Skip to main content

Miguna Atakiwa Kuomba Tena Uraia Wa Kenya


Taarifa kutoka Idara ya uhamiaji nchini Kenya zinasema idara hiyo imemtumia fomu mwanasheria na mwanaharakati wa vuguvugu la NRM nchini Kenya Miguna Miguna ili azijaze kuomba tena uraia wa Kenya na kumuwezesha kuingia tena nchini humo.
Miguna ambaye alipambana na kuishinda Serikali katika jaribio lao la kutaka kumrejesha tena nchini Canada kupitia Dubai usiku wa kuamkia leo ambapo mwenyewe amesisitiza kuwa ni raia wa Kenya na haitaji kusalimisha nyaraka zake za kusafiri ili zipigwe muhuri.
Hata hivyo kaimu mkurugenzi wa idara ya uhamiaji nchini Kenya Joseph Munywoki amesisitiza kuwa mwanaharakati huyo alipoteza haki ya kuwa raia wa nchi hiyo mwaka 1998 wakati alipokuwa rasmi raia wa Canada na wakati huo nchi ya Kenya ilikuwa hairuhusu uraia wa nchi mbili.
Baada ya Miguna Miguna kuleta taharuki kwenye uwanaja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta na hata kuvutana mashati na maofisa wa idara ya uhamiaji na kugoma kuingia kwenye ndege aliyotaiwa kusafiri nayo kwenda Dubai, idara ya uhamiaji iliamua kumuachia na kumpa fomu hizo.
“Ili kuruhusu Miguna kupata tena uraia wake, idara ya uhamiaji imemtumia fo,mu maalumu azijaze kuomba tena kwa utaratibu,” imesema taarifa ya uhamiaji.
Munywoki ambaye anakaimu ukurugenzi wa idara ya uhamiaji, amesema ili Miguna aruhusiwe kuingia nchini humo kama raia wa Kenya ni lazima ajaze fomu hizo upya kuomba kuwa raia wa Kenya.
Mkurugenzi huyo amesema hata hivyo mpaka sasa mwanaharakati huyo wa NASA hajajaza fomu hizo.
Ameongeza kuwa Miguna aligoma kutoa nyaraka zake za kusafiria kwaajili ya ukaguzi na kupigwa muhuru kama sheria inavyotaka pamoja na zile sheria za kimataifa.
Mwanasheria huyo aliwasili nchini Kenya akitokea Canada maajira ya 2.30 kwa saa za Afrika Mashariki akiwa amepanda ndege ya shirika la Emirates.
Wizara ya mambo ya ndani imesema kuwa katika kutekeleza maagizo ya mahakama walimuomba miguna awasilishe nyaraka zake alizotumia kusafiria ili aruhusiwe kuingia nchini humo lakini hakufanya hivyo.
Idara ya uhamiaji nchini Kenya mwezi mmoja uliopita ilimfurusha nchini humo Miguna kwa kile ilichodai anatishia usalama wa taifa na kwamba sio raia wa Kenya baada ya kuukana.
Tangu kumalizika kwa uchaguzi wa marudio mwezi Octoba mwaka jana, Miguna amekuwa akiongoza harakati za vuguvugu la Nasa akipinga ushindi wa rais Uhuru Kenyatta ambapo amekuwa mkosoaji mkubwa wa Serikali na hata kutishia kuchoma picha za rais
.

Comments

Popular posts from this blog

Thousands of protesters clash with police in Chicago: Chaos in the Windy City as 45 activists arrested and one cop stabbed after demonstrators target NATO

By DAILY MAIL REPORTER Thousands of demonstrators upset with the war in Afghanistan, climate change and the erosion of union rights have raised the intensity of a march in downtown Chicago on Sunday as world leaders assembled for a NATO summit. The protest, one of the city's largest in years, turned violent at the end of an anti-NATO march, where demonstrators confronted Chicago police, pushing against a line of officers several blocks from the lakefront convention center where President Obama hosted a gathering of world leaders. Authorities were seen making arrests one by one and leading individual demonstrators away in handcuffs. After a clash near McCormick Place, Chicago Police Superintendent Garry McCarthy said at a news conference that the protests resulted in 45 people being arrested and four officers suffering injuries - one from a stab wound in the leg. Scroll down for video Clash: Demonstrators try to flee the police as they are move in on them

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was

HAYA NI MAKAO MAKUU YA MTANDAO WA Tigo TANZANIA DAR ES SALAAM

MAHALA yalipo ni Lugoda Street Gerezani Industrial Area , kwa sasa mdandao huu umefanya makubwa , kuna Tigo Bwerere Uilisha cheki hiyoooooo watu full kujiachia wana chonga tuu kwenye vyao vilonga.