kila moja katika eneo la

IPHONE KWENYE HARUSI :WAGENI WAALIKWA WATAKATA

Kibongo bongo tumezoea mtu anapotaka kufunga ndoa lazima ipitishwe michango ya kutosha ili kuweza kufanikisha sherehe, na pia mchango wako ndio huwa kiingilio chako yaani bila kuchanga hupati mwaliko. Hizi ni zawadi za iPhone 5 walizopewa wageni waalikwa Mambo yamekuwa kinyume katika harusi ya mtoto wa kike wa Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria aitwaye Faith, ambaye katika harusi yake iliyofanyika jana (April 12) wageni walioalikwa wamefanyiwa surprise kwa kupewa zawadi ya simu za iPhone 5 ‘gold plated customized’, zilizoandikwa majina ya maharusi hao Faith na Godswill. Juu ya mabox yaliyokuwa na zawadi ya simu hizo pameandikwa ‘Leeberry and her Prince wish you all the best for making our day beautifull. Thanx for coming and God Bless you’ Cha kusikitisha ni kwamba aina ya wageni wanaoweza kupata mwaliko wa harusi kama hii ya mtoto wa mkubwa ni watu wa class flani ya watu wanaojiweza, hivyo unaweza kukuta ni mtu ambaye tayari anayemiliki hata iPhones mbili au t

UJIO WA QUEEN DRLEEN- WANATETEMEKA FT SHILOLE

 

TBC biased, Mbowe claims

  Member of the Constituent Assembly Tundu Lissu stresses a point in one of the House sessions in Dodoma recently. On Saturday TBC live broadcasts, both  TV and radio were disconnected as he made a presentation due to what was explained as a consequence of hostile weather in Dar es Salaam.   PHOTO | SALHIM SHAO.  Dodoma.  The Coalition of Defenders of the People’s Constitution (Ukawa) has accused Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) of deliberately interrupting coverage of the Constituent Assembly session on Saturday. Ukawa chairman Freeman Mbowe said yesterday that the move meant to favour CCM interests in the assembly. Mr Mbowe said by shutting down live television and radio coverage of the CA debate when Tundu Lissu was presenting minority views was proof of the State broadcaster’s ill motive  towards those with a divergent opnion. “Lissu’s case should not be taken in isolation. If you follow keenly on their reportage, you will agree with me that all TB

JK :ATEMBELEA MAENEO YALIYOKUMBWA NA MAFURIKO MKOA WA PWANI

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na Mkewe Mama Salma Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza wakikagua athari za mafuriko zilizoharibu vibaya barabara ya Chalinze- Dar es Salaam eneo la Ruvu Darajani leo.Mamia ya abiria walikuwa wamekwama kutokana na mafuriko hayo. (picha na Freddy Maro)

BUSHIRI KOCHA BORA LIGI KUU ZANZIBAR

Makamu Mwenyekiti wa BMZ Khamis Said, kushoto akimkabidhi Cheki ya shilingi milioni moja Kocha Bora wa Ligi Kuu ya Grand Malt, Ali Bushiri wa Timu ya KMKM.inatoka kwa mdau.

Mkutano wa 32 wa Sekta ya Fedha, Soko la Mitaji na Mifuko ya Jamii

Na Mwandishi wetu  MKURUGENZI wa Mfuko unaosimamia mifuko ya hifadhi za Jamii nchini (SSRA) , Irene Isaka ametoa wito kwa wanachama wapya kujiunga kwa wingi kwenye mifuko hiyo kwa sababu muda si mrefu serikali itaweka uwiano wa mafao sawa kwa mifuko yote. Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano wa 32 wa Sekta ya Fedha, Soko la Mitaji na Mifuko ya Jamii (CISNA) wakiendelea na Mkutano huo uliofunguliwa rasmi jana April 10, 2014 na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Peter Ilomo (katikati mwenye tai nyekundu).  Isaka alisema hayo jana katika mkutano wa 32 ambao unazikutanisha nchi wanachama wa SADC unaendelea jijini Dar es Salam. “ Tukiwa katika mkutano huu tunaweza kujifunza mambo mengi kutoka kwa wenzetu wa SADC huku na wao wakijifunza mambo kadhaa kutoka kwetu kwani zipo baadhi ya nchi ambazo hazina mfuko mkuu kama SSRA ambao ndio mfuko mama unaosimamkia kazi na utendaji wa mifuko mingine ya kijamii” alisema Isaka. Aliongeza kwa kusema kuwa hivi sasa kumezuka mtind

JUMUIYA YA WAZAZI CCM MKOA WA MOROGOR WASISITIZA SERIKALI MBILI

 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Morogoro  Mh Abdalah Shaweji Akisikiliza kwa Makini Taarifa za Chama cha Mapinduzi alipowasili wilayani Mvomero kweny Maadhimisho ya Sherehe za Siku ya Wazazi Mkoani Morogoro. Katibu wa Jumuiya Hiyo alifanya Shuguli Mbalimbali Ikiwemo Kupanda miti Kufungua Mashina ya Chama cha Mapinduzi Pamoja na Kukabishi kadi za Uwanachama ambapo Jumla ya Wanachama 150 walijiunga na umoja wa wazazi. Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Morogoro  Mh Abdalah Shaweji Akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ofisi za CCM Wilaya ya Mvomero Wajumbe wa Kmatai ya Utekelezaji wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Morogoro Wakisaini kitabu cha wageni kwenye Ofisi za CCM Wilaya ya Mvomero.   Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Morogoro  Mh Abdalah Shaweji aliyevaa Miwani Akipatiwa maelezo kuhusu kilimo cha Mpunga kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Mkindo kata ya Hembeti Wilaya ya Mvomero ikiwa ni Maadhimisho y

Ningelikuwa mjumbe Bunge Maalum la Katiba...

 Mjengwa NINGELIKUWA Mjumbe kwenye Bunge Maalumu la Katiba msimamo wangu ungelikuwa wa dhahiri kwenye hoja ya Muungano na hata namna ya upigaji kura; kwamba ningepigia kura Muundo wa Serikali Tatu, na hivyo uwepo wa Tanganyika, na ningependelea upigaji kura kwenye masuala muhimu uwe wa SIRI. (Hudugu Ng'amilo) Lakini, kwa vile mimi ni muumini wa nchi yangu niliyozaliwa, hata kama wenye mitazamo sawa na mimi tungeshindwa kwa wingi wa kura, basi, ningebaki na misimamo yangu na hata kuendelea kuipigia debe kuwashawishi wengine, lakini, ningefanya yote kuunga mkono kilichoamuliwa na wengi. Na hapa ndipo ulipo msingi wa hoja yangu, kuwa Katiba ni Maridhiano. Maana, nimepata kuandika, kuwa MARIDHIANO ndio msingi wa UHALALI wa mchakato na hata Katiba yenyewe. Na ndiyo maana ya ukomavu wa kisiasa na kiuongozi. Nilifarijika sana kuwaona na kuwasikia Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Vuai Ali Vuai (CCM) na John Mnyika (CHADEMA). Waliongea maneno ya h

TAZAMA JINSI WAKIMBIZI WANAVYO ZAMIA NCHINI UINGIREZA

Ikiwa ni wiki iliopita tu wakimbizi wanne kuuliwa maeneo ya Calais, basi wameonekana wengine wakiwa wanaingia kwenye lori hilo huku hatma yao ijajulikana kama walifanikiwa au walishindwa.... Ni kitu cha kawaida kuona wakimbizi wakiingia nchini Uingereza ila wengi wao huishia kufariki kwani ni hatari sana   Siku kadhaa sasa imekua ikisikika wakimbizi wanakufa wakiwa wanajaribu kuingia Uingereza kinyemera, Picha hizi zimepigwa na mmoja wa muandishi alipowaona wakimbizi wakiwa waningia katika moja ya lori lililokua linatembea kuelekea katika jiji la Manchester, lori hilo lililokua lipo maeneo ya Calais.        

Jimmy Master Kung'ara katika ujio wa Jamal

Baa ya kuchelewa kuingia sokoni mwaka jana sasa filamu hiyo iliyo wakutanisha wakongwe   wawili katika tasnia ya filamu nchini Jimmy Master na Fike ‘The Wild Cat’ Wilson wakiwa wamekutana katika filamu moja iitwayo Jamal ambayo ikombioni kuingia sokoni.

Mwelekeo wa Kimbunga "HELLEN" na hali ya Mvua

Mamlaka ya Hali ya Hewa imeendelea kufuatilia kwa karibu mifumo ya hali ya hewa na mabadiliko yake pamoja na adhari zake kwa Nchi yetu na kutoa utabiri na tahadhari za hali mbaya ya hewa. Tarahe 28 Machi 2014 mgandamizo mdogo wa hewa katika eneo la Rasi ya Msumbiji kusini magharibi mwa bahari ya Hindi ulianza kuimarika zaidi na kusababisha kuwepo kwa makutano ya upepo na mwelekeo wa vipindi vya mvua kubwa katika maeneo mengi nchini. Tarehe 29 Machi 2014 mgandamizo huo wa hewa (Tropical Depression) uliimarika zaidi na kuwa kimbunga kilichopewa jina 'Hellen' (Tropical Cyclone) uchambuzi ulionesha kuwa kimbunga 'Hellen' kilitarajiwa kuongezeka nguvu (Severe Tropical Cyclone) na kusababisha aongezeko zaidi la mvua na upepo mkali. Hivyo maeneo yafuatayo yalitabiriwa kuwa na adhari zaidi za mabadiliko hayo kuanzia tarehe 30 Machi hadi 01 April 2014 ; Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam

RIDHIWANI KUANZA NA BARABARA KISHA ELIMU NA AFYA

 Ridhiwani Kikwete akihutubia wakazi wa kijiji cha Tokamisasa wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge zinazoendelea ambapo aliwaambia kuwa atahakikisha tatizo la wakulima na wafugaji kwa kuweka mpango bora wa matumizi ya ardhi. Ridhiwani Kikwete akihutubia wakazi wa kijiji cha Tokamisasa wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge zinazoendelea ambapo aliwaambia kuwa atahakikisha tatizo la huduma za afya linatatuliwa, kuboresha miundo mbinu elimu na kurudisha michezo jimboni. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete akicheza muziki na Miraji Mtaturu Katibu wa CCM  Wilaya ya Mufindi wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge jimbo la Chalinze uliofanyika kwenye kitongoji cha Mbuyu kijiji cha Tokamisasa kata ya Ubena Zomozi. Sam wa Ukweli akitumbuiza kwenye kampeni za CCM zilizofanyika katika kijiji cha Tokamisasa kitongoji cha Mbuyu.   Mgombea wa Ubunge wa jimbo la Chalinze CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete