Skip to main content

Mkufunzi Josef Diouf kutoka Shirikisho la masumbwi Dunia (AIBA) atua nchini


Na Mwandishi wetu SHIRIKISHO la Ngumi za ridhaa nchini (BFT) limepiga panga baadhi ya majina ya makocha walioteuliwa kushiriki katika kozi ya kimataifa ya mchezo huo iliyopangwa kufannyika kesho Januari 16 mwaka huu. BFT imewakata washiriki hao baada ya Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) kuwataka BFT kupunguza idadi ya washiriki kutokana na hasara iliyosababishwa na washiriki hao katika kozi ya awali iliyokuwa ifanyike tangu mwezi Novemba mwaka jana. TOC ambayo huandaa kozi za michezo mbalimbali kutokana na ruzuku inayotolewa na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC) ilikuwa iendeshe kozi hiyo tangu mwaka jana lakini haikufanyika kutokana na mkufunzi wa kozi hiyo kutoka nchini Algeria kuingia mitini, Kozi hiyo ya Kimataifa ya Mchezo wa masumbwi kwa mara ya mwisho ilifanyika nchini mwa 2002 ambapo ni ngazi ya juu kabisa ya ukocha Duniani kote
TOC ililazimika kuwalipa nauli baadhi ya washiriki waliotoka nje ya Dar es Salaa kutoka katika fungu la pesa za kuendeshea kozi hiyo hivyo kuwataka BFT kupunguza idadi ya washiriki hasa wale waliofanya utovu wa nidhamu katika kozi ya awali ili kiwango cha pesa kilichobaki kutosheleza mahitaji wa kozi itakayoendeshwa Januari 16 mwaka huu. Akizungumza Dar es Salaam Katibu mkuu wa BFT, Makore Mashaga alisema idadi ya makocha 25 waliowateua inaweza ikapungua tena kulingana na bajeti waliyobaki nayo TOC ambapo hata hivyo hakuyataja majina matano ya washiriki walioachwa . Aliwataja washiriki waliopenya kuhudhuria kozi hiyo ni mpiga picha wa Magazeti ya Busines Time, Majira, Sports Starehe na Jarida la Maisha ambaye pia alikuwa bondia, Rajabu Mhamila 'Super D', Anord Ngumbi, Moses Lema, Anthon Mwang'onda na Edward Emanuel (Dar es Salaam). Wengine ni Yahaya Mvuvi (Tabora), Joseph Mayanga na Zakaria Mwaseba (Morogoro), Omari Saady na Mussa Bakari (Mwanza), Ally Ndee (JKT Mbeya), Emilio Moyo na Gaudens Uyaga (Pwani) Juma Liso (Magereza Kigoma), Lyinda Kalinga (Dodoma) na Abdalah Bakari (Tanga). Wengine ni Mohamed Hashim (Polisi Dar es Salaam), David Yombayomba, Haji Abdalah, Said Omari (JWTZ), Mazimbo Ally, Rogated Damian na Fatuma Milanzi (JKT), Musa Maisori na Hamisi Shaaban (Magereza Dar es Salaam). Kozi hiyo itaendeshwa na mkufunzi wa kimataifa Josef Diouf kutoka Shirikisho la Dunia la mchezo huo (AIBA) ambaye atashirikiana na makamu wa Rais wa BFT, Michael Changarawe. Kozi hiyo itafanyika katika shule ya Sekondari ya Filbert Bayi Kibaha Mkoani Pwani na itafikia tamati Januari 24 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...