Skip to main content

Ningelikuwa mjumbe Bunge Maalum la Katiba...

mjengwa maggid d613f
 Mjengwa

NINGELIKUWA Mjumbe kwenye Bunge Maalumu la Katiba msimamo wangu ungelikuwa wa dhahiri kwenye hoja ya Muungano na hata namna ya upigaji kura; kwamba ningepigia kura Muundo wa Serikali Tatu, na hivyo uwepo wa Tanganyika, na ningependelea upigaji kura kwenye masuala muhimu uwe wa SIRI.(Hudugu Ng'amilo)
Lakini, kwa vile mimi ni muumini wa nchi yangu niliyozaliwa, hata kama wenye mitazamo sawa na mimi tungeshindwa kwa wingi wa kura, basi, ningebaki na misimamo yangu na hata kuendelea kuipigia debe kuwashawishi wengine, lakini, ningefanya yote kuunga mkono kilichoamuliwa na wengi. Na hapa ndipo ulipo msingi wa hoja yangu, kuwa Katiba ni Maridhiano.
Maana, nimepata kuandika, kuwa MARIDHIANO ndio msingi wa UHALALI wa mchakato na hata Katiba yenyewe. Na ndiyo maana ya ukomavu wa kisiasa na kiuongozi.
Nilifarijika sana kuwaona na kuwasikia Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Vuai Ali Vuai (CCM) na John Mnyika (CHADEMA). Waliongea maneno ya hekima na busara sana. Wote hawa ndio waliounda Kamati ya Maridhiano juu ya suala la kura ya Siri au Wazi.
Na kauli za wajumbe hao niliowataja zilifunikwa na kawa lililofumwa kwa maneno yenye hekima na busara kutoka kwa Askofu Donald Mtetemela aliyewawakilisha viongozi wengine wa kidini waliokuwamo kwenye kikao cha Kamati ya Mariadhiano.
Askofu Mtetemela alisema; pamoja na tofauti zilizozijitokeza, pande mbili zimekubaliana kuacha kung'ang'ania misimamo yao ili tusonge mbele katika kutimiza lengo la kupata Katiba Mpya.
Hivyo, inanisikitisha ninaposoma habari kuwa wanaharakati wa Jukwaa la Katiba kuwa wanapanga kulivunja Bunge kwa vile limetafuna bilioni 80. Siioni busara na hekima ya wao wanaharakati kufikia hitimisho hili huku wakifahamu kuwa hapa tulipofikia ni moja ya hatua muhimu kwenye mchakato na pengine harakati za Watanzania kupata Katiba iliyo bora kuliko ile ya mwaka 1977 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 1984.
Sasa kama wanaharakati wa Jukwaa la Katiba wanatumia muda na fedha kuandaa maandamano ya nchi nzima kwa madhumuni ya kuvunja Bunge Maalumu la Katiba, swali, ni ili iweje? Kuna haja ya wanaohusika na mipango hii kujitafakari upya. Ningedhani wangetumia rasilimali walizonazo kwenye kutoa elimu zaidi kwa wananchi juu ya Rasimu ya Katiba na yaliyomo. Kuwapa mwanga zaidi wananchi katika kuyaelewa wanayojadili wabunge wao.
Hii ni nchi yetu sote. Na hili la Katiba ni mchakato. Tusiwe wepesi wa kukata tamaa. Ni vema na ni busara tukaupa nafasi na kuendelea kuunga mkono mchakato wa Katiba unaoendelea sasa.
Chanzo Raia mwema.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...