NEW YORK ,Marekani
MCHEKESHAJI Don Rickles,amewekwa chini ya ulinzi, baada ya kutoa kichekesho ambacho kinaonekana kumdhalilisha Rais Barack Obama kwa njia ya ubaguzi wa rangi.
Kwa mujibu wa mtandao wa Dital Spy, muigizaji huyo wa vichekesho alitiwa mbaroni mwishoni mwa wiki iliyopita wakati tamasha lililoandaliwa na taasisi ya filamu ili kumpa tuzo muigizaji, Shirley MacLaine.
Kwa mujibu wa waandishi wa habari wa Hollywood ,muigizaji huyo alijikuta akiingia matatani baada ya kupewa nafasi ya kutoa neno kumpongeza, MacLaine ambapo alijikuta akitania akisema kwamba :"Mimi sipaswi kufurahi na watu weusi,Ila Rais Obama ni rafiki yangu na jana alikuwa nyumbani kwangu lakini sikumkaribisha.."
Katika tamasha hilo Rickles anaripotiwa kuwashambulia pia nyota wengi akiwamo Jack Nicholson na kaka yake MacLaine, Warren Beatty.
Pia ilielezwa kuwa alichukua muda akimponda Jennifer Aniston, akidai kuwa mwanadada huyo siku moja alikimbia meza yake wakati wakiwa kwenye mgahawa mmoja jijini New York kwa sababu alikuwa katikati ya joto la mashoga.

Comments