Skip to main content

TFDA imefanikiwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea

MAMLAKA ya chakula na dawa (TFDA), imefanikiwa kufikia na kuvuka malengo iliyojiwekea katika udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendendanishi ili kulinda afya ya jamii.

TFDA imeweka mifumo na taratibu za ndani za utoaji huduma bora kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya ISO 9001:2015 kwa huduma za kawaida na ISO 17025:2005 kwa huduma za maabara.

Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Adam Mitangu wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa kazi za udhibiti wa ubora,usalama na ufanisi wa bidhaa chini ya serikali ya awamu ya tano.

Alisema kuwa,mfumo wa usajili wa bidhaa umeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo idadi ya bidhaa za chakula,dawa, vipodozi,vifaa tiba na vitendanishi imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka,katika kipindi cha 2015/2016 hadi17/18.

''TFDA imesajili jumla ya bidhaa 14,345 kutoka bidhaa 8,866 zilizokuwa zimesajiliwa mwaka 2015/16 ambapo ni sawa na ongezeko la asilimia 62, ambapo imetokana na kuongezeka kwa uelewa wa matakwa ya sheria miongoni mwa wafanyabiashara na kukua kwa biashara,''alisema Fimbo.

Alisema TFDA imeweka mifumo ya utoaji wa huduma kwa kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) ambapo taarifa na takwimu TFDA zikiwemo za bidhaa na majengo yaliyosajiliwa na zile za wateja zimewekwa katika mfumo maalumu uitwao IMIS.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa,  mfumo wa IMIS kwa kiasi kikubwa umerahisisha utoaji huduma kwa wateja na kwa sasa wateja wanaweza kuleta maombi yao kwa mtandao bila kufika ofisi zao.

TFDA imeeleza kuwa mifumo mingine ambayo imewekwa na mamlaka hiyo ni pamoja na usimamizi wa rasilimali watu (HR-MIS), uhasibu (EPICOR) pamoja na mahudhurio kazini na mfumo  wa usimamizi wa taarifa za uchunguzi wa maabara(LIMS).

''Ukuaji wa viwanda vya ndani na uwezeshaji wa wasindikaji wa chakula katika jitihada za kujenga Tanzania ya viwanda ifikapo 2025, TFDA imekua mstari wa mbele katika kutoa msaada wa kiufundi na kuwajengea uwezo wenye viwanda vya dawa nchini na kushawishi wawekezaji kujenga viwanda vya dawa,''alisema Fimbo.

Vile vile kuhusiana na sampuli katika maabala ya TFDA imekuwa na jukumu la kufanya uchunguzi wa sampuli za chakula kwa lengo la kujiridhisha na ubora na usalama wake kabla ya kufanya maamuzi ya kiudhibiti ndani ya mamlaka hiyo.

Comments