Skip to main content

WIZARA YA MAJI KUJENGA MTAMBO WA MAJITAKA UTAKAOGHARIMU BILIONI 200



madini
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge akitoa hotuba ya uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa kutathmini maendeleo ya sekta ya maji uliowashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi. Mkutano huo umefanyika leo katika ukumbi wa arnautoglo uliopo maeneo ya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam.
madini-1
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa maendeleo wa sekta ya maji walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa kutathmini maendeleo ya sekta hiyo uliofanyika leo katika ukumbi wa arnautoglo uliopo maeneo ya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Wizara ya Maji na Umwagiliaji imejipanga kuanza ujenzi wa mtambo mkubwa wa majitaka katika maeneo ya Ilala Jijini Dar es Salaam ili kuzuia uchafuzi wa mazingira nchini.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge alipokuwa akizindua Mkutano Mkuu wa kutathmini maendeleo ya sekta ya maji unaolenga kutatua changamoto zinazozuia upatikanaji wa maji salama na uondoshaji wa majitaka nchini.
Mhandisi Lwenge amesema kuwa fedha za mradi huo zimetoka Serikali ya Korea Kusini ambapo kwa sasa wizara hiyo ipo katika mchakato wa kumtafuta Mhandisi mshauri ambaye atafanya mapitio sanifu ya manunuzi ya vifaa na baada ya hapo juhudi za kumtafuta mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mitambo hiyo zitaendelea.
“Mtambo huo utajengwa katika wilaya ya Ilala na mabomba yake kutandazwa katika maeneo yaliyopo katikati ya jiji, Magomeni pamoja na Kurasini ili kuhakikisha maji machafu yanapata sehemu ya kuelekea na kuacha jiji likiwa safi siku zote,” alisema Mhandisi Lwenge.
Mhandisi Lwenge aliongeza kuwa baada ya mtambo huo kukamilika maji yatakayopatikana yatasafishwa na kutumika kwa matumizi mengine yakiwemo ya nyumbani, ufugaji, kilimo cha umwagiliaji au kupelekwa moja kwa moja katika bahari ya Hindi.
Naye Mwakilishi kutoka Asasi za Kiaraia, Josephine Lemoyan amesema kuwa uchafuzi wa mazingira unachangiwa na kutokuwa na miundombinu mizuri ya kupitisha maji machafu hivyo mkutano huo uliofunguliwa leo utajadili mambo mbalimbali ikiwemo njia za  uondoshaji wa majitaka ambayo kwa kiasi kikubwa unaathiri mazingira yanayotuzunguka.
“Katika kila sekta mapungufu huwa hayakosekani hivyo kwa kupitia mikutano ya wadau kama hii inatusaidia kupata mawazo ya kutatua baadhi ya changamoto zinazozuia uendelevu wa miradi mbalimbali ya majisafi na majitaka,”alisema Bi. Josephine.
Bi. Josephine amefafanua kuwa hadi kufikia mwezi Juni 2016 Tanzania imejitahidi kuondoa majitaka kwa asilimia 52.6 na ifikapo mwaka 2020 Tanzania inategemewa kufikia asilimia 75 katika suala zima la uondoaji wa majitaka.
Mkutano huo wa siku mbili ambao umewashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi unafanyika katika ukumbi wa arnautoglo uliopo maeneo ya Mnazi Mmoja, Jijini Dar es Salaam.(P.T)

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...