Skip to main content

Kwa wachezaji ni bahati wachezaji kupata bahati ya kushiriki michuano ya olimpiki


BUENOS AIRES, ARGENTINA
Roberto Ayala
SIO wachezaji wote hupata bahati ya kushiriki michuano ya olimpiki katika maisha yao hususani katika mchezo wa kandanda.

Hata hao waliobahatika huweza kutwaa medali mbili tu.
Miongoni mwao ni Muargentina Roberto Fabian Ayala ambaye alifanikiwa kuitumikia timu ya taifa katika michuano iliyofanyika Atlanta, Canada mwaka 1996 na ile ya mwaka 2004 jijini Athens nchini Ugiriki.
Alipewa jina la ‘El Ratón’ na mashabiki  yaani ‘The Mouse’ kifaa kimojawapo katika kompyuta.
Nyota huyo anasimulia namna ambavyo ina maana kwa mchezaji wa kandanda wa kiwango cha Kimataifa anapoitumikia nchi yake katika michuano ya Olimpiki.
Kwa miaka 15 Ayala alikuwa nyota na nembo ya La Albiceleste.
“Unapokuwa mchezaji, ndoto zako na malengo ni kucheza Kombe la Dunia. Lakini michuano ya Olimpiki ni tofauti kabisa unapotaka kucheza cha kwanza kabisa ni pale unapostaajabishwa na wanamichezo wote kukaa katika kijiji kimoja.”
Ayala ambaye amewahi kuhudumu River Plate, Napoli, AC Milan, Real Zaragoza katika nafasi ya ulinzi wa kati anaongeza, “Nilikuja kujua katika olimpiki yangu ya pili nini maana ya kuwa mwanamichezo. Atlanta ulikuwa mji wa tofauti na ulikuwa mbali lakini mwaka 2004 tulipokaa katika kijiji cha olimpiki niliweza kujionea roho za michezo ya ridhaa ilivyo katika eneo hilo. Muulize mchezaji yoyote dunia mahali popote huwa kinatokea nini ukiwa hapo.”
Hatasahau
Mwaka 1996 Nigeria ilizabua Argentina mabao 3-2. “Tulipoteza katika dakika za mwisho, wakati tukitaka kucheza mtego wa offside, tulikosolewa sana kwa aina hiyo ya uchezaji. Tulijiandaa kwa kila hatua na ilikuwa sahihi kuitumia wakati huo,” alisema Ayala na kuongeza.
“Tatizo lilikuwa ni moja tu, mchezaji wetu mmoja alibaki. Tulithubutu kufanya hivyo na ikatugharimu. Nigeria ilikuwa timu nzuri  sijawahi kuona. Hatukuweza kupoteza kwa timu ya zamani. Ilikuwa ikitutesa sana kwa wakati huo, lakini tukaja kutambua kuwa medali na uzoefu ndio vya thamani,” alisema nyota huyo.
Miaka minane baadaye walitua jijini Athens, ambako Argentina ilitua na fasheni iliyowafanya kutwaa medali ya dhahabu. Kwa kufanya hivyo walishinda michezo sita wakitupia wavuni mabao 17 na kuruhusu moja huku wakimtambulisha rasmi mshambuliaji Carlos Tevez ambaye alitunukiwa tuzo ya ‘Fair Play’.
“Tulipoteza fainali ya Copa America, ilitutia uchungu sana. Timu ili haikuruhusu hata bao moja ikicheza kandanda safi. Binafsi ninakumbuka nililia sana baada ya mchezo ule, nilipiga magoti na kumkumbatia Javier Mascherano tulipotwaa medali pale Athens, ilikuwa ni taji kubwa maisha kuwahi kushinda nikiwa na timu ya taifa,” alisema Ayala.
Nyota huyo wa Argentina mwenye miaka 43 ametoa hamasa kwa kikosi cha sasa cha taifa lake kuwa kinapaswa kupambana kupata medali kwani kina kila sifa za kuweza kufanya hivyo.
Ikumbukwe kwamba ni mchezaji ambaye anashikilia rekodi ya kucheza mechi niyingi kuliko mchezaji yeyote mechi 115 na 63 kati ya hizo akiwa ni nahodha wa La Albiceleste.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...