TAARIFA za kuwepo kwa mgogoro kati ya kocha wa Manchester United, Jose Mourinho na kiungo mwenye thamani ya paundi 89 milioni, Paul Pogba zimetupwa kapuni na wakala wa mchezaji huyo Mino Raiola.
Wakala huyo maarufu amefunguka kuwa hakuna ‘vita’ yoyote inayoendelea baina ya watu hao ambayo inahatarisha mahusiano yao kazini.
Siku za hivi karibuni Mourinho aliamua kumtupa benchi Pogba huku tetesi zikisema kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 anaweza kuondoka klabuni hapo katika dirisha lijalo la usajili akitajwa kuelekea Real Madrid ya Hispania.
Comments