Skip to main content

NINAPOITAFAKARI CCM NA SERIKALI YAKE NACHANGANYIKIWA KABISA



"Masikio hayawezi kuvuka kichwa, kiongozi wa serikali usiyetaka kuambiwa ukweli na chama nenda kalale, acha kazi." Hii ni kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi, Nape Nnauye aliyoitoa wakati akikemea ule aliouita uzembe wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Nape na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana bado wanaendelea kupaza sauti kuwa baadhi ya wateule wa mwenyekiti wao wa chama, Jakaya Kikwete hawaendani na kasi ya kutumikia jamii.Mwaka jana waliibuka na kibwagizo kuwa, serikali yao inayoongozwa na Rais Kikwete ina rundo la mawaziri mizigo, utashi wao ukawa ni kumtaka mwenyekiti awatimue wasikigharimu chama.
Wakati kionjo hicho cha mawaziri mizigo kikionekana kupoa, wameibua kingine kinachoitwa waziri mzururaji; wakimaanisha Nyalandu. Wametoa hoja ang'olewe akalale kwa kuwa ameonesha kuishindwa nafasi ya uwaziri.
Wamesema wazi kuwa, masikio hayazidi kichwa, tafsiri ni kwamba wanaoingoza serikali ni masikio ya CCM ambacho ndiyo kichwa cha rais hadi katibu tawala. Hapa ndipo ninapoitafakari CCM na serikali yake kiasi cha kuchanganyikiwa.
Kwa nini? Nape na Kinana wanaposema karibu kila walikopita wamekutana na migogoro ya ardhi ikiwahusisha wananchi, hifadhi za taifa na kwa upande mwingine wawekezaji na waziri yupoyupo tu; anazurura, kuna kitu cha kutafakari.
Najiuliza; Kinana anapomuona mzururaji Rais Kikwete aliyemchagua katika nafasi hiyo ya uwaziri anakuwa wapi, kalala? Nape anapomuona Nyalandu kuwa ameshindwa kutekeleza jukumu lake; Rais Kikwete, kasafiri? Nachanganyikiwa kabisa!
Ukifuatilia ziara za Nape na Kinana zinazoitwa za kujenga chama kila walipopita viongozi hao hotuba zao nyingi zimejaa ukosoaji kwa baadhi ya watendaji wa serikali, kwa vinywa vyao wamekiri hadharani kuwa udhaifu huo unakidhoofisha chama chao.
Jambo la kujiuliza; hivi kichwa (CCM) na masikio (watendaji) havina ushirikiano ndiyo maana jamii inashuhudia mkanganyiko huo wa kimtazamo? Ikiwa viungo hivi havishirikiani katika utendaji, wananchi wanavigawanyaje ili kinachoonekana dhaifu wakichukie?
Tangu lini mchongoma ukazaa machungwa? Kamwe chemchemi ya maji haiwezi kutoa maji matamu na maji machungu. Naomba nisikilizwe hoja zangu kwa makini.CCM ya Nape na Kinana, mwenyekiti wake ni Rais Kikwete ambaye ni mkuu wa uteuzi wa karibu nafasi zote nyeti za nchi hii, nafasi hizohizo ndizo zinazopigiwa kelele na wasafisha chama kuwa ni dhaifu ki-utendaji!
Kwa nini tusifike mbali zaidi ya fikra hizo, tuvuke mipaka ya ufahamu mpaka tuusogelee ukweli kuwa anayewaangusha siyo Nyalandu na uzururaji wake bali aliyemteua ambaye ni mwenyekiti wa CCM.
Nashangaa kuaminishwa kuwa chama kinaweza kuwa mtetezi wa wanyonge kwa kiwango wanachoonesha akina Kinana, kuipita serikali ambayo inaongozwa na mwenyekiti wa Kinana.
Hivi mashauriano ya chama kifanye nini hawa akina Nape wanayafanyia nyumbani kwao au ofisini? Wanajipangia watakavyo au vikao vya chama na ridhaa ya viongozi wa ngazi za juu akiwemo mwenyeti ndiyo vinavyotoa baraka ya ziara na kupokea mrejesho wa kilichofanywa na watumwaji!
Ikiwa chama kinaongozwa kwa mfumo, iweje rais ambaye ni mwenyekiti asijue kuwa, Nyalandu ni mzururaji na kumtimua kazi mara moja! Waliitwa mawaziri mizigo wakaendelea kudunda kwenye nafasi zao; Nyalandu kaambiwa aache kazi lakini bado anapanda ndege na kulipwa mshahara unaotokana na kodi za wananchi.
Naomba Nape awaambie wananchi wafanye nini ili watenganishe kichwa na masikio kwa sababu wamechoshwa na umaskini. Asipofanya hivyo ipo siku wataamua kukata shingo, wakiondoe kichwa pamoja na masikio yake kisha wavitupe jalalani! Nachochea tu.CHANZO: GLOBAL PUBLISHER

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.