Skip to main content

Majambazi wavamia ndege ya dhahabu

Pichani: Wakazi wa Wilaya ya Geita mkoani Mwanza, wakiangalia mwili wa mtu anayesadikiwa kuwa ni jambazi (jina hajafahamika), akiwa ni mmoja wa watu wanne waliyovamia mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM), akiwa amekufa baada ya kupigwa risasi na askari polisi katika jaribio hilo la kutka kupora dhahabu jana. (Picha na Sitta Tumma)
 WATU wanne wanaosadikiwa kuwa majambazi wamevamia mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM), na kuteka ndege ya kubeba madini hayo na kupora vitofali 68 vya dhahabu iliyokuwa ikisafirishwa kutoka mgodi huo kwenda nje ya nchi yenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni 130.

Hata hivyo, majambazi hao walishindwa kuondoka na dhahabu hiyo baada ya polisi wilayani hapa kuwahi kufika eneo la tukio na kuiokoa, baada ya kupambana na majambazi hao kwa
kurushiana risasi na kuua mmoja.

Dhahabu iliyonusurika kuporwa na majambazi hao kwa mujibu wa madai ya mmoja wa polisi aliyeikagua ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini, ilikuwa ni zaidi ya kilo 1,000.

Polisi huyo alidai kuwa dhahabu hiyo ilikuwa imegawanywa katika makasha 16 huku kila kasha likiwa na vitofali vinne vya dhahabu na kila kitofali kikiwa na uzito wa kilo 25.

Hata hivyo, Ofisa Madini mkazi wa Kanda ya Geita, Juma Sementa, ambaye ofisi yake imekuwa ikikagua na kuhakiki dhahabu kabla ya kusafirishwa kila wiki na mgodi huo, alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu uzito kamili wa dhahabu iliyokaguliwa na ofisi yake juzi kabla ya kusafirishwa
jana, alitofautiana na madai ya polisi.

Sementa alisema ofisi yake ilikagua makasha 25 na kila kasha likiwa na kitofali kimoja cha dhahabu chenye uzito wa kati ya kilo tano na 30.

Katika tukio hilo la aina yake, polisi walimuua mtuhumiwa mmoja baada ya kummiminia risasi kifuani, ingawa tayari alikuwa amejeruhiwa na mmoja wa walinzi wa mgodi huo ambaye ni
raia wa Afrika Kusini.

Tukio hilo lilitokea jana saa 5.55 adhuhuri katika uwanja wa ndege wa mgodi huo ulioko umbali wa kilometa tano kutoka katikati ya mji wa Geita.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka eneo la tukio na kuthibitishwa na baadhi ya maofisa wa polisi wilayani hapa, uchunguzi wa awali ulionesha kuwa majambazi wapatao
wanne walivamia mgodi huo wakiingilia lango kuu la uwanja huo wa ndege.

Ilielezwa kuwa majambazi hao wakiwa na mabomu ya kutupa kwa mkono, bunduki aina ya SMG na bastola, waliishambulia kwa risasi ndege iliyokuwa ikipakia dhahabu kutoka kwenye gari maalumu.

“Hali hiyo iliwafanya walinzi wa mgodi huo waliokuwa wakilinda usalama wa mali iliyokuwa ikisafirishwa, kutimua mbio, lakini alibaki Mzungu raia wa Afrika Kusini mfanyakazi wa
mgodi huo, aliyekuwa na bastola.

“Raia huyo wa Afrika Kusini alipambana na majambazi hao kwa kuwafyatulia risasi,’’ alisema mmoja wa maofisa wa Polisi katika mahojiano maalumu na gazeti hili.

Ilidaiwa kuwa wakati raia huyo akiendelea kufyatuliana risasi na mmoja wa majambazi hao, aliishiwa risasi na kujeruhiwa kwa kupigwa risasi kwenye mkono na kukimbia kuokoa maisha
yake.

Hata hivyo, baada ya muda mfupi, inadaiwa askari Polisi walifika na kupambana na majambazi hao ambapo watatu walitimua mbio na kubaki mmoja ambaye tayari alikuwa amejeruhiwa
na Mzungu huyo; akashambuliana kwa risasi na polisi, lakini alizidiwa na kuuawa.

Bastola, mabomu, bunduki
Jambazi aliyeuawa bado hajatambuliwa jina na alikutwa na bastola aina ya Chenese namba 0048467 ikiwa na risasi sita, na bunduki aina ya SMG namba UA89381997 inayoonekana kusajiliwa Uganda.

Pia alikutwa na mabomu manne ya kutupa kwa mkono, magazini nne na risasi 60 ambazo hazijatumika, huku akiwa amevalia nguo za kawaida nguo nne ndani na ya juu ikiwa ni sare za
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Jambazi huyo naye alimjeruhi kwa risasi mfanyakazi mwingine wa mgodi huo, raia wa Afrika Kusini aliyetambuliwa kwa jina la Engenas Van Der Schuffs, baada ya kumpiga risasi kwenye mkono wa kulia.

Marubani wa ndege iliyoshambuliwa yenye namba SH-TZX walitambuliwa kwa majina ya Meja Kondo Hamza na Hamdan Salehe.

Hata hivyo, habari zilizopatikana kutoka eneo la tukio zilisema ndege hiyo ilishindwa kuondoka kwenye uwanja huo kutokana na moja ya mabawa yake kutobolewa kwa risasi.
Chanzo:Habari Leo
0 comments

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Uganda Police issue fresh terror alert

  By Chris Kiwawulo, The Police have issued a fresh terror alert against a possible attack on Uganda by four terrorists from Kazakhstan. Police spokesperson Judith Nabakooba “We have received a security notification in form of an orange notice of four terrorists originating from Kazakhstan who are planning to travel to foreign countries in order to commit attacks and participate in hostile acts,” Police spokesperson Judith Nabakooba said in a statement on Monday. Nabakooba named the four active members of radical organizations as; Nassiruauly Kairat, Umurzakov Marat Eskendirovich, Kovtun Denis Valerevich and Mazhibayen Alimzhan Akhlazhanovich. By press time, a search on the international web has not yielded anything on the named persons.Last evening, police said that in collaboration with other security agencies vigilance has been stepped up to avert the terrorists’ evil plans. Police have in the past issu...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...