Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2009

Dj Venture Pichani akicheki Hali ya Mambo Mzalendo Pub

CHEKI hapa ni kwenye jengo la Millenium Towe lipo maeneo ya Kijitonyama Dar es Salaam , kama unavyoona Pichani kwa mbali kuna vijana watatu wakicheki bidhaa flani flani , ukudisko la kufamtu likilindima , kwa mbele pembeni anapo piga disko mkali Bon Luv na dj Mackay. Wakati huu ilikuwa jumamosi usiku wa manane , jengo hilo uporomoshwa diskola kufamtu kila jumamosi ndani humo humo sehemu hii twayo Mzalendo Pup. Upigwa nyimbo za Old Schoo, Hip Hop ,R&B ,Mayenu na sasa kunakitu kilicho chomoza kinaitwa mziki wa Mduara usiku ua unabadilika Mduara kwa Mabinti kwa sasa panaumaarufu huo wa kutwanga pia muziki wa aina hiyo. Pichani mbele ni Dj Venture katika usiku huo , yeye ua ni muongeaji wa disko hilo katika vyo mbo vya habari. Jengo hilo linauduma kem kem pia kuna duka la mchoraji maarufu Masudi kipanya , Bank zote yaani ATM , moja wapo ikiwa ni ATM ya CRDB Bank.

Mtoto wa Familia ya Marco Tibasima Mercy Akiwa na Uso wenye Mwonekano wa Furaha

Mercy ni mtoto wa mwisho katika familia hiyo ya Tibasma.

MOJA YA PICHA KATIKA MATUKIO YA SIKUKUU YA EID EL HAJ J NI PICHA YA FAMILIA YA MARCO TIBASIMA

Du Hapa ni Wakati Flani hivi na Huyu ni Mamaa mke wa Mchoraji Maarufu wa Michoro Nchini Hapa.

PICHANI mke wa mchoraji Marco Tibasima aitwaye Riziki , akiwa ameketi sofani akicheki mambo ya familia yake .

MARCO TIBASIMA UNATISHA ..... !!!!!!!

MCHORAJI mahiri wa michoro Marco Tibasima akiwa ameketi maskani yake Kinondoni ambapo alikutwa na blog hii . Tibasima ambaye ni mchoraji mwenye mafanikio , jamaa ni mfano mzruri wa guigwa kutokana na mafanikio aliyoyapata tangu aanze fani hiyo ya uchoraji nimengi sana ambayo ameisha yafanya katika jamii. Pia anamiliki Jarida la Bantu ila tu jamaa yuko bize sana hatua aliyopita mpaka sasa nimmoja wa watu wa mfanomzuri wa kuiga. Alianza hatua ya uchoraji akiwa jijini Mwanza na kikubwa anaukaribu Mkubwa sana na Mzee Bawj , nimtu mwenye umaarufu kupitia kazi zake katika sanaa ya michoro nimtu wa kufikiria anakotoka na anako kwenda blog iliongea naye mengi tu, siku ya sikukuu ya Eid E l Hajj hakiwa home kwake na familia yake.

MERY RUKOSI SASA KUKAMUA NA MOMBA BEND

MSANII mpya Mery Rukosi ambaye kipaji chake kimeanzia kuonekana kwenye shindano la kusaka vipaji vya muziki maarufu kwajina la Bongo Star Seach . kwasasa yupo katika bendi mpya yaiitwayo 'Mjomba Band' inayomilikiwa na msanii mahiri wa mashahiri Mrisho Mpoto. Alhamisi mchana wiki iliyopita alifanya vizuri akiwa na bendi yake hiyo kwenye ukumbi Ubungo Plaza wakati wa maadhimisho ya nane ya siku Mlipa Kodi Tanzania. "Tayari bendi yetu hii , tunajipanga ilikuja na nyimbo zetu kwanihadi sasa bado hatuja rekodi nyimbo yeyote ,"alisema Rukosi . Katika Maadhimisho hayo ya nne ya siku ya Mlipa Kodi kundi hilo lilijipanga vyema na kutoa burudani safi mbele ya wageni waalikwa ambapo Mgeni rasimi alikuwa ni Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo . Kundi hilo la 'Mjomba Band' liliimba wimbo mpya wa uliotungwa kwa ajili ya siku hiyo na vibao vingine kama wimbo wa 'Mjomba' ambao unajulikana kwa wapenzi wengi wa muziki nchini. Hadi sasa kundi hilo la 'Mjom

HUYU NDIYE FIKE WILYSON

POWER OF GOD KUTUA MADUKANI

FILAM mpya ya Power Of God muda wowote kuanzia sasa itatingakwenyesoko la filamu nchini. Kwa mujibu wa muandaaji wa filamu hiyo Fike Wilyson amesema kuwa katikaujio huo , amemshirikisha bondia Charles (Spinks), Mhilu ambaye ni bingwawazamani wa Tanzania katika uzani wa Walter na pia alipata kuwa kocha wa bingwawa Dunia Magoma shabani ,bingwa wa Afrika mambeya Bakari, hii ni filamu yakwanza akicheza kama kocha wa ngumi. Wengine Walioshiriki ni Francis Miyeyusho ,bingwa wa ngumi wa Afrika Mashariki ndani ya muvi hiyo ameshiriki kama mwanafunzi wa ngumi ndni ya Gym ,ni filamu yake ya kwanza kuwa muigizaji. Fike aliwai kuwa Mr Tanzania mara 2, mwaka 2002 na 2004pia aliwai kushikilia mkanda wa ndondi za kuliwa. Fike alishawai kupasua anga na kuishi katika majimbo maarufu ya ndondi duniani kamajimbo la Pennsylvania . Philadelphia ambalo ni jimbo linaloongoza kwa ubora wa wapiganaji wa kiwango cha kidunia cha ndondi likifuatiwa na jimbo la Detroit Michigan japokuwamapambano mengi ya

Andrew Michael NKUBI 'ANDRE 14, X5, MSOME HAPA ANANINI? NI BONGE LA MKALI

A Hapa alikuwa na Blog hii pande za Mwananyamala juzi kwenye Barbeshop moja ya kijana wa The rock City Amiri. Ngoma ambazo alisha wahi kuzitengeneza ni 'Nilikuwepo','Club Shavu' na 'Zawadi ambazo ni za msanii nguli wa Mwanza Dr KB. Jamaa anamaujanja mengi tayari ameisha shirikiana na Studio za Amerika kama Reel Time Studio's katika jimbo la (Kansas City - USA). Awali alimaliza masomo yake ya kidatocha SIX pale Bogu Sekondari .

CHID MZEE WA MBELE ABAMBWA NA Blog HII JANA SAA NNE HASUBUI

Blog hii ilimkuta akiwa Mangogarden Barbeshop , kama anavyoonekana pichani. Chd amekuwa aking'ala kwenye kundi la Bongo Dar es Salaam. Ambapo kipindi hicho Urushwa hewani na katika Luninga moja nchini , licha ya hivyo jamaa ni Promota wa Ngumi nchini hapa.

Gari ya Chd Mzee wa Bele ikiwa imepaki Angaza Mwananyamala Jana.

Baadhi ya mabondia watakao zitwanga leo jiono , wakiteta ilina lile baada ya kuwa wametoka kupima HIV. Du wengi vipimo vilionesha wako poa ndio mada hasa iliyokuwa ikitetwa hapo , kama unavyo waona pichani. Pia Mzee wa Mbele kama mdau wa ngumi halikuwepo katika masimilizi hayo.

Jana Pale Mabondia Walipo Pima HIV 'Ngoma'

MAPAMBANO ya ndondi yatakayofanyika katika Ukumbi wa Umoja Club , MwananyamalaMapinduzi -KINONDONI leo. Cruiserweight Ramandhani Kido Vs Kaminja Ramadhani. Light middle Lucas Benard Vs Mbwana Ally Mohd (Van Dame). Light Midd weght Ibrahim 'Big Right' Vs PaulMsela. Light Welter Weight Jafary Majia (Mr Nice) Vs Ibrahim Amedeus (Star Boy). Light Weight Mussa (Sunga Boy) Vs Josefat John. Fly Weight Becka Mackenzie (Mdachi) Vs Athmani Hsasan. Light Fly Weight Sadat Miyeyusho Vs Ali Hassan. Said (Chaku Master) V/s Daud Mhunzi. Jana Rais wa Shirikisho la Masumbwi Tanzania (TST), pichani katikati Emmanuel Mlundwa aliongozana na baadhi ya mabondia kwenda kupima HIV , Angaza Mwananyamala.

Hili ni Jengo la Angaza Mwananyama walipo Pima HIV Wanamasumbi jana!!

Nyumba hii jana Wanamasumbi walifika na kupimwa HIV.

Haya ni Mambo ya Masiga Msome kwa Sasa Yeye Ananini !!

MSANII wa muziki wa Bongofleva Masiga Alex 'masiga' ,ambaye apoawali alifanya vizuri akiwa ndani ya kundi la 'Bm Love' nakuvuma na wimbo ulioitwa 'Anakundanganya, Anakudanganya huyo' baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu , ameanza hatua nyingine katika muziki kwa kupakua nyimbo mpya. Akizungumza na Jatida la Maisha hivi karibuni , Alex amesema kuwa kwa sasa ameanzisha kundi jingine ambalo tayari linaundwa na wasanii watatu . "Tunakuja na ujio wa albamu yakundi itakayokuwa na nyimbo takribani kumi,"alisema msanii huyo. Alex amewataja wasanii wengine kuwa ni Leah Mud aliye ibiliwa kipaji chake kwenye Bongostar Seach pamoja na Siz - Q ambapo nyimbo tatu tayari zimeishaanzakusambazwa kwenye stesheni mbalimbali za Redio hapa nchini. Aidha msanii huyo alizitaja nyimbo hizo kuwa ni wimbo wa 'Penzi langu' ulioimbwa na Reah Mud , 'Zumu zumu Zumu' ulioimbwa na Siz - Q na wimbo uitwao 'Mshikaji' ukiwa umeibwa na Masiga. Masiga ambaye kwa s

A M ANAKUJA KWA MWENDO WA KASI

MSANII wa muziki wa Bongofleva Maurid Pepe 'AM' ameanza hatua ya kukamilisha albamu kwa ajili ya ujio mpya , ambapo tayari amekamilisha nyimbo takribani nne zenye majina ya 'Longo Longo' 'Sina noma' , 'Sema' , pamoja na mwingine uitwao 'Usiondoke'. Akizungumza na Jarida la Maisha sikuchache zilizopita msanii Pepe alisema kuwa uono mwanzo wa matayalisho kwa ajili ya ujio wa alibamu yao mapema mwakani. "Haya ni mafanikio yanayoonesha kuleta njia ya kuyafikia mafanikio mapya kwa siku za usoni;"alesema Pepe. Msanii huyo ambaye amemtaja msanii mwingine aitwaye Hassan Omari kuwa ni mmoja ya msanii muhimu kwake kwani atashiriki nyimbo nyingi studio na tayari ameisha shirikiana naye kwenye vyimbo hizo za awali, zilizo rekodiwa katika studio za Imotion Records , OM Studio na G-2 chini ya produza Roi. Pichani kama tulivyo mkuta akienda kumjulia hali babake katka Hospitali ya Mwananyamala.

Huyu ni Yule aliyewai Kuimba wimbo Anakudanganya , Anakudanganya huyo.

Jamaa huyo anaitwa Masiga Alex, aliwai kuimba wimbo huo akiwa kundi moja na Banana Ally Zolo kwa sasa ni mtu mwenye elimu bora ya Juu yani alimaliza Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam , baada ya pilika pilika zote . Jamaa ni muajiliwa wa Kampuni ya simu ya Mkonono (Tigo) anachapa mwendo na maisha kiulaini tu sasa . Pichani amefanya maongezi na Blog hii leo saa nane mchana kesho tuta yaweka hewani maelezo yake. Picha hiyo anaonekana akiwajibika leo katika ofisi hizo za (Togo).

Jese Mtambo na Chid Mlitoa shoo Bab Kubwa 'Gang Star' Alimkumbatia Chid alikubali.

BUSTA kweli sana tu, ulikamua kinoma ulikuwa ni wakati mpya wa usiku wa jumamosi , umetuacha , sijui tu , kulikuwa na mengi ya kuchukua kubolesha namna ya kudili na jukwaa . Sasa ni fundisho Jose Mtambo toka kigamboni uliwakilisha vema michano ya Hip Hop wana Hip Hop wengi uliwagusa wewe na mchizi wa Ilala babake mlitisha shoo zenu jukwaani , mliibeba shoo yaani katika Hip Hop pia ni ngumu sana kuwasahau du.

HILIKUWA BALAA SASA IMEBAKI STORY TU JIJINI

Bado cheche alizo ziacha jijini Dar es Salaam msanii nguli wa Marekani Busta Rhymes zinasimuliwa na mashabiki wengi kwenye mitaa. Dangerous, Get high tonight, Woo Hah got you all in check, Make it clap, I know what You want hivi ni kati ya vibao vilivyo simama vili leta soo mashabiki lukuki walinyooshamikono juuuuu .... kwamuda mwingi wa onesho la jamaa, jamaa alifanya kazi ya kiutu uzima jukwaani. Nguli wengine tunao wafahamu wa Kibongo nao waliwakilisha vema, Marlow, Hussein Machozi, Ali Kiba, Chege, Black Rhino, Langa, Chid Benz, Prof J na Hard Blasters, Daz Nundaz, Wateule, Juma Nature, Joe Makini, Fid Q, Mangwea pia walinga'ra katika tamasha hilo kwa sababu walijitahidi kujituma, kutawala jukwaa, kuimba kwa kutoa sauti, kucheza jukwaani na kuimba nyimbo zenye tungo za kuvutia. The event was jointly spointly sponsored by Serengeti Brewerie and Zain, Kusaga is confident that local artists , who play a mojar part in the Fiesta , benefit a lot from the event. Apart from conti

Hilikuwa ya Kweli 4 th TAXPAYERS' DAY CELEBRATIONS-2009, INSHU ILIFANYIKA UBUNGO PLAZA

Hapa ilikuwa ni Inshu yaTanzania Revenue Authority (TRA), leo ambapo wamelezo mengi na kugawa zawadi kwa baadhi ya watu mbali mbali ususani mwenye makampuni yanayo lipa vilivyo . 4 th Taxpayers' Day Celebrations - 2009.

Hii ni Mjomba Band Babake

Wakijadili Inshu Wakati Huo Ubungo Plaza

Wakwanza kushoto ni msanii ambaye kipaji chake kimeibuliwa na Bongo Star Seach , msanii huyo Merry Rukosi pichani akiteta jambo na wasanii wenzake waliomo ndani ya bendi hiyo ya Mjomba Band

Bendi Mpya ya Msanii wa Mashahiri Mrisho Mpoto Akitumbuiza

Mshike mshike huo bwana ilikuwa ni leo mchana kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza Dar es Salaa , wakwanza kushoto ni Nuruel Mbowe ambaye pia licha ya kuwemo ndani ya bendi hiyo ua pia ni bonge la kifaa kwenye Bendi nyingine iitwayo B Band inayomilikiwa na Banana Ally Zolo.

Inshu Zote Hizi ni Leo

Hii Ni Leo Kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza

MWIMBAJI WA KUNDLA TAARAB LA JAHAZ MWANAHAWA ALI

WAKAZI wa mkoani morogoro wanatarajia kushuhudia uzindizi wa alabamu mpya ya muziki wa Taarab Novemba27, pale kundi la Jahazi Modern Taarab litakapo poromosha vibao vyake vipya vilivyo ndani ya albamu yao mpya iitwayoDaktari wa Mapenzi. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana msemaji waUzinduzi huo Said Mdoe alisema kuwa hadi sasa maandalizi yashoo ya burudani hiyo yanaenda vizuri . "Tunatazamia wakazi wa mji kasoro bahari watafika kwa wingikushuhudia uzinduzi huo kwani bado tunafikilia mambo mengine yatakayo boresha mafanikio katika burudani hiyo,"alisema Mdoe. Alisema bendi hiyo inataraji kutumbuiza nyimbo zake mpya kama Daktari wa Mapenzi iliyoibwa na Mzee Yusufu inayobeba jina la albamu nyingine ni Roho mbaya haijengi iliyoimbwa na Mwana hawa Ali , Domokaya ulioimbwa na Abubakar Amigo , Chokochoko mchokoe pweza ulioimbwa na Mariam Amour. Nyimbo nyingine ni Fungu la Mungu Silikosi ulioimbwa na Leila Rashid pampja nawimbo uitwao Ng;ombe wa Masikini Hazai ulioimbwa na Fat