Skip to main content

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezindua Chaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezinduaChaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel na amewataka watu wote waliopewa dhamana ya kuiendesha wahakikishe wanazingatia viwango vya kimataifa katika vipindi watakavyokuwa wanaviandaa.
“Vipindi vyenu ni lazima vivutie kama vile tunavyoviangalia katika chaneli za wanyama za kimataifa kama vile National Geographic, Discovery, Travel na zingine ili lengo lililokusudiwa wakati wa kuanzishwa kwake litime.”

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Desemba 15) wakati akizindua chaneli hiyo kwenye Ofisi za TBC, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo ametoa wito kwa Wizara zote zinazohusika na uanzishwaji wa Chaneli hiyo kuhakikisha zinailea wakati ikijijenga kujiendesha kibiashara.

Amesema Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizotenga moja ya tatu ya eneo lote la nchi kwa ajili ya uhifadhi, ambapo kuna tamaduni za makabila mbalimbali, ngoma za kuvutia, vyakula vya asili, sinema za maisha yetu na lugha adhimu ya Kiswahili.

“Hivyo, kwa kuanzishwa kwa chaneli hii inayotengeneza vipindi na kuonesha vivutio hivi ndani na nje ya Tanzania itasaidia watalii huko waliko kujua huu utajiri wetu na kuchagua kuja kutalii nchini. Ni matumaini yangu kuwa hii Tanzania Safari Channel ninayoizindua leo itaongeza thamani katika kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea Tanzania.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametaja faidazinazotokana na utalii ambazo ni pamoja na kuliingizia Taifa fedha za kigeni, ambapo kiasi cha Dola za Kimarekani bilioni 2.3 zimeingia kwa mwaka 2017. Fedha hizo ni sawa na sh. trilioni 5.04.

Pia sekta hiyo ya utalii inatoa ajira kwa Watanzania zaidi ya milioni 1.5 wanaojihusisha katika shughuli mbalimbali zikiwemo usafiri wa ndani kwa watalii, uongozaji watalii kwenye maeneo yenye vivutio, kuuza bidhaa kwa watalii kama vyakula, vinywaji, vinyago, nguo, zawadi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema licha ya mafanikio hayo, lakini hatupaswi kuridhika nayo kwani Tanzania inapokea watalii milioni 1.3 kwa mwaka wakati nchi kama Misri na Afrika Kusini hupokea zaidi ya watalii milioni 10.

“Lazima tujiulize, ni kwa nini sisi tulio na vivutio vingi kuanzia hifadhi maarufu ya Serengeti, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro, hifadhi ya Ruaha, Sadani (Hifadhi pekee iliyopakana na bahari), Zanzibar ambako  kuna fukwe maridadi, malikale, maporomoko ya maji na vingine vingi na baadhi ya hivi vivutio vimewekwa katika kundi la maajabu ya Dunia tunapata watalii wachache.”

Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuhusu uboreshwaji wa bustani katika barabara inayotokea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, ambapo amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isac Kamwelwe asimamie jambo hilo pamoja na matangazo yanayowekwa katika barabara hiyo yaoneshe vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Kadhalika uzinduzi huyo ni utekelezwaji wa maagizo ya Rais Dkt. John Magufuli aliyoyatoa Mei 16 mwaka jana alipotembea TBC kuwa, pamoja na mambo mengine aliwataka waangalie uwezekano wa kuanzisha chaneli itakayotangaza hifadhi na vivutio vya utalii nchini.

Pia Uzinduzi wa Chaneli hiyo ya utalii ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 29 iliyoielekeza Serikali kuweka mkakati wa kimataifa wa utangazaji wa utalii ili kuwavutia watalii wengi zaidi na kufikia idadi ya 2,000,000 ifikapo mwaka 2020.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Khamis Kigwangala. Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isac Kamwelwe pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.