Skip to main content

Majeshi ya Nigeria yaungwa mkono

Mwakilishi wa katibu mkuu katika nchi za Afrika Magharibi Mohamed ibn chambas
 Mwakilishi wa katibu mkuu katika nchi za Afrika Magharibi Mohamed ibn chambas


Mapambano yanayoendelea dhidi ya magaidi wa boko haramu kaskazini mwa nchi ya Nigeria yanaonekana kuungwa mkono na mashirika mawili ya kimataifa.
Msemaji wa jeshi la anga la Nigeria alithibitisha kupokea taaarifa hiyo kutoka kwa mwakilishi wa katibu mkuu wa umoja wa mataifa katika nchini za magharibi mwa Afrika, Mohamed ibn chambas.
Mwakilishi huyo amesema kuwa”ni muda wetu sote kupambana na kusitisha shughuli za Boko Haram katika ukanda wetu na kuunganisha nguvu ya pamoja kupambana na kikundi hiki, mapigano dhidi ya Boko Haramu yamekuwa ya kimataifa na Afrika nzima na ninaamini majeshi ya Chad yatatuunga mkono kwenye mapambano haya”.
Chambas ameongeza kwamba “kipaumbele cha umoja wa mataifa ni kuimarisha mapambano dhidi ya magaidi wa boko haramu ambao wamesababisha matatizo makubwa nchini Nigeria pia katika nchi jirani za Kameruni, Niger na Chad”.

Comments