Skip to main content

Yanga yaeleza kilicho izamisha 2-0 nyumbani


Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga sasa inahitaji ushindi wa mabao 2-0 ugenini, ili kusonga mbele kwa mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.





Bao la mshambuliaji Obrey Chirwa halikutosha kuisaidia Yanga kuepuka kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya 2-1 na Township Rollers kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizunguzia kipigo hicho Kocha msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa alisema kosa kubwa walilofanya ni kuwaruhusu wapinzani wao kuchezea sana mpira.

"Tumeshajua wapi ambapo tumekosea baada ya mchezo huu, tuliwaacha sana wenzetu wakicheza, kikubwa tunajipanga kwaajili ya mechi ijayo," alisema.

Yanga inayoandamwa na majeruhi katika kikosi chake cha kwanza ilianza mchezo huo wakimtumia kipa wake chipukizi Ramadhani Kabwili huku mkongwe Mcameroon Youth Rostan akiwa benchi.

Kocha wa Yanga, George Lwandamina ambaye jana hakuonekana katika mkutano wa wanahabari aliingia katika mchezo huo akitumia mfumo wa 4-4-2, kwa kuwaanzisha mbele Chirwa na Ibrahim Ajibu.

Lwandamina anayehusishwa na kutakiwa na Zesco alionekana kuzidiwa mbinu na mpinzani wake Nikola Kavazovic wa Rollers ambaye alisema tangu juzi kwamba ataingia uwanjani kwa kuhakikisha hawapi Yanga nafasi  kumiliki mpira.

Mbinu hiyo ya Msebria zilifanikiwa baada wachezaji wa Rollers kutawala mchezo wao kuamua ni vipi mchezo utakwenda huku Yanga wakionekana muda mwingi wakipoteza malengo yao.

Dakika 11, Township Rollers ilipata bao la kuongoza lililofungwa na Lemponye Tshreletso kwa shuti kali akiwa umbali mita 25.

Baada ya bao hilo Yanga iliamka na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha dakika 30, wakati Chirwa alipomalizia kazi nzuri ya Papy Tshishimbi aliyegongeana na Pius Buswita kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa sare ya bao 1-1.

Kipindi cha Pili Yanga iliingia kwa kasi na kufanya mashambulizi mfululizo langoni mwa Township lakini kukosa umakini kwa washambuliaji wake Ajibu, Chirwa, Juma Mahadhi kuliwanyima mabao.

Kila dakika zilivyokuwa zinaenda ndivyo wachezaji wa Yanga walivyoanza kuonyesha dalili za kuchoka na kutoa mwanya kwa wageni kutawala mchezo.

Mabingwa hao wa Botswana aliandika bao la pili dakika 83, kupitia Motsholetsi Sikele akipiga shuti mbele ya kipa Kabwili.

Kabla ya bao hilo Rollers walipigiana pasi zaidi ya 20 wakiwavuta wachezaji wa Yanga kabla ya kupenyezwa pasi kwa mfungaji akiwa ndani ya eneo la 18 la Yanga.

Kocha mkuu wa Township Rollers, Kavazovic alisema bado anaiheshimu Yanga licha ya kupata ushindi huo.

"Nimekuwa nikiifuatilia klabu hii wiki tatu nyuma ili nijue wanachezaje, wazuri bado nawaheshimu katika mchezo wa marudiano tukiwa nyumbani," alisema Kavazovic.

Huu ni ushindi wa kwanza kwa Township Rollers kushinda ugenini katika mashindano ya CAF tangu 2015.

Kabla ya mechi hiyo mabingwa hao wa Botswana mafanikio yao makubwa ugenini ni kupata sare moja tu, lakini michezo yote wamefungwa ila ni hatari zaidi wanapocheza nyumbani.

Rollers imefungwa mechi moja tu nyumbani ilipofungwa na Kaizer Chiefs bao 1-0 katika mchezo uliofanyika Februari 28, 2015 katika mchezo wa kwanza waliocheza Afrika Kusini pia Chiefs ilishinda 2-1.

Tangu wakati huo imecheza mechi sita za mashindano na kirafiki na klabu mbalimbali imefungwa michezo mitatu ya ugenini na kupata sare moja wakati ikishinda mbili za nyumbani.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...