Baraza la Maaskofu: Uwepo wa katiba inayotakiwa na wananchi katika Taifa lolote lile ndio msingi mzuri wa kujenga na kudumisha amani
Baraza
la Maaskofu nchini limesema kuwa uwepo wa katiba inayotakiwa na
wananchi katika Taifa lolote lile ndio msingi mzuri wa kujenga na
kudumisha amani yenye umoja na maelewano miongoni mwa wananchi.
Akizungumza
katika ufunguzi wa kongamano la kujadili katiba na amani lililoandaliwa
na kituo cha sheria na haki za Binadamu Naibu katibu Mkuu wa Baraza
hilo Padri Daniel Dulle amesema
kuwa amani hiyo inadumishwa kwa mazungumzo ya pamoja ili kuhakikisha
malengo na madhumuni ya kupata katiba mpya inayokidhi kiu ya watanzania
inapatikana kwa Amani.
Aidha
amsema kuwa kama wananchi wengi watakuwa na uhitaji wa kupata katiba
mpya ni vema mchakato huo ukiibuliwa upya maana katika katika katiba
iliyopendekezwa kuna mambo kadha wa kadha yalikuwa yameshaibuliwa
amabayo ni mazuri na yangeweza kutuliza kiu ya baadhi ya wananchi wengi
kwenye ushiriki wao katika shughuli zote za kijamii,kisiasa ,haki na
amani
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Anna Henga amesema
ingekuwa vizuri katiba mpya ikapatikana hata kabla ya uchaguzi Mkuu
mwaka 2020 kwa nia ya kumaliza changamoto zinazojitokeza kabla na baada
ya uchaguzi.
Naye profesa Mwesiga Baregu ambaye
alikuwa mjumbe wa tume ya mabadiliko ya katiba amesema kuwa kiporo cha
mchakato wa katiba mpya kilichobaki hakina budi kufanyiwa kazi na
hatimaye katiba mpya ambayo imesubiriwa na watanzania wengi iweze
kupatikana na kuwa chachu kwa maendeleo ya Taifa.
Comments