Skip to main content

Diamond na mchumba wake Zari wazua gumzo Airport…


diamond na zari
BAADA ya kula bata za kutosha Bongo, wakati wakisindikizana kimahaba, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, wamezua gumzo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar, Ijumaa lina mchapo kamili.
Mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady (mwenye gauni jekundu) akishuka kutoka gari la ‘Diamond Platnumz’.
HABARI KAMILI
Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri mishale ya mchana, Jumanne iliyopita katika maegesho ya airport (uwanja wa ndege) ambapo Diamond alikuwa akimsindikiza Zari aliyekuwa akitimua Bongo baada ya kufanya yao kwa siku kadhaa.
KABLA YA TUKIO
Awali kabla ya tukio hilo, gazeti hili lilipokea ‘ubuyu’ kutoka kwa chanzo chake cha kuaminika kwamba, wawili hao walikuwa wakijiandaa katika hoteli waliyokuwa kwa siku kadhaa iliyopo kwenye Ufukwe wa Bahari ya Hindi, tayari kuelekea uwanja wa ndege.
Zari au The Boss Lady akimwelekeza kitu mpambe wa ‘Diomond’.
“Ijumaa acheni kulaza damu, kwa taarifa yenu Diamond ndiyo anajiandaa kumpeleka Zari airport wahini pale mpate tukio kamili ili kumaliza ubishi kuwa kweli walikuwa wote Bongo,” kilisema chanzo hicho kikiomba hifadhi ya jina gazetini.
IJUMAA MZIGONI
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu walitia gia kwenye ‘motokaa’ ambapo dakika kadhaa baadaye walikuwa wametega satelaiti zao uwanjani hapo tayari kwa kunasa tukio.
Gari jeusi aina ya BMW X6 ya mkali ‘Diamond’ ikiendeshwa na mpambe wake aliyejulikana kwa jina la Q-Boy huku mwenyewe (Diamond) siti ya nyuma.
BMW X6 LATOKEA
Wakati wanahabari wetu wakiwa wanakaribia kukata tamaa, ghafla lilitokea gari jeusi aina ya BMW X6 ambalo tofauti na magari mengine, badala ya namba za usajili, lenyewe lilikuwa na maandishi yaliyosomeka kwa herufi kubwa ‘PLATNUMZ’ kisha likapaki kwenye eneo la maegesho uwanjani hapo.
Gari hilo lilikuwa likiendeshwa na kijana mmoja wa Diamond aliyejulikana kwa jina la Q-Boy na pembeni mwake kwenye siti ya abiria alikuwepo mpambe mwingine wa msanii huyo ambaye jina halikupatikana.
DIAMOND AJIFUNGIA
Wakiwa siti ya nyuma, wakati Zari anashuka, Diamond alijifungia kwenye gari ili kuwakwepa mapaparazi baada ya kuwashtukia kuwa walikuwa wakimsubiri
WAZUA GUMZO
Wawili hao walizua gumzo uwanjani hapo ambapo baadhi ya watu wakiwemo Wazungu walikuwa wakiwashangaa huku Wabongo wakitamani Diamond atoke kwenye gari amtambulishe Zari kama ndiye mrithi wa Wema au la!
“Huyu Diamond naye balaa. Kampata wapi mtoto mrembo kiasi hiki? Hakyanani na mimi bora niwe msanii nitafaidi. Mtoto kaumbika hasa,” alisikika mmoja wa madereva teksi huku wenzake wakimkatisha tamaa kuwa hawezi kuwa msanii. Zari alishuka na yule mpambe wa Diamond na kuambatana hadi sehemu ya kukaguliwa ili akapande ndege.
IJUMAA LAMBANA ZARI
Kabla ya kufikia sehemu hiyo, wanahabari wetu walibahatika kumfotoa picha za kutosha Zari kisha kumfuata na kumuuliza alikuwa na ishu gani na Diamond ambaye alikuwa naye hotelini Bongo kwa takriban siku tano.
Hata hivyo, Zari alishindwa kujibu na kuishia kusema kuwa hana maoni.“No comment,” alisema Zari na hata alipoombwa kufafanuzi kidogo aligoma.
DIAMOND AFUNGUKA
Baada ya tukio hilo, wanahabari wetu walimtafuta Diamond kwa njia ya simu ili azungumzie kwa kina juu ya uwepo wa Zari Bongo na tuhuma za kujihusisha naye kwenye mapenzi ambapo Diamond alifunguka:
“Niliwaona airport mkimpiga picha na gari langu na mkaongea naye.
“Kweli ninyi ni noma sana, lakini nadhani mliandika hivi karibuni kuwa mimi nimeachwa na Wema (Sepetu).
“Ukweli hakuna mwanaume anayeweza kujitoa kwa demu wake hasa kumpatia zawadi ya gari kama niliyotoa kwenye bethidei ya Wema halafu baadaye usikie kuna mwanaume mwingine katoa zaidi na ukaendelea kufurahia.
ZARI NI RAFIKI TU JAMANI!
“Sitaki kuongea mengi ila Zari naomba atambulike kama rafiki yangu tu jamani.”
YATOKANAYO
Hivi karibuni Diamond alimwagana na Wema ambapo siku chache baadaye habari zilivuja kwamba Zari ambaye ni msanii wa kike tajiri Afrika Mashariki ndiye mwenye uwezo wa kuziba pengo hilo mara tu baada kuonekana na jamaa huyo

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.