Skip to main content

Ningelikuwa mjumbe Bunge Maalum la Katiba...

mjengwa maggid d613f
 Mjengwa

NINGELIKUWA Mjumbe kwenye Bunge Maalumu la Katiba msimamo wangu ungelikuwa wa dhahiri kwenye hoja ya Muungano na hata namna ya upigaji kura; kwamba ningepigia kura Muundo wa Serikali Tatu, na hivyo uwepo wa Tanganyika, na ningependelea upigaji kura kwenye masuala muhimu uwe wa SIRI.(Hudugu Ng'amilo)
Lakini, kwa vile mimi ni muumini wa nchi yangu niliyozaliwa, hata kama wenye mitazamo sawa na mimi tungeshindwa kwa wingi wa kura, basi, ningebaki na misimamo yangu na hata kuendelea kuipigia debe kuwashawishi wengine, lakini, ningefanya yote kuunga mkono kilichoamuliwa na wengi. Na hapa ndipo ulipo msingi wa hoja yangu, kuwa Katiba ni Maridhiano.
Maana, nimepata kuandika, kuwa MARIDHIANO ndio msingi wa UHALALI wa mchakato na hata Katiba yenyewe. Na ndiyo maana ya ukomavu wa kisiasa na kiuongozi.
Nilifarijika sana kuwaona na kuwasikia Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Vuai Ali Vuai (CCM) na John Mnyika (CHADEMA). Waliongea maneno ya hekima na busara sana. Wote hawa ndio waliounda Kamati ya Maridhiano juu ya suala la kura ya Siri au Wazi.
Na kauli za wajumbe hao niliowataja zilifunikwa na kawa lililofumwa kwa maneno yenye hekima na busara kutoka kwa Askofu Donald Mtetemela aliyewawakilisha viongozi wengine wa kidini waliokuwamo kwenye kikao cha Kamati ya Mariadhiano.
Askofu Mtetemela alisema; pamoja na tofauti zilizozijitokeza, pande mbili zimekubaliana kuacha kung'ang'ania misimamo yao ili tusonge mbele katika kutimiza lengo la kupata Katiba Mpya.
Hivyo, inanisikitisha ninaposoma habari kuwa wanaharakati wa Jukwaa la Katiba kuwa wanapanga kulivunja Bunge kwa vile limetafuna bilioni 80. Siioni busara na hekima ya wao wanaharakati kufikia hitimisho hili huku wakifahamu kuwa hapa tulipofikia ni moja ya hatua muhimu kwenye mchakato na pengine harakati za Watanzania kupata Katiba iliyo bora kuliko ile ya mwaka 1977 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 1984.
Sasa kama wanaharakati wa Jukwaa la Katiba wanatumia muda na fedha kuandaa maandamano ya nchi nzima kwa madhumuni ya kuvunja Bunge Maalumu la Katiba, swali, ni ili iweje? Kuna haja ya wanaohusika na mipango hii kujitafakari upya. Ningedhani wangetumia rasilimali walizonazo kwenye kutoa elimu zaidi kwa wananchi juu ya Rasimu ya Katiba na yaliyomo. Kuwapa mwanga zaidi wananchi katika kuyaelewa wanayojadili wabunge wao.
Hii ni nchi yetu sote. Na hili la Katiba ni mchakato. Tusiwe wepesi wa kukata tamaa. Ni vema na ni busara tukaupa nafasi na kuendelea kuunga mkono mchakato wa Katiba unaoendelea sasa.
Chanzo Raia mwema.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.