Skip to main content

Shirika la Posta nchini lawataka wafanyabiashara nchini kutangaza bidhaa zao kiteknolojia

WAFANYABIASHARA wa Kilimo nchini wametakiwa Shirika la Posta nchiniya Shirika la Posta nchini katika kutangaza bidhaa zao pamoja 
na kuuza.
Image result for Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye
Hayo yamesemwa na  Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi 
Atashasta Nditiye  alipofungua mkutano wa 16 wa 
Mashirika ya Posta yaliyopo Nchi zilizo kusini mwa Afrika (SADEC), huku 
akisisitiza kwa kufanya hivyo wafanyabiashara hao wataweza kuuza bidhaa 
zao Dunia nzima.

''Unajua Shirika la Posta sasa hivi, linajulikana Dunia nzima, hivyo 
wafanyabiashara kama watatumia website hii watapata fulsa ya kuonekana
 dunia nzima, hali itakayopelekea kupata masoko makubwa ya Kimataifa'', alisema.


Alisema alisema kuwa, Shirika la Posta hivi sasa limehimarika linajiaendesha 
kwa faida, hivyo lina uwezo wa kusafirisha vifurushi popote Duniani  na mzigo 
wako ukafika salama na pesa yako ukaipata bila matatizo.

 Naibu huyo amezitaka taasisi zote za Serikali kulitumia Shirika hilo, katika
 kusafirisha vifurushi ili kuliongezea uwezo liweze kuendelea kujiendesha kwa
 faida ili liweze kutoa gawiwo kwa Serikali kila mwaka.

Nditiye aliongeza kuwa, wanatarajia kurekebisha baadhi ya sheria zilizokuwa 
zikionekana kuwabana wateja, ili kwenda na wakati kwani mambo ya teknolojia
 yamekuwa kwa kasi.

Aidha  alisema kuwa, katika kuboresha huduma zao, Shirika la Posta 
limeanzisha huduma ya Posta mlangoni ambayo tayari imeshaanza katika Mikoa 
ya Dar es Salaam, Arusha  na Dodoma.

Pia alisema shirika la Posta Tanzania tangu lizinduwe  huduma 
mpya POSTA MLANGONI limeendelea kuimalisha huduma hiyo katika jiji 
la Dar es Salaam ambapo kila mwananchi atapelekewa kufurushi, 
taarifa au bidhaa zilizotumwa kwa kupitia Ofisi za Posta kwa sasa
wameshatoa taarifa kwa madiwani,wawasiliane na watendaji wa Serikali
za mitaa,ili wapeleke majina ya mitaa yao Makao Makuu ya Posta,ili 
zoezi hilo likamilike wananchi waweze kupelekewa barua au vifurushi
vyao mpaka mlangoni mwao.

''Lengo la Posta Mlangoni ni kuenea Tanzania nzima, isipokuwa kwa sasa 
tumeanza na hii Mikoa mitatu, hivyo wananachi wasubiri wapatatiwa huduma 
hiyo kwa kufuatwa majumbani mwao'', alisema.

Mkutano huo wa 16, una lengo la kujadili mambo mbali mbali yahusuyo Posta, 
pamoja na kujadilianani jinsi gani wataweza kuimarisha huduma zao ili ziweze 
kufanyika kwa ufanisi mkubwa.



Naye mwenyekiti wa bodi  ya Wakurugenzi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), 
Luteni Kanali mstaafu, Dk. Haroun Kondo alisema kuwa mkutano huo kufanyika
hapa nchini unaweza  kutafuta pia fursa za kuboresha huduma kama mambo ya 
kiteknolojia.


Comments