Skip to main content

Serikali yalizishwa na mradi sekta za kilimo na mifugo

SERIKALI imeridhishwa na mradi wa mapinduzi katika sekta za kilimo na mifugo baada ya mradi huo unaotekelezwa katika halmashauri nne za Mkoa wa Mwanza kuonyesha mafanikio na tija kwa wakulima na wafugaji.

Akizungumza katika mahojiano na waandishi wa habari wilayani Misungwi hivi karibuni Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais(TAMISEMI) John Cheyo alisema baada ya kukutana na wakulima walikiri kuwa mradi huo una tija.

“Tulipokutana na wakulima maeneo mbalimbali ya mradi walikiri una tija na hivyo tukiuhamisha na kuupeleka katika mikoa mingine kunaweza kuwa mabadiliko makubwa zaidi kwenye kilimo. Ili kuongeza uzalishaji wakulima wanatakiwa kusaidiwa utaalamu na ushauri wa kupanda mbegu kwa nafasi na matumizi bora ya pembejeo,” alisema Cheyo.

Alifafanua kuwa mradi huo unafanya kazi kwa kushirikiana na serikali ya Mkoa wa Mwanza kwenye maeneo manne kujaribu zao la alizeti huko Buchosa na Sengerema ambako lilikuwa halijaanza ili wawasaidie wakulima walime kibiashara na kuongeza kipato, pia  Dalberg inajaribu kuongeza nguvu kwenye zao la pamba liwe na tija zaidi.

Mradi huo pia unawajengea uwezo maofisa ugani na mifugo kwa kuwapa kompyuta, vifaa vya kazi na  usafiri ili kufuatilia na kukusanya taarifa, kutunza takwimu na kumbukumbu kwa kutumia kompyuta.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mradi Dalberg Tanzania Steve Kisakye alisema kuwa mwaka 2016 serikali kupitia sekta ya kilimo na mifugo ilianza kufanya kazi na Dalberg 3D ikijikita kwa kutoa mafunzo na ufadhili wenye tija kwenye kilimo na ufugaji katika kuongeza uwezo kwenye sekta hiyo.

Alisema mradi huo unaotekelezwa katika halmashauri za Misungwi, Kwimba,Sengerema na Buchosa mkoani Mwanza unalenga kuibua mbinu mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za kilimo na ufugaji kwa kuzingatia vipaumbele vya kila halmashauri.

Kisakye alieleza kuwa mradi wa Dalberg 3D wa kuleta  mapinduzi katika sekta ya kilimo uliombwa na kubuniwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) ili kuangalia mabadiliko yanayotakiwa licha ya wengi kuchangia hakukuwa na mchango wa kuisadia serikali iendele mbele na kuleta mabadiliko kwa wakulima na wafugaji.

“Serikali inafanya kazi kubwa ya kuwasaidia maofisa ugani kwa kuwajengea uwezo na kuwawezesha wakulima kupanga mikakati mipya ila hakukuwa na mchango wa kuisaidia serikali kuleta mabadiliko chanya ili iweze kwenda mbele.Hivyo mtizamo wa serikali ni kwamba hakukuwa na usaidizi wa kuisadia taaluma ya masuala ya ugani,”alisema Kisakye.

Aliongeza kazi kubwa ya mradi wa Dalberg 3D ni kuwajengea uwezo na kuwapa taaluma mpya, kupanga mipango kabambe na mikakati mipya katika kuendeleza tija kwenye kilimo na ufugaji,ukusanyaji wa taarifa na kuzichambua ili zifanyiwe kazi.

Wakizungumza kwa nyakati maofisa kilimo na ugani wa halmashauri za Misungwi, Sengerema na Kwimba walisema yapo mabadiliko makubwa kwa wakulima baada ya kupata elimu na matumizi bora ya pembejeo.

 “Mradi huu umebadili mitizamo ya watumishi wa umma katika sekta hizi (kilimo na mifugo) kwa kila mmoja kujua wajibu wa kufanya kazi si lazima afundishwe,”alisema Afisa Kilimo Kwimba Alfred Mabuga.

Naye Afisa Kilimo Wilaya ya Misungwi Kwilasa Mahigu alisema “ Matarajio ni kuongeza tija ili ekari moja ya pamba iliyokuwa ikizalisha kilo 250 hadi 300 izalishe kilo 700 hadi 850. Hivyo ufanisi umepatikana baada ya Dalberg kuwasaidia maofisa wetu kufikisha mbegu bora na kwa wakati katika kata na vijiji, kufuatilia na kutoa mbinu bora kwa wakulima.” 

Aidha,  mmoja wa wakulima wa wilayani Sengerema Ndaki Butulya kwa niaba ya wenzake alisema mashamba yao walikuwa hawayatunzi kitaalamu lakini baada ya kupata elimu na kuanza kutumia mbolea ya kupandia na kukuzia mazao baada ya palizi sasa wanapata mavuno mengi.
1.Shamba%2Bdarasa%2Bla%2Bpamba
 Baadhi ya wakulima wilayani Sengerema wakiwa katika moja ya shamba darasa la zao la pamba walilolianzisha baada ya kupata elimu kwa ufadhili wa mradi wa Dalberg 3D.
3%2BDalberg%2BMisungwi
 Afisa Mfugo Wilaya ya Misungwi  Dk. Chrispine Shami (mbele), Mratibu wa Dalberg wilayani humo Ines Muganyizi wakimuongoza  Mkurugenzi wa Uratibu (TAMISEMI)Dk. Andrew Komba (wa tatu nyuma)kukagua mashamba ya mfano ya  utekelezaji wa mradi wa Dalberg  3D wilayani humo.
7.Mfugaji%2Bakiswaga%2Bng%2527ombe%2B%2Bkuwaigiza%2Bndani%2Bya%2Bjosho
 Mfugaji  wilayani Misungwi ambaye jina lake halikupatikana mara akiswaga ng’ombe wake kuingia ndani ya josho kwa ajili ya kuwaogesha dawa ya kuua wadudu. Josho hilo ni moja kati ya majosho yaliyofufuliwa kwa ufadhili wa mradi wa Dalberg 3D unaotekelezwa katika halmashauri nane za Mkoa wa Mwanza ambapo wameanza kuzingatia elimu ya ufugaji wanayopewa na wataalamu wa mifugo kupitia mradi huo. 
8.%2BShamba%2Bdarasa%2Bla%2Bpamba
 Mkurugenzi wa mradi wa Dalberg Tanzania Steve Kisakye (kushoto) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais(TAMISEMI) John Cheyo (katikati)kabla ya kukabidhi pikipiki za usafiri kwa maofisa ugani na mifugo katika Wilaya ya Sengerema.Kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Alfred Kipole.
IMG_9699%2BVyombo%2Bvya%2Busafiri
 Mkurugenzi wa Dalberg Steve Kisakye (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Rais (TAMISEMI) John Cheyo pikipiki kwa ajili ya usafiri wa maofisa Kilimo (ugani) na Mifugo katika Wilaya ya Sengerema  ili ziwarahisishie usafiri wa kwenda vijijini kutoa elimu kwa wakulima na wafugaji pamoja na kukusanya taarifa.
IMG_9738%2BPokea%2Bpikipiki%2Bya%2B%2Busafiri
Mkurugenzi wa Uratibu (TAMISEMI) Dk. Andrew Komba (mwenye shati la drafti) akimsikiliza ofisa Ugani wa Kata ya Mondo katika wilaya ya Misungwi John Choto baada ya kukagua shamba la pamba la mkulima Muhoja Ngole (kushoto). Mkulima huyo amelima na kulitunza shamba hilo kwa kuzingatia ushauri wa watalaamu chini ya ufadhili wa Mradi wa Dalberg.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...