Skip to main content

Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf, ametangaza kujitosa katika kinyang’anyiro cha Uwakilishi katika jimbo la Kiembesamaki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kupitia chama cha wananchi CUF

Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf
---
Aliyewahi kuwa Waziri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mansour Himid Yussuf, ametangaza kujitosa katika kinyang’anyiro cha Uwakilishi katika jimbo la Kiembesamaki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Atachukua fomu ya kuwania jimbo hilo kupitia CUF.

Mansour ambaye alifukuzwa uanachama ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Agosti 26 mwaka huu, baadaye alitangaza kujiunga na CUF.

Akituhubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika Uwanja wa Bustanini, Kiembesamaki, alisema tayari amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na ameirejesha.

Mwanasiasa huyo alitumia mkutano huo kuwaomba radhi kwa matendo aliyokuwa akiyaona wakitendewa Wazanzibari, yakiwamo kupigwa na kudhalilishwa na Serikali wakati wote akiwa ndani ya Serikali.

Akizungumzia safari yake ya kujiunga na CUF, Mansour alisema haikuwa rahisi kwake kwani wazee wa Kiembesamaki na wananchi waliamini amekwisha katika siasa.

“Mlilia sana, niliwaambia tulieni wakati bado…milinifariji katika safari yangu ya kujiunga CUF, pamoja na ugumu uliopo lazima niseme ukweli, mlikuwa na wasiwasi kwamba baada ya mimi kwenda jela labda sitogombea.

“Mliona nilikuwa taabani na nawapa pole wale wote waliopata misukosuko kama yangu, wazee walikuwa na wasiwasi labda sitogombea lakini sasa nasema wazi sitorudi nyuma,” alisema Mnsour.

Mansour alisema katika harakati zake za kuwania uwakilishi katika jimbo hilo ataomba kura hata katika matawi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwani ni yeye ndiye aliyejenga matawi hayo.

“Sitoogopa kuingia katika tawi lolote la CCM kuomba kura, yote nimejenga mwenyewe, nitakwenda humo humo, hizi ndiyo siasa za CUF za leo, CCM na CUF wote wangu,” alisema Mansour.

Mansour alisema hajuti kufukuzwa kwake CCM wala hawezi kumnunia mtu yeyote lakini akasisitiza ataendelea kuwaheshimu kwa vile ni chama chao.

Alisema mwaka 2010 yalipokuwapo mazungumzo ya maridhiano aliwaambia wananchi wa Kiembesamaki umuhimu wa maridhiano hayo katika kujenga jamii iliyotulia Zanzibar.

Alisema ingawa wawakilishi wengi walipinga ndani ya Baraza la Wawakilishi lakini hakutetereka kwa kuwa aliamini lengo la maridhiano haikuwa ni kumtengenezea Seif nafasi ya uongozi au mawaziri saba kutoka CUF.

“Maalim hana njaa, mawaziri hawana njaa, lengo ni kuleta utulivu, Maalim anaumwa na siasa hizi za ufisadi, lengo ni kuondoa chuki na kujenga historia mpya na kujenga vyombo vya Serikali vinavyowajibika kwa dola,” alisema Mansour.

Katika mkutano huo, Makamu wa Kwanza wa Rais Serikali Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Seif Sharif Hamad aliwataka viongozi wa Jeshi la Polisi Zanzibar kusoma sheria ya vyama vya siasa na kuacha kuiburuza CUF.

Seif ambaye ni Katibu Mkuu wa CUF, alilazimika kutoa ushauri huo baada ya kile kinachodaiwa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mjini kuuzuia mkutano kwa sababu zisizoeleweka.

Alisema CUF haitaweza kuendelea kuvumilia uonevu unaofanywa na jeshi hilo kwa kuzuia mikutano yao kwa sababu chama hicho kina haki sawa katika serikali ya umoja wa taifa kama ilivyo CCM.

Akizungumzia hatua ya Mansour, Seif alisema Mansour ndiye mgombea sahihi wa Kiembesamaki kwa Chama cha Wananchi (CUF).















http://www.hakingowi.com

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...