Skip to main content

Minziro kutibua sherehe Yanga leo?

Fred Felix Minziro
Yanga inaumana na JKT Ruvu ya Fred Felix Minziro leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, lakini ni kocha mkuu wa kikosi hicho cha wanajeshi anayeweza kutibua hesabu za mwenzake wa Yanga, Hans Pluijm kusaka ubingwa.
Minziro aliyekulia na kucheza soka Yanga kwa maisha yake yote ya miaka 13, aliinoa timu hiyo kabla ya kutimuliwa, anakutana nayo (Yanga) ikiongoza ligi ikiwa na pointi 37 na kufuatiwa na Azam yenye pointi 36 na Simba ni ya tatu ikiwa na pointi 32.
Kocha huyo alisema Yanga wasitarajie mteremko kwao na watakomaa nao leo kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu.
"Tuko vizuri na Yanga wasitarajie mteremko kwetu, tutacheza kwa kiwango kikubwa kuhakikisha tunaibuka washindi, najua ni timu nzuri na inaongoza ligi lakini hata sisi tuko pabaya tunahitaji kujinasua na kupanda nafasi za juu ili kukwepa kushuka daraja," alisema Minziro.
Kwa upande wake, Pluijm amekiri kuwa hautakuwa mchezo rahisi kuikabili JKT Ruvu ambayo ni timu ngumu kama ilivyo ligi yenyewe.
Timu hiyo hivi inaikabili JKT Ruvu ikiwa na presha kwani inahitaji ushindi kwa hali yoyote ile kutokana na wapinzani wao, Azam kuwafuatia kwa karibu.
Pluijm aliliambia gazeti hili kuwa wamejiandaa vizuri, ingawa haitakuwa kazi rahisi kwao kupata ushindi mbele ya wanajeshi hao kwani ligi ni ngumu hivi sasa na kila timu iko katika kiwango kizuri.
Alisema amewaelekeza wachezaji wake kuichukulia kwa umakini mkubwa michezo yote iliyobaki ili waweze kushinda na kutwaa ubingwa.
"Ligi ni ngumu na kila timu imeonyesha uwezo mkubwa na ndiyo maana nasema haitakuwa kazi rahisi kushinda dhidi ya JKT Ruvu, lakini tumejiandaa, wachezaji wangu wako katika kiwango kizuri na naamini tutapata pointi zote tatu.
"Kikubwa ni kushinda kila mechi iliyo mbele yetu, hatuhitaji kupoteza chochote maana mpinzani wetu Azam anatufuatia kwa kasi hivyo lazima tupambane kuhakikisha kila mechi inakuwa kama fainali kwetu, nawaamini wachezaji wangu watafanya kazi nzuri na kuweza kupata ushindi kesho (leo)," alisema Pluijm.
Hata hivyo, Yanga itamkosa mshambuliaji wake mahiri, Amissi Tambwe mwenye kadi tatu za njano, kiungo Andrey Coutinho aliye majeruhi pamoja na Jerryson Tegete anayesumbuliwa na maumivu ya bega.
Mrisho Ngassa aliyekuwa na maumivu ya nyama za paja na kuukosa mchezo uliopita dhidi ya Mgambo Shooting amerejea kikosini na kufanya mazoezi na wenzake jana asubuhi, ingawa daktari wa timu hiyo Juma Sufiani alisema watamwangalia atakavyoamka leo ili kujua maendeleo yake na kama atacheza mchezo wa leo au la.
Hata hivyo, pia kiungo Said Juma Makapu aliyezimia uwanjani dakika za mwisho katika mchezo dhidi ya Mgambo amerejea na kufanya mazoezi na wenzake jana asubuhi.
JKT Ruvu itamkosa Zubery Napho ambaye alipata maumivu katika mazoezi wakati ikijiandaa kuikabili Ndanda wiki iliyopita.
Chanzo:Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.