Skip to main content

Jalada lakwamisha kesi ya Lulu


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Kisutu Dar es Salaam jana ilishindwa kuendelea kusikiliza kesi ya tuhuma za mauaji inayomkabili msanii nyota wa filamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' kutokana na kutokuwepo kwa jalada halisi la kesi yake.
Lulu (17) alifikishwa katika mahakama hiyo kama kawaida, lakini hakupandishwa kizimbani kutokana na jalada la kesi hiyo kupelekwa Mahakama Kuu.
Msanii huyo aliwakilishwa mahakamani hapo na wakili wake, Peter Kibatala anayemtetea.
Wakili wa serikali, Keneth Sekwao alidai kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika, ambapo aliomba ipangwe tarehe nyingine ya kutajwa.
Kufuatia ombi hilo, Hakimu Mkazi Augustina Mmbando anayesikiliza kesi hiyo, alisema itatajwa tena Julai 2 mwaka huu.
Lulu alifikishwa mahakama hapo saa tatu asubuhi akiwa katika gari la magereza. Ilipofika saa nne, Lulu aliondolewa mahakamani hapo akiwa katika gari la magereza na kuwaacha hoi waandishi wa habari waliokuwa wakimsubiri ili waweze kumpiga picha.
Habari za kuaminika zilizopatikana mahakamani hapo zilidai kuwa, baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, kutoa uamuzi wa kuchunguza umri wa Lulu, kila kitu kilisimamishwa kwa vile jalada halisi halipo.
Kwa mujibu wa habari hizo, kabla ya uamuzi wa Mahakama Kuu kutolewa, kesi hiyo ilipangazwa kutajwa jana na kwamba kwa kawaida, baada ya uamuzi huo, Jaji anayesikiliza maombi ya uchunguzi wa umri wa msanii huyo alipaswa kumwandikia barua Hakimu Augustina ili kumweleza kuhusu kusimamishwa kwa kesi hiyo mahakamani hapo.
Habari hizo ziliendelea kudai kuwa, hakimu anayesikiliza kesi hiyo alipaswa kupewa nakala ya uamuzi huo na kwamba mshitakiwa hakupaswa kufikishwa mahakamani hadi uamuzi kuhusu utata wa umri utakapotolewa.
Jaji Fauz Twaib wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam anatarajia kutoa uamuzi kuhusu utata huo wa umri Juni 25 mwaka huu.
Awali, Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu ilikataa ombi la upande wa utetezi la kutaka ufanywe uchunguzi kuhusu umri sahihi wa Lulu.
Kwa mujibu wa hati ya mashitaka, Lulu anadaiwa kuwa Aprili 7 mwaka huu, eneo la Sinza Vatican, Dar es Salaam, alimuua msanii mwenzake, Steven Kanumba.
Marehemu Kanumba alizikwa Aprili 10, mwaka huu kwenye makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam katika mazishi, ambayo yalihudhuriwa na maelfu ya watu, wakiwemo viongozi wa serikali. Inatoka kwa  mdau.

Comments

Popular posts from this blog

MBINU ZA KUMFIKISHA MWANAMKE MWENYE MAKALIO MAKUBWA KILELENI KWA HARAKA

Kwa kawaida wanawake wanafikia kilele (mwisho wa utamu wa ngono) kati ya dakika ishirini na saa moja, yaani kwa kifupi inawachukua muda mrefu sana hali inayopelekea mpenzi mvivu kuchoka na ufanyaji wake utakuwa wa “ovyo” hali itakayo kufanya wewe kuishiwa na hamu ya kuendelea. Pamoja na kuchelewa huko ambako kunatokana na utofauti wetu kati ya mwanaume na mwanamke lakini nakumbuka hapo nyuma nilikutana na wanawake 2 waliokuwa ndani ya ndoa na wamezaa lakini hawajawahi kabisa kujua utamu wa tendo hilo alimaharufu kama “kufanya mapenzi”. Natambua kuwa ni ngumu au niseme si wanawake wote ambao wamejaaliwa kimaumbile kwamba wanafanikiwa kufika kileleni zaidi ya mara mbili kila wanapofanya mapenzi/ngono (kumbuka ni kati ya dakika 15 na saa moja hivyo Jibaba hapa awe na uwezo wa kujizuia kwa zaidi ya dk 45) na ikiwa jamaa ni “mzamiaji” basi unaweza ukaondoka na goli 3 ktk mzunguuko mmoja. Lakini kwa nini basi baadhi yao tu ndio wafike kileleni na wengine was...

Mushikiwabo to UN: Enhance civilian protection

By Eugene Kwibuka Rwanda’s Minister of Foreign Affairs and Cooperation has urged the United Nations Security Council (UNSC) to invest more energy in the prevention of conflicts for better protection of civilians living in conflict-torn areas. Rwanda’s Foreign minister, Louise Mushikiwabo Louise Mushikiwabo made the call during an open debate on the protection of civilians in armed conflict which the UNSC held in New York on Tuesday. “Rwanda’s core message today is that enhancing the protection of civilians in armed conflict requires action before a conflict starts. The proliferation of non-state armed groups makes civilian protection both more urgent, and harder to achieve,” she said. For better protection of civilians in armed-conflict areas, the minister emphasised the need to increase investments in professionalising the military and police forces through adequate training. “Only when the leadership of armed forces shares the international...

Saudi King urges U.N. action against religious insults

Saudi King Abdullah urged the United Nations to produce a resolution condemning insults on monotheistic religions after the anti-Islam film in the U.S. that sparked deadly protests in many Muslim countries last month. (AFP) By AFP, MINA/SAUDI ARABIA Saudi King Abdullah on Saturday demanded a U.N. resolution condemning insults on monotheistic religions after a low-budget film produced in the U.S. sparked deadly protests last month. “I demand a U.N. resolution that condemns any country or group that insults religions and prophets,” he said during a meeting at his palace with religious figures and heads of hajj delegations in the Mina valley where pilgrims were performing final rituals of hajj. “It is our duty and that of every Muslim to protect Islam and defend the prophets.” A low-budget film produced in the U.S., Innocence of Muslims, triggered a wave of deadly anti-American violence last month across the Muslim world targeting US symbols ranging ...