Skip to main content

Mwadini, Kapombe ndani, Boko, Kado njeMonday, 31 October 2011 18:43 0diggsdigg [kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen] kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen Sosthnes Nyoni KOCHA wa timu ya taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen jana ametangaza rasmi kikosi chake akimuita kwa mara ya kwanza kipa, Mwadini Ally ikiwa uthibitisho sahihi wa mwitikio wa kelele za wadau wa soka nchini waliokuwa wakimpigia debe ajumuishwe. Kipa Ally, anaungana na chipukizi Shomari Kapombe katika orodha ya wachezaji wapya walioitwa na Poulsen tayari kwa mechi dhidi ya Chad. Poulsen alikuwa kwenye wakati mgumu mwanzoni mwa mwezi uliopita alipoamua kuwateua makipa Shabaan Dihile na Shabaan Kado kwenye kikosi chake wakiwa hawana namba katika klabu zao na kumwacha Mwadini ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwa timu yake Azam msimu huu. Pia, Stars itaendelea kumkosa nahodha wake Shadrack Nsajigwa anayesumbuliwa na majeruhi yaliyomweka nje ya uwanja kwa zaidi ya wiki tatu sasa. Kikosi cha Stars itaingia kambini rasmi Novemba 3 kujiandaa na mechi ya mchujo ya kuwania kushiriki fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Chad itayofanyika Novemba 11 jijini N'Djamena. Poulsen aliwarejesha kundini beki wa kulia wa Yanga, Godfrey Taifa pamoja na mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu. Kurejea kwa Ulimwengu katika kikosi hicho kumemfanya Mdenmark huyo kumtupia virago kinara wa ufungaji wa Ligi Kuu Tanzania mshambuliaji John Boko. Mshambuliaji huyo wa Azam ameshafunga mabao saba hadi sasa, lakini kiwango kiduni alichoonyesha kwenye mchezo wa kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika 2012 dhidi ya Morocco umesababisha kuachwa. Mbali ya Boko wengi walioachwa kwenye kikosi cha wachezaji 22 ni beki wa Simba, Victor Costa, makipa Shaaban Kado wa Yanga na Shaaban Dihile wa JKT Ruvu, kiungo Jabir Aziz wa Azam. Poulsen aliitaja sababu ya kuwaacha Nsajigwa na Costa kuwa ni kutokana na wachezaji hao kutokuwa timamu kiafya huku akisema nyota wengine amewaaacha kutokana kuporomoka viwango, ufinyu wa nafasi na wengine kukosa nafasi a kucheza kwenye timu zao. "Nimemwacha Nsajigwa na Costa kwa sababu bado hawako fiti kwa asilimia mia, lakini pia kuna suala la kuporomoka, ufinyu wa nafasi na wengine hawapati nafasi kwenye timu zao, kwa mfano Shaaban Kado ni kipa mzuri tu lakini muda mrefu hachezi,"alisema Poulsen. Akizungumzia pambano hilo,Poulsen alisema kuwa litagumu gumu kwa vile wanacheza na timu wasiyoijua na ambayo nayo inatafuta nafasi. Kikosi cha Taifa Stars ni pamoja makipa Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya), Erasto Nyoni (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Godfrey Taita (Yanga) na Juma Jabu (Simba). Viungo:Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Ramadhan Chombo (Azam) na Shomari Kapombe (Simba). Washambuliaji:Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam), Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu(TP Mazembe, DR Congo), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), na Hussein Javu (Mtibwa Sugar). Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Boniface Wambura kikosi cha Stars kinatarajia kuondoka nchini Novemba 9 kuelekea Chad kikiwa na msafara wa watu 35 na kurejea nchini Novemba 12 siku moja baada ya mchezo.

Monday, 31 October 2011 18:43

kocha wa timu ya Taifa,Jan Poulsen
Sosthnes Nyoni
KOCHA wa timu ya taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen jana ametangaza rasmi kikosi chake akimuita kwa mara ya kwanza kipa, Mwadini Ally ikiwa uthibitisho sahihi wa mwitikio wa kelele za wadau wa soka nchini waliokuwa wakimpigia debe ajumuishwe.

Kipa Ally, anaungana na chipukizi Shomari Kapombe katika orodha ya wachezaji wapya walioitwa na Poulsen tayari kwa mechi dhidi ya Chad.

Poulsen alikuwa kwenye wakati mgumu mwanzoni mwa mwezi uliopita alipoamua kuwateua makipa Shabaan Dihile na Shabaan Kado kwenye kikosi chake wakiwa hawana namba katika klabu zao na kumwacha Mwadini ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwa timu yake Azam msimu huu.

Pia, Stars itaendelea kumkosa nahodha wake Shadrack Nsajigwa anayesumbuliwa na majeruhi yaliyomweka nje ya uwanja kwa zaidi ya wiki tatu sasa.

Kikosi cha Stars itaingia kambini rasmi Novemba 3 kujiandaa na mechi ya mchujo ya kuwania kushiriki fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Chad itayofanyika Novemba 11 jijini N'Djamena.

Poulsen aliwarejesha kundini beki wa kulia wa Yanga, Godfrey Taifa pamoja na mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu.

Kurejea kwa Ulimwengu katika kikosi hicho kumemfanya Mdenmark huyo kumtupia virago kinara wa ufungaji wa Ligi Kuu Tanzania mshambuliaji John Boko.

Mshambuliaji huyo wa Azam ameshafunga mabao saba hadi sasa, lakini kiwango kiduni alichoonyesha kwenye mchezo wa kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika 2012 dhidi ya Morocco umesababisha kuachwa.

Mbali ya Boko wengi walioachwa kwenye kikosi cha wachezaji 22 ni beki wa Simba, Victor Costa, makipa Shaaban Kado wa Yanga na Shaaban Dihile wa JKT Ruvu, kiungo Jabir Aziz wa Azam.

Poulsen aliitaja sababu ya kuwaacha Nsajigwa na Costa kuwa ni kutokana na wachezaji hao kutokuwa timamu kiafya huku akisema nyota wengine amewaaacha kutokana kuporomoka viwango, ufinyu wa nafasi na wengine kukosa nafasi a kucheza kwenye timu zao.

"Nimemwacha Nsajigwa na Costa kwa sababu bado hawako fiti kwa asilimia mia, lakini pia kuna suala la kuporomoka, ufinyu wa nafasi na wengine hawapati nafasi kwenye timu zao, kwa mfano Shaaban Kado ni kipa mzuri tu lakini muda mrefu hachezi,"alisema Poulsen.

Akizungumzia pambano hilo,Poulsen alisema kuwa litagumu gumu kwa vile wanacheza na timu wasiyoijua na ambayo nayo inatafuta nafasi.

Kikosi cha Taifa Stars ni pamoja makipa Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ally (Azam).

Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Juma Nyoso (Simba), Idrissa Rajab (Sofapaka, Kenya), Erasto Nyoni (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Godfrey Taita (Yanga) na Juma Jabu (Simba).

Viungo:Henry Joseph (Kongsvinger IL, Norway), Nurdin Bakari (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Abdi Kassim (DT Long An, Vietnam), Ramadhan Chombo (Azam) na Shomari Kapombe (Simba).

Washambuliaji:Nizar Khalfan (Vancouver Whitecaps, Canada), Mrisho Ngassa (Azam), Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu(TP Mazembe, DR Congo), Dan Mrwanda (DT Long An, Vietnam), Athuman Machupa (Vasalund IF, Sweden), na Hussein Javu (Mtibwa Sugar).

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Boniface Wambura kikosi cha Stars kinatarajia kuondoka nchini Novemba 9 kuelekea Chad kikiwa na msafara wa watu 35 na kurejea nchini Novemba 12 siku moja baada ya mchezo.Chanzo ni www.mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.