MWANAMITINDO wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata amesema hafurahii kuitwa mrembo kwa sababu kazi yake ni tofauti na fani hiyo.
Flaviana (25), ambaye aliwahi kutwaa taji la Miss Universe Tanzania mwaka 2007, alisema hayo wiki hii kupitia kipindi cha Mkasi kilichorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Channel Five.
Alisema kazi ya uanamitindo imempa heshima na thamani kubwa kwa vile anaweza kwenda popote na kusikilizwa, tofauti na wasichana wengine waliowahi kushiriki mashindano ya urembo.
Mwanadada huyo alisema wanamitindo waliopo sasa Tanzania wanajiharibia wenyewe kutokana na kutokuwa makini na kazi yao na pia kutojiheshimu.
Binti huyo maridhawa aliwaponda wabunifu wa mavazi wa Tanzania kuwa, hawawalipi wanamitindo wao inavyotakiwa, badala yake wamekuwa wakiwatumia kujinufaisha.
“Wabunifu hawawalipi wanamtindo wao ndio sababu mimi binafsi hatuelewani. Wengine wanawalipa wanamitindo sh. 50,000 wakati pesa wanazopata ni nyingi.
“Kuna siku niliwahi kuwaeleza baadhi ya wanamitindo bajeti ya wabunifu wa mavazi, lakini wengine hawakujali, pengine kwa sababu wanapenda kuuza sura,”alisema mwanamitindo huyo mwenye makazi yake nchini Marekani hivi sasa.
Flaviana (25), ambaye aliwahi kutwaa taji la Miss Universe Tanzania mwaka 2007, alisema hayo wiki hii kupitia kipindi cha Mkasi kilichorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Channel Five.
Alisema kazi ya uanamitindo imempa heshima na thamani kubwa kwa vile anaweza kwenda popote na kusikilizwa, tofauti na wasichana wengine waliowahi kushiriki mashindano ya urembo.
Mwanadada huyo alisema wanamitindo waliopo sasa Tanzania wanajiharibia wenyewe kutokana na kutokuwa makini na kazi yao na pia kutojiheshimu.
Binti huyo maridhawa aliwaponda wabunifu wa mavazi wa Tanzania kuwa, hawawalipi wanamitindo wao inavyotakiwa, badala yake wamekuwa wakiwatumia kujinufaisha.
“Wabunifu hawawalipi wanamtindo wao ndio sababu mimi binafsi hatuelewani. Wengine wanawalipa wanamitindo sh. 50,000 wakati pesa wanazopata ni nyingi.
“Kuna siku niliwahi kuwaeleza baadhi ya wanamitindo bajeti ya wabunifu wa mavazi, lakini wengine hawakujali, pengine kwa sababu wanapenda kuuza sura,”alisema mwanamitindo huyo mwenye makazi yake nchini Marekani hivi sasa.


Comments