Skip to main content

Wajua Umuhimu wa namba tisa

ZURICH, USWISI
Anthony Martial (katikati) akifunga bao dhidi ya Liverpool, Clyne (kushoto) akisindika kwa macho

KUNA washambuliaji wengi katika ulimwengu wa kandanda katika Ligi Kuu nchini Tanzania utakutana na namba tisa wengi kama John Bocco, Amis Tambwe, Donald Ngoma, Malimi Busungu na wengine wengi.
Nje  ya Tanzania utawaona Michael Olunga (Kenya), Edin Dzeko (Bosni-Herzegovina), Luis Suarez (Uruguay), Clint Dempsey (Marekani), Mario Balotelli (Italia) na kadhalika.
Mfano wetu utaanzia kwa nyota aliyekuwapo Liverpool ya England na sasa yupo katika klabu ya AC Milan huyo ni Mario Balotelli.
Alipokuwa Liverpool wengi walikaririwa wakisema uwezo wa nyota huyo umekwisha hivyo kocha wake wakati huo Brendan Rodgers ikaonekana  alifanya usajili usio kuwa na macho akimwacha Luis Suarez atimkie Barcelona ya Hispania.
Swali ni kweli Balotelli alikuwa akichezeshwa kama yeye alivyo au kocha Brendan alikuwa akimtengeneza kwa ajili ya nafasi  nyingine, jibu kale tutalipata mbele.  
LEO tujikite katika uchambuzi wa namba washambuliaji  wanavyotakiwa kuwa ili kuzifanya timu kuwa na matokeo mazuri dimbani.
Mshambuliaji wa shabaha
Nguvu, uimara na umbo linaloonekana ni mahitaji ya kwanza kwa ‘foward’ yeyote duniani.
Uwezo wa kukaa na mpira na uwezo wa kuuweka mwili wake kati ya mlinzi wa timu pinzani na mpira ni sifa muhimu katika nafasi ya ushambuliaji.
Anapaswa kuwa na uwezo wa kukaa na mpira  ili awaruhusu wachezaji wenzake kufika na kutengeneza mashambulizi.
Timu nyingi hupenda kuwatumia washambuliaji wa jinsi hii ili kupata matokeo mazuri.
Kwa mfano Chelsea, Stoke City, West Ham katika Ligi Kuu ya England (EPL) na Real Madrid  katika La Liga.
Jamie Carragher wa Liverpool aliwahi kumsifia Rick Lamert kuwa ni mshambuliaji mwenye shabaha kuliko Balotelli, je ni kweli?
Mshambuliaji mwenye shabaha ni lazima awe na uwezo mkubwa wa kupiga mashuti yenye nguvu yanayolenga goli ili kuwachanganya walinzi wa timu pinzani.
Hapa utakutana na nyota kama Peter Crouch, Wilfred Bony, Diego Costa, Riobin van Persie, Mario Mandzukic, Didier Drogba na wengine.
Washambuliaji hawa wamebarikiwa sana huwa ni wazima sana wanapopata mipira ya hewani pia hutoa msaada mkubwa wakati wa kulinda kona zinapopigwa kwenye lango lao na mapigo huru.
Mshambuliaji mwizi
Unawakumbuka Ruud van Nistelrooy, Filipo Inzaghi na Raúl Gonzalez walipokuwa katika ubora wao?
Washambuliaji hawa siku zote hawakusimama pekee yao wakisubiri kuletewa mipira kama barua lakini walikuwa na kipaji  cha kujua ni wapi wasimame  ambako ni sahihi kwa muda mwafaka.
Uwezo wao mkubwa wa umaliziaji  katika eneo lolote ndani ya kisanduku cha penalti uliwafanya wang’are isivyokuwa kawaida.
Utamjua tu pindi atakapoukwamisha mpira katika nyavu za lango la mpinzani lakini unaweza kujiuliza mbinu aliyoitumia.
Jibu lake  ni jepesi tu, walikuwa makini na haraka kuiba mipira kwa wachezaji wa timu pinzani pindi wanapozubaa katika kisanduku cha penalti.
Hapa kuna mchezaji mahiri kutoka Cameroon, Samuel Eto’o hakika utamkubali nyota huyo kwa wizi aliokuwa akiufanya katika kisanduku cha goli la mpinzani na kuukwamisha mpira wavuni.
Sir Alex Ferguson aliwahi kusema kuhusu Inzaghi kuwa “Huyu alizaliwa kwa offside” akiwa na maana namna alivyokuwa akijiweka katika uwanja utafikiri yupo ‘offside’ kumbe sekunde mbili mbele yupo eneo jingine ukifunguka sekunde ya tano tayari ashafunga.
Namba 9 wa uongo
Mchezaji mwenyewe anaweza kujitengeneza anapokuwa dimbani kuwa namba 9 wa uongo kama alivyo Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ambapo wao kwa asili sio ‘forward’.
Kwa kufanya hivyo utawachanganya walinzi wa timu pinzani  kwani utakuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira na kutembea na mpira hatimaye utaweza kutoa pasi ya mauaji  kwa ajili ya kuangalia namna mtakavyocheza ‘One-Two’
Mfumo huo pia uliweza kumuibua Cesc Fabregas kama ‘Namba tisa wa uongo’.
Jambo la msingi hapo ni kuwa mmwepesi hali itakayokufanya uogopeke na walinzi wa timu pinzani.
Trequartista
Trequartista imekuwa maarufu sana nchini Italia ambapo robo tatu ya uwanja hujazwa na forward au kiungo mshambuliaji ambaye ataimiliki robo tatu ta uwanja huo .
Ataweza hivyo tu endapo ana uwezo mkubwa kuwa kupiga pasi, kuona, kumiliki mpira na maarifa mengine ya kandanda lakini kubwa zaidi ni  uwezo mzuri wa kupiga katika lango la mpinzani.
Utawakumbuka Diego Maradona, Zinedine Zidane, Riquelme na Johan Cruyff, Alessandro del Piero.
Kwa sasa utakutana na David Silva, Isco na Juna Mata pia Rooney.
Mshambuliaji anayepanua uwanja
Hapa huwezi kumuacha Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Alexis Sanchez.
Mara nyingi mshambuliaji wa aina  hii hupenda sana kucheza katika winga huku wakijivunia kuwa na mguu imara, kasi na stamina.
Timu zinazopenda kutumia mashambulizi ya ghafla basi huwatumia sana nyota wa jinsi hii ambao wana nguvu za kuwazidi walinzi wa pembeni (full backs).

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.