Skip to main content

tendwa asema cuf ifutwe

ITAKA IREJEE AMRI YA MAHAKAMA, ASEMA ADHABU YA KUIDHARAU NI KUFUTWA
 Waandishi wetu  MSAJILI wa Vyama vya siasa nchini, John Tendwa amekionya Chama cha Wananchi (CUF), kwa kuendesha kikao kilichowajadili na kuwafukuza Hamad Rashid Mohamed na wenzake wakati kimepewa amri na Mahakama Kuu ya kutofanya hivyo huku akikitaka kirejee na kutii amri hiyo.Kauli ya Tendwa imekuja siku moja baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema kusema kitendo hicho cha CUF kuendesha kikao hicho ni ukiukwaji wa Katiba ya nchi. 
“Sijaiona amri ya mahakama (court order) inayowazuia CUF kuendelea na mkutano wao, lakini ninasema kuwa kuna uhalali wa kuwapo kwa tukio hilo? Ushauri wangu ni kwamba CUF warudi kutekeleza amri ya mahakama,” alisema Dar es Salaam jana na kuongeza: 
“Mahakama ni mhimili wa Serikali wenye mamlaka kamili ya Katiba ya nchi. Mahakama imefanya uamuzi unaopaswa kuheshimiwa.”  Alitaja baadhi ya makosa ambayo chama kinaweza kupoteza sifa ya kuwa chama cha siasa kuwa ni pamoja na kukiuka Katiba ya nchi, kuwa na siasa za upande mmoja na kufanya siasa zinazochochea vurugu.

Barua kutoka CUF
 Kuhusu barua kutoka CUF, Tendwa alisema ofisi yake haijapata barua yoyote ya chama hicho inayoeleza kuhusu uamuzi wa kumfukuza uanachama Hamad Rashid na wenzake.  “Mimi sijaona barua kutoka CUF inayohusu kufukuzwa uanachama kwa Hamad na hata ingekuwa imepelekwa Ofisi za Bunge ningefahamishwa,” alisema Tendwa.

 Tendwa alisema sababu zinazotolewa na CUF kuwa Hamad Rashid alikuwa akifanya mikutano kinyume na taratibu za chama, hazina mashiko kwa kuwa hakuna kosa kwa mbunge kufanya mkutano wa hadhara na wananchi.  “Hakuna kosa kwa mbunge aliyechaguliwa na wananchi kufanya mkutano mahali popote katika nchi na kutoa msaada, si lazima kuomba ruhusa kwa yeyote wakati akitekeleza jukumu hilo,” alisema Tendwa.  Aonya vyama

Tendwa alivionya vyama vya siasa kutatua migogoro kwa njia ya mazungumzo badala ya kufukuzana uanachama akisema
mfumo huo ndiyo unaoweza kujenga vyama hivyo na kuvipatia uwezo wa kukubaliwa na wananchi na kupewa dhamana ya kuongoza nchi.  

“Mfano, leo hii  CUF wanachama wake wanarudisha kadi kwa tukio la Hamad… huku ni kukidhoofisha chama,” alisema Tendwa.  Hamad: Sijapewa barua   Kwa upande wake, Hamad Rashid alisema bado hajapewa barua ya kufukuzwa uanachama lakini akasema kwamba viongozi wa CUF wamepeleka barua ya kutomtambua katika Ofisi ya Bunge.  

Alisema hadi jana alikuwa hajapokea barua yoyote inayoonyesha kufukuzwa uanachama, jambo alilodai ni kinyume cha kanuni na taratibu za kumvua mtu uanachama.  “Mpaka sasa sijapokea barua ya kunivua uanachama lakini, nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa viongozi wa CUF wamepeleka barua ya kutonitambua kwa Spika wa Bunge,” alisema Hamad....www.mwananchi.co.tz

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...