Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa onyo kwa Redio na vituo
vya runinga nchini kuhusu kupiga nyimbo za wasanii wa muziki ambazo
zinakiuka maadili ya mtanzania na vifungu vya sheria ya ya utangazaji.
Afisa Utangazaji TCRA, Rolf Kibaja
Akizungumza na waandishi wa Habari leo Machi 1, 2018 jijini Dar es
salaam, Afisa Utangazaji TCRA, Rolf Kibaja, amesema sheria na kanuni za
huduma ya utangazi zipo na lazima zifuatwe na kama kuna Media
itakayokiuka itachukuliwa hatua bila huruma.

Comments