MSHINDI wa Kampeni
ya Daka Mkwanja iliyokuwa ikiendeshwa na Benki ya Afrika nchini(BOA ) Bw.Reuben Kinamhala mkazi wa Mwandege wilayani Mkuranga mkoani
Pwani,amekabidhiwa Sh. Milioni 10.
Makabidhiano hayo yamefanyika leoJijini Dar es Salaam ambapo Meneja wa
Masoko na Utafiti wa benki hiyo, Muganyizi Bisheko amesema kampeni hiyo ilianza
mwishoni wa mwezi Novemba mwaka jana na kumalizika Februari 26 mwaka huu huku
akisisitiza ililenga kusherehekea miaka 10 ya BOA tangu ianzishwe hapa nchini.
.Pichani ni Mshindi
wa Kampeni ya Daka Mkwanja, Bw. Reuben Kinamhala wa pili kutoka kushoto
akikabidhiwa Sh milioni 10 na Meneja Masoko na Utafiti wa Benki ya BOA,
Muganyizi Bisheko leo mchana Makao Makuu ya Benki hiyo Mtaa wa Ohio jijini Dar
es Salaam
"Mzee wa Kanisa la Fellowship Pentecostal Reuben ambaye ni Mteja wa Tawi la Mtoni wilayani Temeke
amejishindia Sh. milioni 10 za Daka Mkwanja na kuwa hali hiyo ni moja wapo ya fursa iliyojitokeza kwake kwa kuwa mteja wetu kuanzia mwaka 2016,”
amesema Muganyizi.
Muganyizi alibainisha kuwa kampeni hiyo ililenga kuwaongezea wateja
ufahamu na kutambua umuhimu wa kuhifadhi fedha zao benki na kwamba mteja alitakiwa
kuweka kuanzia Sh milioni moja kipindi chote cha kampeni.
BOA Bank imefafanua kuwa hivi karibuni itazindua kampeni
nyingine itakayowawezesha wateja zaidi ya mmoja kujishindia fedha , ikitarajiwa
kuanza Machi 7 hadi mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu.
Kwa upande wake, Reubeni ameishukuru
benki hiyo na kubainisha fedha hizo atatzitumia katika majukumumu ya kifamilia
ikiwemo kusomesha watoto shule na kukua kiuchumi pamoja na
kumsiadia mke wake katika shughuli zake za ujasiriamali.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mauzo cha benki hiyo, Linda Mario
amewaomba watanzania kujenga utamaduni wa kufungua akaunti kwa ajili ya
kuhifadhi fedha zao na usalama.
Amesema Bwana Reuben aliweka fedha kama kampeni ilivyoagiza
huku akibainisha hakutegemea kama angeibuka na mshindi.


Comments