Skip to main content

Sitta: Niliwahi kukataa rushwa ya Sh140 milioni

Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta
Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema anasimama kifua mbele kupambana na rushwa kwa kuwa aliwahi kuikataa rushwa ya Dola 70,000 (sawa na Sh140,000) milioni).
Sitta alisema hayo jana wakati akizungumza na makada wa chama hicho waliojitokeza kumdhamini katika wilaya ya Geita mkoani Geita na kusema kuna baadhi ya watia nia wanaopita wakisema kuwa wakiwa marais watapambana na rushwa wakati ukiwatazama macho yao yanaonyesha ni wala rushwa. Viwango vya kubadili fedha za kigeni, kwa sasa Dola moja ya Marekani sawa na Sh2,000.
“Nilitumwa Canada kutafuta ndege tatu, jioni moja tukiwa Canada tunajiandaa kuondoka, akaja mkurugenzi wa masoko wa kampuni tuliyonunua ndege, akaniambia waziri tuna kautaratibu hapa ukifanikisha ndege zetu zikanunuliwa tunatoa bakshishi ya Dola 70,000 utataka hizi hela tuzipeleke benki gani,” alisema Sitta akimnukuu ofisa huyo wa masoko.
“Watazameni hawa watu... mtu kawa waziri mwaka mmoja leo anataka urais, halafu anasema atapambana na rushwa...utapambana na rushwa wapi wakati hata hujapita kwenye mitego ya rushwa. Watazameni kwa makini, mtawajua tu kwa macho, kwani macho yao yamekaa kijanjajanja kweli,” alisema. Aliendelea, “Kwa kuwa mimi nililelewa vizuri nilijua tu huo ni mtego wa shetani, nikamwambia mkurugenzi nitampa jibu kesho, nikawasiliana na wakubwa zangu kwanza wakakubali ni chukue hiyo pesa ikasomeshe marubani wa ndege.”
Sitta aliwataka wananchi hao kuwatazama kwa makini watangaza nia hao, na kuwauliza iwapo tayari walishawahi kupambanishwa na rushwa.
Lowassa aonya kuhusu viongozi wanafiki
Kigoma. Wakazi wa Kigoma wametakiwa kuwa makini na kauli za baadhi ya viongozi wa Serikali wanaojinadi kwa kusema wanawapenda Watanzania maskini, lakini mioyoni mwao hawana huruma.
Hayo yalisemwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa alipokuwa akitafuta wadhamini
mkoani hapa, muda mfupi baada ya kukabidhiwa fomu zenye majina ya wanachama waliojitokeza kumdhamini.
Akiwa katika ofisi ya CCM mkoa, Katibu wa CCM Wilaya ya Kigoma Mjini, Nohoji Kubaji alimkabidhi Lowassa fomu 45 za wana CCM waliomdhamini.
“Wapo viongozi, wanajifanya wanawapenda na kuwajali watu masikini, lakini wao wenyewe unawakuta ni matajiri, hawa jamaa ni waongo sana hawa,” alisema.
Lowassa aliwataka wakazi Kigoma kumuombea ili dua na sala zao ziweze kumsaidia afikie malengo aliyojiwekea. “Nina dhamira ya kuwatumikia, lakini lazima mniombee sana dua na sala ili mambo yangu yaende vizuri hatimaye nishinde kuwa Rais wa Tanzania. Mimi nachukia sana umaskini, kwa hiyo lazima tuwe kama Malaysia ambayo kiongozi wake alipambana kuhakikisha wananchi wanaondokana na umaskini,” alisema.
Wasira awashangaa wanaotumia matarumbeta
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira amesema anashangazwa na baadhi ya wagombea wenzake, wanaokwenda kutafuta wadhamini kwa matarumbeta na miziki ya kuwaita wananchi.
Wasira alitoa kauli hiyo mjini Musoma katika Ofisi ya CCM Mkoa, Adamu Ngalawa wakati alipokuwa akipokea majina na kadi za wadhamini waliojitokeza kumdhamini.
Alisema wagombea wanaofanya hivyo wanakiuka taratibu, kanuni, sheria na katiba za chama kwa kuwa chama hicho tawala kilishapitisha kuwa wakati wa kutafuta wadhamini hakuna mgomWbea kuhutubia mkutano wa hadhara.
“Kuna wagombea wanaitisha mkutano wa hadhara na kuwaita wananchi wakati hawana cha kuwahutubia kwa kuwa wamezuiliwa kufanya hivyo...wanabaki wakiwaeleza wananchi mniombee, wawaombee nini? Mimi nimeshatembea mikoa zaidi ya 20 na hakuna sehemu nimewaita wananchi tofauti na kutoa taarifa kwenye chama ili wadhamini niwapate,” alisema.
Wasira alisema mkoa wa Mara una wagombea wanne wanaowania urais, lakini hakuna atakayejitoa kwa misingi ya kuachiana kura kwa sababu hakuna mwananchi wa kawaida atakayepiga kura bali maamuzi yatafanywa na Kamati Kuu ya CCM. 
Chanzo:Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.