Skip to main content

Lowassa awekwa mtu kati Monduli

Kiongozi wa madiwani 19 wa ccm,  Julius Kalanga
WAKATI wakongwe wa siasa wakimhadharisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, kutofuata mashabiki wanaomtaka ahame CCM ambako amelelewa na ndiko anakoheshimika, madiwani 20 wa chama hicho katika Jimbo la Monduli, wamejiunga na Chadema.
Madiwani hao wameingia Chadema na kufuatwa na wenyeviti sita wa vijiji pamoja na viongozi wa jumuiya za CCM, huku wakimwomba Lowassa ambaye ni Mbunge wa jimbo hilo, kufanya kinachoitwa ni uamuzi mgumu wa kuwafuata, baada ya CCM kukata jina lake sambamba na wagombea urais wengine 33, wakiwemo waliowahi kuwa mawaziri wakuu kama yeye.
Akizungumza jana katika mkutano wa hadhara, kabla ya kukabidhi kadi yake na za wenzake 19 wa CCM kwa viongozi wa Chadema, kiongozi wa Madiwani hao, Julius Kalanga kutoka Kata ya Lepurko, alisema wamefanya uamuzi aliouita mgumu, ambao Lowassa amekuwa akiuzungumza.
“Sisi tumeamua kujiunga Chadema kutafuta haki na kuondoka CCM ambako wanachakachua Katiba ya Chama kwa kumpitisha kiongozi wanayemtaka, badala ya kufuata Katiba na wananchi wanachotaka. “Tunamwomba Mheshimiwa wetu Lowassa, atufuate huku Chadema, afanye uamuzi mgumu aliokuwa akisema kila siku na asiogope kuhama... atakuwa amefanya uamuzi wenye tija kwa Taifa,” alisema Kalanga.
Diwani huyo pia aliwasihi wananchi kufuata madiwani wao wanakokwenda kwa sababu hata huko watachukua fomu na kugombea ili kuing’oa CCM madarakani.
Waliohama
Madiwani waliohama chama ni wa kata ya Engaruka, Engutoto, Esilalei, Loksale, Majengo, Makuyuni, Meserani, Nalalani, Lemooti, Moita, Monduli Juu, Monduli Mjini, Mferejini, Mswakini, Mto wa Mbu, Migungani, Selela, Sepeko na Lashaini.
Madiwani na viongozi hao ni Kalanga mwenyewe, Edward Lenanu, Bazir Siamini, Sigur Olekibinti, Loti Yamat, Goodluck Lerunya, Pashet Sengurumi, Yase Runja, Gidion Kimongishu, Dora Kipuyo, Mary Morindat, Sara Lomayan na Halima Lusinde.
Wengine ni Dotto Mlacha, Hawa Nyambiry, Alex Kamanda, Sion Kapela, Maria Lemta, Onesmo Naikoyo, Shaban Adam, Enditosidai Naikulo na Elifuraha Simon.
Pia yupo Dinna Solomon, Loti Naparana, Jocy Laizer, Edward Mathayo, Piniel Loning’o, Napir Mukare, Inot Leringa, Kalaine Lowassa, Maria Mepukori, Mary Stivin na Edward Kone.
Ushauri wa wakongwe
Mwito huo wa madiwani wa Monduli, unatofautiana na ushauri wa kada mkongwe wa CCM, Steven Mashishanga, aliyekaririwa akimtaka Lowassa atulie na aachane na ushawishi wa watu wanaomtaka ahame chama hicho.
Mashishanga katika mahojiano yake na gazeti moja la kila siku juzi, alimkumbusha Lowassa kuwa bado ni kiongozi anayeheshimiwa na jamii na kumuasa kuwa kama anahisi ameonewa, asamehe.
Akifafanua hoja zake, Mashishanga alisema wanaomshawishi Lowassa ahame CCM na wale wanaohama chama hicho kwa sababu ya kukatwa kwa jina la Lowassa katika kuwania urais, si wana CCM wa uhakika.
Kwa mujibu wa Mashishanga, ndani ya CCM mgombea akiteuliwa, wanachama huachana na yaliyopita na kuwa wamoja kwa ajili ya kukiendeleza chama.
Malaigwanani
Mbali na Mashishanga, pia wazee wa kimila wa jamii ya wafugaji wa Kimasai, maarufu malaigwanani kutoka Wilaya ya Monduli, nao wamemuomba Lowassa kuendelea kuwa kada wa CCM, kwa sababu ndicho chama kilichomlea na anakijua.
Mmoja wa malaigwanani, Mzee Joseph Mesopiro, kutoka Kata ya Sepeko, alikaririwa na vyombo vya habari kwa niaba ya malaigwanani akisema, wanakusudia kutuma ujumbe maalumu kwa Lowassa, utakaomshauri asihame CCM kama baadhi ya watu aliowaita wapambe wanavyomshauri.
Laigwanani mwingine, Julius Laizer kutoka Kata ya Moita, alisema bado anaamini kuwa CCM itaendelea kubaki imara, hata kama baadhi ya watu watakihama.
Lazier alisema viongozi waliolelewa na kukuzwa CCM, wanaamini chama hicho kitaendelea kuwa imara na hawako tayari kukubali ushawishi wowote wa kutaka wahamie upinzani.
Naye Mwenyekiti wa CCM Kata ya Lepurko wilayani Monduli, Njoput Alami, alikaririwa akibeza taarifa za kushawishi watu kuhama CCM kwa kisingizio cha Lowassa kukatwa katika majina ya wawania urais, akiziita ni kelele za wapambe wanaohofia kukosa fursa walizotarajia, iwapo Lowassa angeteuliwa kuwa mgombea urais wa CCM.
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa aliwakaribisha na kusema Chadema watu wote wanapendana na hakuna ukubwa wala uongozi, hivyo wanapokuja huko ni kazi moja ya ukamanda kuwatumikia wananchi.Chanzo ni http://www.mjengwablog.com

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...