Skip to main content

Misaada zaidi kwa waathirika wa mafuriko


Mkuu wa Mkoa wa DSM Said Mecky Sadick (kulia) akipokea hundi ya shilingi milioni tano
(5m/-) kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Fadhili Manongi (kushoto)
leo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa DSM kwaajili ya waathirika wa mafuriko wa mkoa wa Da r es
Salaam (Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO),



MISAADA BADO INAHITAJIKA
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
 16/1/2012
 
MKUU wa mkoa wa Dares Salaam Said Mecky Sadick amesema bado misaada zaidi inahitajika  ili kuweza kuwasaidia  wahanga wa mafuriko hususan ya  shughuli za ujenzi na mahitaji ya watoto  walioanza shule.
 
Kauli hiyo ilitolewa leo (jana) na Sadick  wakati akizungumza na waandishi wa habari  ofisi kwake jijini Dares Salaam mara baada ya kupokea msaada wa  hundi ya sh. milioni tano kutoka  Mamlaka ya  Usafiri wa Anga Tanzania, ambayo ilikadhiwa kwake na Mkurugenzi Mkuu  Fadhili Manongi.
 
“Bado misaada inahitajika tunaendelea kutoa wito kwa watu walioguswa kuweza kutoa michango yao ili kuweza kusaidia shughuli za ujenzi na mahitaji ya wanafunzi walianza shule mfano madaftari, vitabu na huduma zingine zinazohusiana na elimu,” alisema.  
 
Aliongeza kuwa  changamoto nyingine  iliyopo ni kujenga nyumba za walimu na kliniki ya wakinamama na watoto,hivyo aliwaomba Watanzania, taasisi, mashirika na watu binafsi  walioguswa kuendelea kuchangia.
 
Wakati huohuo, Chama cha Wafanyabiashara wa Kichina Tanzania (CBCT),kilikabidhi hundi kivuli  yenye thamani  sh. milioni 10 ya michango ya vitu mbalimbali kwa  ajili ya wahanga hao kwa Mkuu huyo, ambayo ilikabidhiwa katika sherehe ya mwaka mpya wa Kichina kwa Makamu wa Rais Dk Mohammed  Gharib Bilal juzi usiku.
 
Hundi hiyo   ilikabidhiwa kwa Sadick na Mwenyekiti wa CBRT Zhu Jinfeng, ambapo alisema misaada mingine imendelea kutolewa hivyo michango hiyo hadi leo(jana) imefikia sh. milioni 12,550,000.
 
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa mkoa alisema agizo la kuangalia uwezekano wa  kuwapatia viwanja wapangaji liko palepale na watalitekeleza kama alivyoagiza Rais Jakaya Kikwete, hivyo utaratibu utaanza mara baada kukamilisha zoezi la wamiliki.
 
Aliongeza kuwa utaratibu huo wa wapangaji pia unahitaji fedha  kwa ajili ya kufanya tathimni mpya utoaji wa fidia kwa wananchi watakaopisha maeneo hayo.
 

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.