Skip to main content

Kauli ya JK kwa Polisi inahitaji ufafanuzi

Rais Jakaya Kikwete amelitaka Jeshi la Polisi nchini kujiandaa kikamilifu kukabiliana na vurugu zozote zitakazojitokeza wakati wa uandikishaji wa wapigakura, upigaji Kura ya Maoni kuhusu Katiba Inayopendekezwa pamoja na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu.
Akizungumza juzi jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya maofisa warakibu wasaidizi iliyofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi, Rais Kikwete alisema dalili zinaonyesha kwamba kuna watu wamejipanga wakiwa na nia ya kuhatarisha amani wakati wa matukio hayo.
Kwa tafsiri yoyote ile, kauli hiyo ya Rais Kikwete ni nzito na pengine ndio sababu wananchi wengi waliotupigia simu jana walionyesha hofu kwamba kauli hiyo inahitaji ufafanuzi, vinginevyo inaweza kuchukuliwa na Jeshi la Polisi kama agizo au kisingizio cha kuvunja haki za binadamu kwa kupambana na wananchi iwapo watapinga au kuhoji ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni za uendeshaji wa matukio hayo muhimu kwa mustakabali wa Taifa letu. Hofu hiyo ya wananchi huenda inatokana na maudhui ya kauli hiyo ya Rais, ambayo imeonyesha kwamba Rais amejiridhisha kwamba watu hao ambao hakuwataja wamejipanga kuhatarisha amani wakati matukio hayo yakiendelea.(P.T)
Hoja ya wananchi hapa ni kuwa, kwa kuwa matukio hayo kama Uchaguzi Mkuu na kadhalika ni muhimu sana kwa hali ya baadaye ya nchi yetu, kama kuna watu ambao kweli wamepanga kuvuruga matukio hayo ni lazima wafichuliwe na kudhibitiwa mapema kabla hawajafanikiwa kuvuruga matukio hayo. Hatudhani kama Rais anaweza kutoa tuhuma nzito kama hizo bila serikali yake kuwa na ushahidi wa kutosha wa kuwapo watu hao, ambao bila shaka ni hatari kwa usalama wa nchi yetu. Katika hali kama hiyo, wananchi wako tayari kushirikiana nayo kuhakikisha matukio hayo ya kihistoria yanafanyika kwa amani na mafanikio makubwa. Hivyo, badala ya Rais kuliagiza Jeshi la Polisi nchini kujiandaa kikamilifu kwa mapambano dhidi ya watu hao, tungetarajia watu hao wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kabla ya kutekeleza njama hizo.
Hicho ndicho chanzo cha wananchi kuwa na hofu. Kauli hiyo ya Rais inachukuliwa kama agizo, ambalo uzoefu wetu umetuonyesha kwamba kwa makusudi au kwa bahati mbaya hutekelezwa na vyombo vya dola na mamlaka nyingine za kiserikali kinyume na ilivyokusudiwa. Mara nyingi kauli za viongozi hutekelezwa vibaya kama hazitolewi ufafanuzi wa kutosha. Kwa mfano, kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyoitoa mwaka jana kwamba wananchi wasiofuata sheria za nchi 'wapigwe tu' ililichochea Jeshi la Polisi kuzidisha vitendo vya uonevu dhidi ya raia, ikiwa ni pamoja na uvunjaji wa haki za binadamu.
Ndio maana wananchi wanataka ufafanuzi kuhusu kauli hiyo ya Rais Kikwete. Kwamba itakuwapo vurugu, hivyo polisi wajiandae na Serikali itawapa vifaa. Wananchi wanaona kauli hiyo imewaacha njia panda na wanahofia polisi itawaelekezea kipigo, kwani wanatambua kwamba amri ya amiri jeshi mkuu ni amri halali kisheria na kikatiba. Ni amri inayotaka utii wa utekelezaji. Ni amri inayohitaji ufafanuzi, kwani ikitolewa katika nchi kama Tanzania ambayo imekuwa ikiongozwa kwa mujibu wa sheria na Katiba inaweza kutafsiriwa kwamba Jeshi la Polisi halitakuwa na jukumu tena la kulinda haki na usalama wa raia. Kinachotakiwa katika kauli hii ya Rais ni ufafanuzi zaidi.
Chanzo:Mwananchi

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...