Skip to main content

WAZALISHAJI WATAKIWA KUHAKIKI UBORA WA BIDHAA ZAO KUPITIA MAABARA ZA TBS



Frank Mvungi

MAELEZO

DAR ES SALAAM

SERIKALI imewataka wazalishaji na wajasiriamali nchini kuhakikisha kuwa bidhaa

wanazozalisha zinakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Shirika la Viwango

Tanzania (TBS) ili kuchochea ukuaji wa uchumi.





Kauli hiyo imetolewa Leo Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Maabara ya

Uhandisi wa Ujenzi ya Shirika la Viwango Nchini, Mhandisi Stephen Minja wakati wa

ziara ya waandishi wa habari kutembelea na kujionea namna maabara za shirika hilo

zinavyotekeleza jukumu lake la kuhakiki viwango vya ubora hapa nchini.

Akifafanua zaidi Minja amesema kuwa mabara za shirika hilo zipo kwa ajili ya

kuhudumia wazalishaji wa bidhaa mbalimbali na wale wanaoingiza bidhaa kutoka nje

ya nchi lengo ili kuhakiki ubora wa bidhaa zote ili kuepusha athari zinazoweza

kujitokeza kwa watumiaji.
“Maabara yetu ina viwango vya kimataifa na gharama zake ni nafuu ambazo kila

mwananchi anaweza kumudu lengo likiwa ni kutoa huduma kwa wananchi na

kuchangia kuchochea maendeleo kwa kudhibiti bidhaa hafifu” alisema Minja

Aliongeza kuwa maabara hiyo inapima bidhaa za ujenzi kama nondo, chokaa, vigae,

mbao, mabomba ya maji, simenti, nguzo za umeme,matofali,zege, mchanga na

bidhaa zote zinazotumika katika ujenzi wa barabara ikiwemo lami.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa kitengo cha maabara ya umeme, Mhandisi Anectus

Ndunguru amesema kuwa vifaa vyote vya umeme vinavyozalishwa na kuingizwa nchini

lazima vipimwe ubora wake kuona kama vinakidhi vigezo ili kuepusha majanga.

Alitaja baadhi ya vifaa ambavyo lazima vihakikiwe ubora wake kuwa ni vifaa vyote

vinavyotumika katika kujenga mfumo wa umeme katika majengo, taa za majumbani,

pasi, redio, televisheni, waya .
Akizungumzia athari za kutumia vifaa visvyo na ubora Ndunguru amesema kuwa athari

za matumizi ya vifaa hivyo ni makubwa ikiwemo kusababisha majanga na kupotea kwa

umeme hivyo kuongeza gharama kwa mtumiaji.

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limekuwa likisisitiza matumizi ya bidhaa zenye

ubora na zilizohakikiwa na kuepuka bidhaa hafifu ambazo kwa sasa zimedhibitiwa na

shirika hilo kwa kiwango kikubwa hali inayochochea ukuaji wa sekta ya Viwanda hapa

nchini.



Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.