Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini Danford Kitwana akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam kuhusu umuhimu wa kuzingatia maadili ya taaluma ya uwandishi wa habari ili kuepuka kuandika habari ambayo sio rafiki kwa jamii, Kitwana ni miongoni mwa wakufunzi katika Semina iliyoandaliwa na Tume ya Taifa UNESCO kwa ajili ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari.
Programu Afisa wa habari na Mawasiliano Tume ya Taifa UNESCO Lusajo Mwaiteleke akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu semina hiyo, ambapo ameeleza kuwa wameamua kunadaa semina ya madilii kwa wanahabari kutokana changamoto zilizopo katika tasnia ya habari ikiwemo kuripoti habari ambayo inakwenda kinyume na maadili.
Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini Danford Kitwana wakati wakiwa katika Semina iliyoandaliwa na Tume ya Elimu , Sayansi na Utamaduni wa Umoja wa Mataifa (UNESCO) jijini Dar es Salaam
Waandishi wa habari nchini wametakiwa kizingatia maadili ya taaluma zao ili kuandika habari zenye ukweli pamoja na kuwa na mslai mapana ya jamii na taifa jambo ambalo litasaidia kuongeza uweledi katika tasnia ya habari.
Hayo yamebainishwa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini Danford Kitwana wakati akitoa semina kwa waandishi wa habari kuhusu maadili ya taaluma ya uwandishi wa habari ambayo imeonekana kwa baadhi wanahabari kutozingatia na kusababisha kupungua kwa uweledi katika taaluma hiyo.
Kitwana amesema ni vyema waandishi wa habari kuzingatia maadili ya taaluma ili kuepuka migogoro ambayo inaweza kujitokeza baada ya kuripo taarifa zisizokuwa na maadili.
“Magazeti angalau wanajitaidi kutafuta usawa katika habari zao (balanc).. lakini tatizo lipo kwa kwenye radio na Tv, hivyo naomba tuzingatie kanuni na maadili ya uwandishi ili kuongeza kufanisi katika utendaji ” amesema Kitwana.
Amefafanua kuwa changamoto bado zipo katika tasnia ya uwandishi wa habari ikiwemo ukosefu wa mafunzo kwa waandishi, wahariri bora, ukosefu wa kipato cha kutosha kwa vyombo vya habari ambapo kwa namna moja au nyengine inaludisha nyuma maendeleo.
Programu Afisa wa habari na Mawasiliano Tume ya Taifa UNESCO Lusajo Mwaiteleke , amesema kwa sasa kumekuwa na ukuaji mkubwa hasa katika upande wa mitandao na kusababisha kuongezeka kwa changamoto katika tasnia ya bahari.
Amesema kuwa kumekuwepo na utoaji wa taarifa mbalimbali ambazo nyengine zinakwenda kinyume na maadili jambo ambalo UNESCO imeona ni vyema kutoa elimu ili kuongeza uweledi katika tasnia ya habari hapa nchini.
"Kupitia semina hii tunaamini waandishi wa habari wataripoti habari zao kwa kuzingatia maadili na kanuni na kuongeza uweledi pamoja na ufanisi na utendaji bora" amesema Mwaiteleke.
Kwa upande wao waandishi wa habari waliohudhuria semina hiyo wamesema wanashukuru kuandaliwa kwa semina hiyo kwani wamejifunza mengi na kuomba semina kama hizo kutolewa kila mara ili kuboresha tasnia ya habari nchini.



Comments